Notifications
  • MY DIARY (17)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA SABATULIPOISHIA...Nilijifikiria mara mbili nikajikuta namkubalia kwani alionekana ni mpole na mstaarabu sana.Basi tukaenda hadi kwake ambapo haikuwa mbali na hapo tulipokuwa na kweli alikuwa na chumba na sebule na sebuleni kwake niliona picha ya ukutani akiwe yeye na mke wake nahisi ilikuwa siku ya harusi yao.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nikasema huyu kijana atakuwa amefunga ndoa…
  • MY DIARY (16)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA SITATULIPOISHIA...Mwanamke akaamua kuingia jikoni na kukarangiza viazi na nyama rosti na kilipoiva kililetwa mezani tukaendelea kujenga afya. Sikuaamini kama Joyce alikuwa anakumbuka hata kupika kwa sababu alibadilka sana na alikuwa akiishi maisha ya starehe.. Lakini aliniprovu wrong kwa kutoa rost ya hatari.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Baada ya kula alinambia kuwa alikuwa amechoka…
  • MY DIARY (15)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA TANOTULIPOISHIA...Hapo mzungu wa watu hakuweza kuvumilia tena aliichomeka yote.Mmmmmh mmmmmh ishiiiiiiiiiiii yeaaaaaahhhhhhhh yeaaaaaaah ni miguno niliyoitoa mara baada ya kusikia joto tamu la kiungo hicho.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Ikabid nijivute kwa nyuma ili lengo likiwa ni kukaa vizuri ili kichwa cha nyoka kiwe juu juu ya pango langu ili niweze kukisugua sawa sawa na pia…
  • MY DIARY (14)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA NNETULIPOISHIA...Nikamuuuuliza hivi wewe haugopi maradhi? Akanijibu kuwa angekuwa haogopi basi angeshakufa. Sikiliza Leah hapa nipo na vile vipimo vya ukimwi hivyo usiwe na wasiwasi tutapima wote wanne kama wapo fresh tutaingia kazini wewe si unatafuta hela ya kujiunga na chuo au?IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Kabla sijajibu akanambia nitakupa na dawa ya kumeza ya kuzuia mimba na pia…
  • MY DIARY (13)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA TATUTULIPOISHIA...Joyce akaanza kujimiminia mwenyewe, kweli dunia ina mambo wakati wenzake wakichanganya nay ale maji makubwa yeye alikuwa akinywa kavu kavu.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi mimi sikuwa na jinsi zaidi ya kuaagiza ile bia yangu ambayo alinifundisha yaani savanna. Safari hii hakusubiri ili ifike mwisho ili anitambulishe bali tulivyoanza tu kunywa akawaambia wale…
  • MY DIARY (12)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA MBILITULIPOISHIA...Niliamua kufanya ziara ili nijue pakoje na mwisho wa siku niliamini kuwa kutokana na umaarufu wa marehemu baba yangu isingekuwa kazi sana kulipata shamba lake..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi nilitembea kijiji hadi kijiji huku nikijaribu kuuliza kwa wenye viti wa mtaa kama walikuwa wakimjua marehemu Bura. Kwa kweli kazi ilikuwa ngumu sikuweza kuvimaliza vijiji…
  • MY DIARY (11)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA MOJATULIPOISHIA...Wakati akiongea maneno hayo mara mtarimbo ukaanza kusimama nikajisemeha nimeshakosea nilitakiwa niondoke nilivyoona kimelele tu, nikajua hapo lazima atanitafuuna bila huruma. Basi akaingia bafuni akachukua sabuni akajipaka ili kujisisimua ngoma isimame vizuri.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Yaaani nilichanganyikiwa na huko bafuni nilisikia maneno ambayo yalinichekesha…
  • MY DIARY (10)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMITULIPOISHIA...Nikamwambia Joyce ndo maana mimi nakupendaga. Nikamwambia “nitakuapa feedback ngoja nimpigie asije akaja na makufuli yake leo hii. Nikampigia baba mwenye nyumba eti kwa kujiamini kabisa akapokea nakusema “ Halow mrembo” Nikamwambia Yes mpenzi kitu ambacho kilimfurahisha sana..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Kuokoa hela ya vocha nikamwambia nimekubali ombi lako alafu nikakata…
  • MY DIARY (9)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TISATULIPOISHIA...Basi Dj wangu aliendelea na mautundu yake akaniwekea mambo ya pwani na hapo ndipo uvumilivu ulipomshinda akaja kunibambia na mimi sikuona haja ya kumbania kwa kuwa ni mali zake mwenyewe. Nilizungusha nyonga na kiuno mpaka nikachoka nikajitupa kitandani ili nipumzike. Nafsi yake ilikuwa imeridhika kwani hakutka tena penzi bali alichukua lap top yake na kuanza kunionesha picha na vitu vingine ambavyo vilinipa raha.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA…
  • MY DIARY (8)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA NANETULIPOISHIA...Sijui hata haya maneno yalitoka wapi, fahamu zilinitoka na Ticha aliamua kuninyanyasa maana nilishajikojolea zaidi ya mara tano. Basi na yeye kwa kutafuta mbwembwe alianza yale mambo yao ya katerero, siunajua tena mwalimu John alitokea pande za Bukoba.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alinichezea sana na baadaye nilishangaa kukuta jamaa ameshaingiza kunako. Sikujielewa kwa…

SHETANI ALINIITA KUZIMU (3)


SEHEMU YA TATU
TULIPOISHIA...
Akiwa ametulia alisema; “Nimefika hapa baada ya kuitwa na nyinyi, naomba mniambie kinachowasibu ili niwasaidie kisha nirudi kwenye makazi yangu.”

KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA CnZ Media APP INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
Baada ya kutoa kauli hiyo, yule dogo alijongea mbele ya malkia na kumsujudia na kumwambia alimwita kwa sababu katika himaya yao walipata mgeni.

Kufuatia kuambiwa hivyo, malkia alitikisa kichwa na kuuliza; “Huyo mgeni yupo wapi?” Alipouliza hivyo, dogo alimuonesha kwa kidole nilipokuwa nimekaa ndipo

malkia alitikisa kichwa kuonesha alifurahi. “Kwahiyo mlitaka nimfahamu mgeni wetu?” alimwuliza yule mtoto mchawi. Dogo alimwambia licha ya kumfahamu

walihitaji nipewe nguvu ili nianze kufanya kazi ya kichawi kwa sababu tayari nilikwisha kabidhiwa mkoba wa bibi yangu.

Yule dogo alipotoa kauli hiyo, malkia aliinama sijui alifanyaje nikashangaa kuona mkia wake umenifikia, ukaanzaa kunipigapiga mwilini na kichwani. Wakati

nikipigwa na mkia huo, mwili ulinisisimka na kujikuta nimepata nguvu nyingi za kichawi, lakini kabla malkia hajaondoka aliniambia kuanzia siku hiyo niombe

kitu chochote nitapata. Baada ya kutoa kauli hiyo kilitokea kimbunga, kufumba na kufummbua, malkia alitoweka na kimbunga kikakoma.

Tukio hilo liliwafurahisha sana wachawi wenzangu ambao walirukaruka huku na huko na kuanza kuimba nyimbo hadi walipoamriwa kutulia na yule dogo. Kwa kuwa

nilikuwa nimechoka sana na niliambiwa nikitaka kitu chochote niombe kitakuwa, nikaomba utokee ungo ‘ndege’ya wachawi. Niliamua kuomba usafiri huo kwa sababu

nilikuwa nimechoka sana na nilihitaji kurudi nyumbani, nikasema: “Ungo tokea!”

Kwa mara ya kwanza niliamini kweli uchawi upo na ulikuwa na nguvu, ungo niliouomba ulitokea na kuja kutua mbele yangu. Wachawi wenzangu walinishangilia sana,

nilichokifanya kabla sijapanda na kuanza safari nilikwenda kuchukua mkoba wa kichawi wa marehemu bibi yangu.

Nikiwa na mkoba huo nilikaa ndani ya ungo na kutamka maneno haya: “We ungo naomba unirudishe nyumbani kwetu kwa sababu nimechoka sana.” Baada ya kutoa kauli

hiyo, kilitokea kimbunga kikauzoa ule ungo na kuupaisha juu, katika hali ya kushangaza nikauona ukitua juu ya nyumba yetu. Bila ya kuelekezwa na mtu,

niliteremka na kwenda kwenye pembe ya ukuta nikapitia na kuingia chumbani kwangu. Kwa kuwa ilikuwa ni usiku sana, hakuna aliyenishtukia nikauchukua mkoba wa

bibi na kwenda kuuweka chini ya kitanda ambako ilikuwa vigumu kuonwa na watu wengine.

KWA kuwa ilikuwa usiku sana, baada ya kuuficha mkoba huo sehemu ambayo ilikuwa siyo rahisi mtu mwingine kuuona, nilipanda kitandani nikalala. Haukupita muda

mrefu nilipitiwa na usingizi mzito, kufuatia uchovu niliokuwanao nilala hadi saa nne asubuhi ambapo niliamka. Baada ya kunawa usoni, nilichukua jembe na

kuanza kuelekea shambani. Nikiwa sijafika mbali, nilimuona baba mdogo aliyekwenda shamabi alfajiri akirudi.

Nilipokutana naye hata bila ya salamu aliniuliza nilikuwa nakwenda wapi muda ule, nilimfahamisha shambani. Baada ya kumpa jibu hilo, aliniuliza muda ule

ilikuwa saa ngapi nikwambia saa nne, kwa hasira alisema; ‘mpumbavu sana wewe,huu ndiyo muda wa kwenda shambani? Haya rudi nyumbani.’ Nilipobaini baba

alichukia, nilirudi nyumbani nikaweka jembe. Kwa kuwa sikuwa na kazi nyingine niliingia chumbani ambapo nililala hadi saa sita na nusu mchana nikaamka ili nipike.

Kabla sijaanza mapishi niligundua ndani hakukuwa na maji ndipo nilikwenda kisimani ambako nilikuta kuna umati wa watu wakisubiri kuchota maji. Kufuatia shida

ya maji, nilikaa huko hadi saa kumi jioni nikarejea nyumbani. Baba mdogo alichukizwa sana na kitendo cha kuchelewa kurudi. Aliponiuliza nilichelewa wapi,

nilimfahamisha jinsi kisimani kulivyokuwa na watu wengi, hakunielewa akaanza kunifokea kwamba nilikuwa ninacheza. Kwa hasira alizokuwanazo alichukua fimbo na

kuanza kunitandika sehemu mbalimbali, nilipata maumivu maka sana,

Alipomaliza kunicharaza bakora aliniambia nikachukue mpunga ndani kisha niutwange kwa ajili ya mlo wa usiku. Kwa kuwa ndani hatukuwa na kinu, nilikwenda

kuazima kwa jirani yetu kisha nikaanza kufanya kazi hiyo. Kawaida unapotwanga mpunga lazima utamwagika chini, wakati nikiendelea na zoezi hilo kwa bahati

mbaya ulimwagika. Baba aliyekuwa ameketi alipoona mpunga umemwagika alikasirika ambapo alinifuata na kunizaba kibao ambacho kilinichanganya akili.

Kitendo hicho kilinikera, nilimwambia kwamba nilimvumilia sana na kufikia kikomo hivyo lazima nitamkomesha. “Wewe mtoto unasemaje… utanikomesha mimi… kweli wewe ni mwenda wazimu,”

Kutokana na hasira nilizokuwanazo, nilimwambia ile nyumba yake ataiona chungu na kukimbia kwani nilikuwa nimechoshwa na tabia yake ya kunipiga bila sababu.

Nilipomwambia hivyo alisema ataona kati yake na mimi nani mjanja na kuniambia nimuombe msamaha kwa kauli yangu, nikamwambia sitamuomba na kusisitiza lazima

ataikimbia nyumba yake. Baada ya kumwambia hivyo, niliacha kutwanga mpunga na kuingia chumbani kwangu, ile naingia nilishangaa kukuta chumba chote kikinuka

harufu ya bangi. Kule kwetu tunaziita "NJEMU"

Moja kwa moja nilijua aliyevuta bangi alikuwa ni yule ndugu yangu tuliyekuwa tukilala pamoja, nikachukia sana. Kukufafanulia ni kwamba hakuna kitu ambacho

akipatani na wachawi kama harufu ya bangi, nilifungua dirisha na mlango ili harufu itoke nje. Kwa hasira nilizokuwa nazo, nilipanga kumkomesha ndugu yangu huyo.

KWA hasira nilizokuwanazo, nilipanga kumkomesha ndugu yangu huyo ambaye sikuelewa alikuwa amekwenda wapi, nikaamua kumsaka kwa kutumia darubini ya kichawi.

Kukufafanulia hapo ni kwamba wachawi wana vifaa vyao maalumu vya kuwaangalia maadui zao walio mbali, baada ya kumwangalia nilimuona amekaa maskani akicheza

bao. Nilichokifanya nilichukua ule mkoba wangu wa kichawi nikachanganya ndumba kama nilivyofundishwa nikamuweka roho ya kupakimbia pale nyumbani, yaani tangu siku ile asirudi tena.

Baada ya kufanya uchawi huo, nilitoka na kuendelea kufanya mambo yangu huku nikiwa na hasira kufuatia baba mdogo kunipiga bila sababu. Hata hivyo, nilipanga

kumhamisha pale nyumbani baada ya kupita siku sita, kwa upande wa yule kijana ni kweli hakurudi nyumbani na tulipokutana njiani alinichangamkia kwa furaha

kuliko zamani. Nilipomwuliza kwa nini hakupenda kurudi nyumbani, akaishia kucheka na kunieleza kwamba aliamua tu mwenyewe.

Kumtega nilimwuliza kuhusu kuja kuchukua nguo zake, akaniambia alikuwa na zingine, nikajua uchawi wangu ulifanya kazi. Niliishi na baba mdogo kwa chuki hadi

ilipofika siku ya tano ndipo niliamua kumkimbiza pale nyumbani ili nipamiliki.

Usiku wa manane kukiwa kimya muda ambao wachawi huwa huru kufanya mambo yao, niliamka na kutengeneza ulosi kisha nilinuiza kwamba baba mdogo aondoke na

asirudi tena. Nilipomaliza, nilimfuata kiuchawi chumbani kwake na kumuwekea roho ya kuikimbia nyumba yake kisha nikarudi kulala chumbani kwangu. Kulipokucha

niliamka na kumkuta baba mdogo akiwa anaota jua la asubuhi, aliponiona alinichangamkia sana tofauti na siku nyingine tangu tulipokorofishana.

“Kaloli mwanangu umeamka salama?”

Aliponiuliza hivyo nilimwambia nilikuwa mzima wa afya ndipo alinieleza kwamba alihitaji kuzungumza na mimi, nikamwambia sawa. Baba mdogo aliniambia kwamba

nitakapomaliza kazi zangu ndipo tutaongea, nikamwambia hakukuwa na shida. Kama tulivyokubaliana, baada ya kumaliza kazi nilimfuata baba mdogo ambaye siku

hiyo hakwenda shambani ndipo alinifahamisha kwamba alikuwa anataka kuhamia kwao.

Alipotoa kauli hiyo nilifurahi sana kwani nilijua uchawi wangu ulifanya kazi, nikamwuliza kwa nini aliamua kurudi kwao na pale atapaacha na nani! Baba

aliniambia kwamba nyumba na kila kitu kilichokuwepo pale vitakuwa mali yangu, moyoni nikasema; ‘mimi si nilikuambia utaikimbia nyumba yako ukabisha…mimi

ndiyo Kaloli!’ Kumdhihaki nilimchimba anieleze sababu iliyomfanya aondoke, akaniambia alichoka tu kukaa pale hivyo aliamua kwenda kuishi na wazazi wake.

“Hivyo ndivyo nilivyoamua, nikiondoka sitarudi tena hapa…huu mji nimekuachia na hakuna mtu atakayekusumbua,”

Baada ya baba kuniambia hivyo, nilimuuliza alitarajia kuondoka lini, akasema siku iliyofuata asubuhi na mapema. Kauli hiyo ya baba ilinifurahisha sana kwani

nilijua muda wa kujitawala pale nyumbani uliwadia, jioni ilipofika baba aliniita na kuniambia kwamba ilitokea ghafla tu kupachukia sana pale alipokuwa akiishi.

Nilipomuuliza sababu za kupachukia alisema sijui anapaonaje ni heri arudi akaishi na wazazi wake, nikamwambia ulikuwa uamuzi wa busara.

Siku iliyofuata baba akiwa na furaha aliniaga ambapo nilimsindikiza akaondoka akiwa na begi la nguo tu, huku nyuma nikajisifu kwa kumkomesha. Kukufafanulia

hapo ni kwamba wachawi huwa hawana huruma wanapoamua kumroga mtu, huwa hawajali kama mtu husika ni mzazi au ndugu yake wa damu. Baba alipoondoka kwa furaha

niliyokuwa nayo, nilimchinja kuku kisha nilimchoma na kumla ikiwa ni kujipongeza kwa kumuondoa pale nyumbani kwa sababu ndiye alikuwa kikwazo.

Kwa kuwa nyumba ilikuwa kubwa, siku ya pili nilimtafuta dalali na kumwambia anitafutie wapangaji wanne, ambapo walipatikana watatu. Wapangaji hao wakiume

walikuwa na wake zao ambao walikuwa wazuri sana, baada ya kupita siku mbili yule dalali alimleta dada mmoja mzuri ambaye hakuwa na mume, nikampangisha chumba

kilichobaki. Nilipoishi na wapangaji hao kwa muda wa miezi minne ndipo niliamua nianze kuwawangia usiku, lengo langu lilikuwa ni kuwadhibiti kwa kila kitu.

Mpangaji wa kwanza kumchezea alikuwa wa chumba cha tatu kushoto kutoka nilichokuwa nalala aliyekuwa na mke mdogomdogo mzuri.

Nakumbuka siku hiyo usiku wa manane, niliamka kichawi yaani nikiwa sina nguo mwilini na kuingia katika chumba cha wapangaji hao. Baada ya kuingia niliwakuta

wakiwa wamelala, nilimtia roho ya usingizi yule mwanaume kisha nikambeba na kumlaza chini akiwa hajitambui. Akiwa amelala fofofo, nilipanda kitandani na

kuanza kufanya mapenzi na mkewe hadi niliporidhika ndipo nilimbeba yule mwanaume na kumlaza kitandani kisha nikamtoa ile roho ya usingizi.

Baada ya kufanya hivyo, nilirudi chumbani kwangu nikajilaza kitandani nikiwa mwenye furaha kufuatia kitendo nilichomfanyia yule mke wa mtu. Kwa kuwa usiku huo nilikuwa na hamu sana ya kula nyama, sikuweza kupata usingizi kabisa, nikaamua kuiita ndege ya kichawi (ungo). Baada ya kufanya hivyo, hazikupita dakika nyingi nikasikia kitu kimetua sakafuni tii, nilipoangalia niliuona ungo.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
58 Shetani Aliniita Kuzimu Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni