MTAA WA TATU (47)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA AROBAINI NA SABA
Watu walikunywa pombe na kusikiliza nyimbo za maombolezo, Yani kwaya, ndani ya
Usiku huo mwanaume akatoka na kwenda sehemu moja hivi
Ndani ya clab
Kulikuwa na zinga la part watu wakipari na kuchizika yote ni kupoteza stress
NIOMBE SAPOTI, BONYEZA TANGAZO LINALOKUJA NA KUJAA KWENYE SIMU YAKO WAKATI UKIFUNGUA SIMULIZI AU LILE LINALOKUWA KATIKATI YA SIMULIZI ZETUKABLA HAUJAIFUNGUA NDANI, PIA KUNA LILE LINAKUJA NA KUNG'ANG'ANIA HAPO CHINI, BONYEZA WALAU MARA 3-4 HIVI HIYO NDIO SAPOTI YAKO KWANGU, TAFADHALI NIPE NGUVU NAKUTEGEMEA SANA MSOMAJI WANGU
SASA ENDELEA...
Hafidhi akaingia na kwenda kukaa pembezoni kabisa na mlango wa kuelekea chooni,
“mambo vipi?"
Kuna binti mrembo wa haja yani kimuonekano tu unaweza kusema huyu ndio mshindi wa
Mashindano ya warembo duniani.
Sura yake ya duwara iliyopendezeshwa na macho yake makubwa kidogo puwa iliyochongoka kama vile msomari
Midomo mipana yani ongea yake utasema ni mvivu wa kuongea.
Kumbe walaa kifua chake kilichobeba vichuguu viwili viliweza kuchomoza vyema kwenye kitop chake.
Wakati kiuno utasema sijui nini
Binafsi alikuwa na kila sifa ya kuitwa miss dunia.
Ndio aliyemtolea salamu
Hafidhi, kwanza akamtizama yule binti juu chini pasipo kuitikia,
“samahani kaka yangu nilikuwa nakusalimia tu kama hautojali wacha mi niende"
Bibiye akaongea hivyo na kugeuza kurudi alipotoka,
Hafidhi akabaki kutabasamu tu, na kumsindikiza kwa macho
Binti yule mwenye mwendo kama twiga chini alikuwa kavaa sketi iliyo muishia
Mapajani, viatu vya mchuchumio yani kila hatuwa aipigayo vinatowa mlio fulani wenye kupendeza.
“vipi Mona Risa yule mkaka umeongea nae chochote?"
“hapana hakuweza kuitikia hata salamu yangu ndio kwanza kaninyamazia kimya, nikaona isiwe shida wacha niondoke asije akaniona
Malaya bure"
“duhuu yani shost!
Na urembo wote uliokuwa nao jamaa hakuitikia salamu kweli?"
“ndio hakuitikia,
Wakati wanaongea ghafla kuna washikaji wakaingia ndani ya ukumbi huo mmoja wapo alikuwa
Steven kama unamkumbuka ndio aliyemuuwa Yusra na mke wa Raisi,
“oyaa kaka Steven cheki totozi zile"..
Steven akatizama sehemu anayo
Onyeshewa hizo totozi na kusema
“ndio kaka nimeziona sema kama ujuavyo hiyo sio Starehe yangu
Kama vipi wee nenda tu"..
Basi wakagongesheana mikono na kujigawanya, jamaa kufika tu akamshika bibiye kiunoni,
“wee mkaka nini jamani embu niache"..
Mona Risa akahitaji kujitowa mikononi mwa yule kijana.
Sema jamaa alikuwa kamganda kama ruba,
“tulia bibiye tambuwa hapa upo kwenye mikono salama,
Ghafla jamaa kabla hajaongea sana kwa kujinadi akapigwa kifuti cha shavuni akayumba na kwenda chini
Aliyefanya kitendo hiko alikuwa mwenzake
Mona Risa, jamaa akainuka na kumuona binti mwingine kamsimamia mbele.
“nani kanipiga? Nauliza nani anatafuta matatizo?"
Kusema kweli ndani ya ukumbi huo sauti ya mziki ilikuwa kubwa sana kama sauti ya jamaa haikuweza kusikika kwa yeyote ilikuwa kama vile kanong'ona tu.
Jamaa baada kuona kila mtu yuko bize hakuna wakumjibu, akamsogelea yule binti
Aliyesimama mbele yake
“wee Malaya embu nipishe"
Akafanya kama kumuweka pembeni hivi kitendo bila kuchelewa vifuti na viwiko
vya harakaraka vikaanza kutuwa mwilini mwa jamaa
Hakika binti alikuwa akipiga style za Montai kutoka kule nchini Thailand utasema kazaliwa nazo.
Jamaa hakuweza kuhimili kipigo kile na kujikuta akitupwa kulee
Akaenda kudondokea kwenye meza.
Watu ukumbini wakashituka kumbe kuna ugomvi ahaa,
Wenzake na jamaa wakaja mbio na kumshika mwenzao
“Dick kuna nini kimekutokea?"
Ndio kauli aliyoulizwa yule jamaa akiwa chini hajiwezi hata kunyanyuka utasema mlevi wa chang'aa, akabaki kuonyeshea kidole
kisha akawa kimyaa,
“yani wewe binti ndio umempiga huyu
yani hujitakii mema kabisa, subiri tukufunze adabu japokuwa nyie ndio Mama zetu Dada zetu Shangazi zetu na Bibi zetu Wake zetu
sema kwahili haina jinsi tunakuchapa tu,
si akasogea mmoja wao na kufanya kumpiga kibao cha shavuni,
Binti akarudi nyuma kwa kukwepa huku akiruka juu kidogo na kumkita kifuti cha kifua yule jamaa
akayumba na kucheuwa damu,
wakaona isiwe shida kumbe binti anajifanya kujuwa wacha wamchangie wakaenda kumvamia kwa pamoja
hakika bibiye alikuwa fiti maana aliweza kuwatandika wote ndani ya dakika saba hakuna aliyeweza kuamka,
wakati yote yakifanyika
Steven alikuwa yupo kwenye chumba kimoja hivi akiongea biashara hakuweza kutambuwa kama huku nnje kimenuka kwa upande wa wenzake,
Hafidhi aliweza kushuhudia mwanzo mwisho na kuishia kutabasamu tu,
Steven nae ndio anatoka kwanza akabaki kushangaa na kwenda kumshika yule ambaye alikuwa akiugulia maumivu pale chini,
“Seif kitu gani kimetokea ndugu nani katenda haya?"
Basi kijana Seif akanyoosha kidole kumuonyeshea yule
binti kwanza Steven akatabasamu na kumfata bibiye
“wewe ndio umetenda vile?"
Wewe ndio umewapiga ndugu zangu? Nijibu mbona uko kimya"...
Steven akang'aka kwa sauti kubwa yenye kuchanganyika na hasira fulani sema maswali yake
yakajibiwa kwa kupigwa teke na kurudishwa nyuma kwa kuyumba,
Kwanza akacheka na kujifuta ile sehemu kwa dharau kisha akasema
“mtoto akililia wembe mpe achezee ukimkata ndio atajuwa basi akaja kwa speed
Na kuzunguka utasema kafungwa kamba ndio anavilingishwa kumbe ni moja
kati ya style
Binti akajikuta anakumbwa kwa kupigwa mateke ya haraka akarushwa na kwenda kudondokea Kaunta
Chupa na glass za vinywaji pengele
sema bibiye akainuka na kuitaji kujibu mapigo mbele ya Steven kijana mwenye dharau hakuweza kufuwa dafu alipiga style zake za Montai ndio kwanza
Mwanaume alizitowa kwa dharau na kumpiga ngumi za mbavu,
Binti akadebweda ghafla akaingia binti mwingine ambaye ni Mona Risa
Steven akatupwa kule baada tiknik za ajabu kutuwa usoni mwake.
Hakika kilikuwa ni kitendo cha ghafla sana kwa yeye kufanyiwa vile, akiwa bado kalala chini Mwanaume
akachumpa na kusimama juu kisha akacheka kwa dharau. Wakati mapigano yakiendelea huku ukumbini
kwa wakati huo Hafidhi alikuwa ameingia kwenye kile chumba ambacho kijana Steven alitoka “wee nani
umefata nini ndani ya chumba changu?’’ Aliuliza swali mzee wa makamo hivi, dakika chache zilizopita
alikuwa akizungumza na Steven, “tulia hivyohivyo nyau mweusi wee ukisema uneng’eneke nitakata
kichwa chako, sasa naitaji uniambie wenzako wameenda wapi?’’
“Shatapu wacha kunitisha wee mtoto wa kahaba mzoefu, hivi unatambuwa kama mama yako nilikuwa
nashika makalio yake na kuyafinyaaa ghaaa Mzee akashindwa kuendelea kuongea baada jambia kupita
shingoni mwake damu zikamchruzika kwa wingi na kudondokea kwenye meza.
“shenzi zako yani umtusi mama yangu kiboya hivi sasa wape salamu zao kuzimu, Mwanaume akaongea
hivyo huku akilifuta damu lile jambia kwenye suti ya Mzee kisha akabeba brifcasi na kutoka zake kama
vile sio yeye wakati huku ukumbini kulikuwa kumenoga balaa yani ilikuwa piga nikupige baina ya Steven
na bibiye Mona Risa watu wakabaki kushangilia tu, kusema kweli bibiye alikuwa yuko fiti si mchezo
Steven kijasho kilimtoka na kujiambia kapata mpizani wa kweli ilibidi Steven atumie ujanja fulani baada
kujisachi mfukoni na kutowa kichupa kidogo wakati bibiye Mona Risa kakunja ngumi akashitukia vitu
kama chembechembe za unga hivi vikituwa machoni kwake, sekunde si nyingi akapoteza uwezo wa
kuona Steven akaitumia nafasi hiyo kumpiga kama kawaida yake jamaa akizidiwa anakuwa na hasira
akakishika kichwa cha bibiye na kutaka kumnyonga kabla ya kufanya hivyo kuna Mwanaume wa shoka
akaja kuokowa jahazi kwa kuruka teknik ya maana yani kile kishindo cha mateke kutuwa kifuani kwake
kilimfanya Steven atupwe mbali na pale akaitaji kunyanyuka akashindwa na kuishia kujishika sehemu ya
moyo, na kucheuwa damu Mona Risa akaweza kufumbuwa macho baada kumwagiwa maji usoni si
akachenji kwa kutaka kupigana na Hafidhi pasipo kutambuwa ndio aliyeweza kumpatia msaada,
mwenzake akawai kumshika kwa kumwambia
“Mona embu tulia huyu mkaka ndio kakusaidia’’ Hafidhi hakutaka kuongea sana akalifata brifcase lake
na kuondoka zake, “Suzan mbona bosi hapokei simu?’’ mmoja kati ya wahudumu alimuuliza mwenzake
“kama vipi nenda kamtizame maana huku kushavurugika mwambie aje ajionee hali harisi’’ basi Suzan
akatoka na kuelekea chumbani kwa bosi wake, akabisha hodi baada kufika mlangoni hapo, sema kukawa
kimya hakuweza kuitikiwa richa ya kupaza sauti kuita akabaki kujiuliza sijui huyu bwege atakuwa yupo
na malaya gani kudadeki zake asitake kunifanya mimi kama mtoto mdogo. Si kaniambia mimi ndio wa
pekee juu yake. Baada bibiye kufikilia hivyo akakishika kitasa cha mlango na kugunduwa mlango upo
wazi akausukuma na kuingia ndani kitendo cha kuingia tu ghafla akajikuta akipiga mueleka wa nguvu na
kudondoka chini, baada kukanyaga dimbwi la damu pasipo yeye mwenyewe kuona .
Akapiga kelele zenye kuchanganyika na kitete mtoto wakike alipagawa si kidogo kelele zake ziliwafanya
watu wakimbilie chumbani mule.
Kila mmoja akabaki mdomo wazi baada kugunduwa bosi wa Clab hiyo kashauwawa kwa kuchinjwa polisi
wakafika na kufanya uchunguzi wao kisha mwili ukabebwa Steven hakuweza kuamini baada kuona Bosi
aliyeweza kumpa kazi kauwawa kinyama namna ile akavuta kumbukumbu zake na kumkumbuka yule
kijana aliyemtandika mateke kisha akaondoka akiwa kabeba brifcase ndani ya Clab kila mtu akaambiwa,
Hakukuwa na jinsi watu wakatoka
Clab ikafungwa kwa kuwekwa utepe mwekundu huku polisi
Wakichukuwa maelezo kwa baadhi ya watu,
Bibiye Mona Risa kwenye mawazo yake
aliweza kutambuwa wauwaji ni kile kikundi kilichoanzisha fujo ndani ya ukumbi ule,
Wakati Steven akimkumbuka vyema
Hafidhi basi akaitowa simu yake na kumpigia sijui nani akasikika akisema
“ehee! Ndio mwenyewe, hapana babu siwezi kumfananisha atakuwa ndio yeye,
Itakuwa Makata hakumuuwa bwana,
Ndani ya usiku huu kamuuwa bosi wangu"...
Steven aliongea kwa pupa akiwa ndani ya gari,
Wakati wakikata mitaa kumbe nyuma yao kuna pikipiki ikiwafatilia pasipo wao kutambuwa"..
*************************************************************
Mariam hakuweza kuamini aiseee si kaambiwa Hafidhi yupo nyumbani kwake akifanya mauwaji inakuwaje tena akutane nae pale mlangoni, akabaki kutumbuwa macho kama vile mpiga chabo, akashituliwa na sauti ya Hafidhi ikimuuliza “Vipi baby mbona hivyo? Kuna tatizo au?’’ Mariam akabaki kimya tu ndipo simu yake ikaita tena kabla ya kuipokea Hafidhi akawai kumpola na kuipokea yeye maana kupitia macho ya bibiye aliweza kumsoma kila kitu, “Dada wahi shemeji ndio anavunja mlango huku please ndio nakufa mimi,’’ Mwanaume baada kuisikia sauti ile hakutaka kujiuliza sana akatoka mbio huku akimwambia Mariam “baby nifate,’’ Wakaingia ndani ya gari hiyo speed waliondoka nayo hapo utasema wapo kwenye mashindano ya olimpiki, “unajuwa mpaka sasa baby sielewi chochote inakuwaje Othman aseme ni wewe ndio umekuja nyumbani kwangu kufanya mauwaji?’’ “Baby tulia usiwe na presha tambuwa kitu kimoja ndani ya dunia hii kuna Copy na Past sasa kuna maboya fulani wanatafuta kiki kupitia mimi subiri tufike na uwone huyo Hafidhi j Ikram feki namnyonya mavi. Maana hadi facebook utakuta wanatumia hili jina la kipekee’’
NAOMBA SAPOTI, KUNA MATANGAZO(ADS) YANAJITOKEZA KWENYE APP YETU, LIMOJA LINAJAA KWENYE KIOO CHAKO JINGINE LINANG'ANG'ANIA HAPO CHINI KABISA, BONYEZA JAPO MARA 2 AU 3 KILA UKIFUNGUA SIMULIZI HIYO ITANIPA NGUVU YA KUENDELEA ZAIDI NA SIMULIZI ZETU🙏🙏
TAZAMA KICHEKESHO HIKI KISHA BONYEZA SUBSCRIBE ILIYOPO CHINI YAKE WAKATI TUKIELEKEA KWENYE MUENDELEZO

USIKOSE SEHEMU YA AROBAINI NA NANE
Maoni, Ushauri na Chochote Share Namimi Katika Mawasiliano Haya:
+255 718 274 413
+255 764 339 438
ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Maoni, Ushauri na Chochote Share Namimi Katika Mawasiliano Haya:
+255 718 274 413
+255 764 339 438
ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni