Notifications
  • THE NIGHTMARE (6)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA SITAILIPOISHIA...“toa loud speaker bwana.”Aliongea Balqis baada ya Sharji kubonyeza kitufe cha kupaza sauti.“kwanini hutaki nisikie maongezi yenu?” aliongea Karimu kwa sauti ya ukali kidogo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...“kwani kuna ubaya mimi nikiongea private na mdogo wako?” alijibu Balqis baada ya kuisikia sauti ya Karimu.“hakuna ubaya.” Alijibu Karim kwa sauti ya…
  • THE NIGHTMARE (5)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA TANOILIPOISHIA...Alijikuta outomatic akijisemea kwa mshangao baada ya kumuona dada mmoja mrembo mwenye asili ya kiarabu akiingia mule ndani. Hakuvaa ushungi kama alivyowazoea kuwaona waarabu wengi ambao alikutana nao. Huyu alivaa suruali ya jeanz nyeusi na juu akiwa na kikoti chake cheusi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Kati kati kulikua na nguo Fulani nyeupe iliyonakshiwa…
  • THE NIGHTMARE (4)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA NNEILIPOISHIA...Aliongea Khalidi na kuufungua mkanda wa suruali yake na kuanza kumtandika Karim.“unanipiga mimi?...utaona!”IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Aliongea Karim na kuondoka huku analia.*****************************Zilipita wiki mbili bila ya Karim kuonekana nyumbani kwao. Sabra alisikitika kidogo kutokana na kuwapenda sana watoto wake japokuwa huyo mtoto mkubwa hakuwa…
  • THE NIGHTMARE (3)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA TATUILIPOISHIA...Akiwa hewani akikata mawingu kurudi Tanzania, kichwa chake kilikua na mawazo mengi sana juu ya mume wake. Aliikumbuka siku waliyofunga ndoa.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Pia alijua kwanini mume wake alipendelea kufanya kazi uingereza na yeye kumfungulia ofisi huku huku Tanzania. Hakujua kuwa kazi anayoifanya mumewe ni ile ya kutembea na tajiri mkubwa…
  • THE NIGHTMARE (2)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA PILIILIPOISHIA...Khalidi alishangaa kuitwa na mtu asiyemfahamu. Alitoka na kwenda kumuangalia huyo mtu maana kiukweli hakua na ndugu aishie hapa Dar hata mmoja anayemfahamu..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Alipigwa na butwaa baada ya kumuona Sabra pale.“ahsante mungu.” Aliongea Khalidi baada ya kumuona tu yule binti pale.“pole sasa kaka yangu, nisamahe mie.” Aliongea Sabra kwa…
  • THE NIGHTMARE (1)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA KWANZANi kipindi cha mvua za masika. Upepo mkali, na mvua kubwa iliendelea kunyesha kwa kasi kila kona ya nchi ya Tanzania.Ipo mikoa iliyofurahia mvua hizo kwa kuwa walikua wanaisubiria kwa hamu kwa ajili ya kilimo. Lakini ipo mikoa iliyokua inapata shida kwa uharabifu wa mazingira na mengineyo mengi.Moja ya miko hiyo ni Dar-es-salaam. Watu wanaoishi katika mkoa huo walichukia mvua mfululizo kutokana na sababu mbalimbali. Biashara nyingi…
  • MY DIARY (50)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA HAMSINITULIPOISHIA...Nilimnongo’oneza kuwa atumie kinga ili nisimwambukize ukimwi akanijibu kwa sauti ya mahaba nisiwe na hofu yeye yupo tayari kufa kwa ajili ya penzi langu hivyo hawezi kutumia kinga kwa mke wake aliyemoa tena siku muhimu kama hiyo.Sikutaka kumbishia yeye ndo muaamuzi wa mwisho kuhusu afya yake hivyo nilimuacha aendelee kufanya yake.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Kumbe na…
  • MY DIARY (49)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA TISATULIPOISHIA...Baada ya maneno ya kusilimu ambayo waliambiwa wayatamke kiongozi huyo alisema neno ya mwisho kabla hajashuka.” Kila alie na akili timamu, mwenye busara naa anaetaka haki, na kusimama pamoja na haki, basi akiangalia dunia ilivyo na jinsi inavyokwenda basi lazima kutakuwa na nguvu kuuu nayo ni mwenyezi mungu.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Kuna vitu vingi sana…
  • MY DIARY (48)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA NANETULIPOISHIA...Familia yangu haikukubali kabisa mimi kuolewa na rangi nyeusi hivyo walinitenga na kusema hawanitambui kuwa mimi ni ndugu yao.Lakini kutokana na mapenzi mazito niliyokuwa nayo kwa baba yake na Leah nilijikuta nipo tayari kwa lolote hivyo nikahama na kwenda kuishi Tanzania.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Katika miaka hiyo tuliyokaa nilibahatika kupata mtoto huyu…
  • MY DIARY (47)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA SABATULIPOISHIA...Lakini ilifikia mahali ndoto hiyo inanijia hata mchana nikiwa nimekaa mahali tulivu.Ilikuwa inanipa taswira nzuri ya sehemu ambayo madini yalikuwepo.Basi nilianza mikakati ya kulitafuta eneo hilo na hiyo ni mara baada ya ushauri wa mpenzi wangu Candy hapo akimaaanisha yule dada aliyekuwa naye pale jukwaaani.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Candy alinisihii sana…

MTAA WA TATU (54)

Mwandishi: Hafidhi J Ikram

SEHEMU YA HAMSINI NA NNE
Hafidhi baada kuwapiga chenga za mwili polisi na kikosi ca ma FBI safari hii tunamuona akiwa maeneo ya Mbagala sehemu ambayo alipanga chumba sema tokea rafiki yake wa karibu ambaye ni Jackson afariki dunia nae kuonekana kwenye mitaa hiyo imekuwa kwa nadra sana.

NIOMBE SAPOTI, BONYEZA TANGAZO LINALOKUJA NA KUJAA KWENYE SIMU YAKO WAKATI UKIFUNGUA SIMULIZI AU LILE LINALOKUWA KATIKATI YA SIMULIZI ZETUKABLA HAUJAIFUNGUA NDANI, PIA KUNA LILE LINAKUJA NA KUNG'ANG'ANIA HAPO CHINI, BONYEZA WALAU MARA 3-4 HIVI HIYO NDIO SAPOTI YAKO KWANGU, TAFADHALI NIPE NGUVU NAKUTEGEMEA SANA MSOMAJI WANGU
SASA ENDELEA...
“Wee kaka mambo?’’ ilikuwa salamu kutoka kwa binti mmoja hivi akimsalimia Hafidhi

“Poa niambie dada yangu umzima weye?’’ Hafidhi akaitikia salamu sijui kwa kiswahili cha wapi na kuuliza swali. “mi mzima hofu kwako tu’’ binti nae akajibu, baada salamu kila mmoja akabaki kumtizama mwenzie kwa jicho la kiwiziwizi kabla ya simu ya Hafidhi kusikika ikiita ndani kwakuwa alikuwa akiosha vyombo akamuomba yule binti kwa kumwambia “Sister samahani kama hutojali je unaweza kwenda kuniletea simu yangu ipo mezani hapo’’ pasipo binti yule kuitikia akainuka na kuingia ndani kisha akatoka na kumkabidhi simu,

“Thank you my sister Hafidhi akashukuru kwa lugha ya kigeni binti akatabasamu tu “Halloo nani mwenzangu?’’ Hafidhi baada kupokea simu akauliza swali kwani number ilikuwa ngeni, sauti ikasikika ikicheka kwa dharau tena ilikuwa sauti ya kikebaada kucheka akakata simu pasipo kuongea chochote kile “halloo,,,halloo,,ohoo shit! Hivi duniani kuna watu wengine machizi ehee?’’ akasikika Hafidhi akiuliza hivyo, yule binti akamtazama na kuuliza “kwanini unasema hivyo?’’ “si huyu mtu kanipigia simu baada kuongea kaishia kucheka na kukata simu kama sio uchizi kitu gani’’,,,,”Mmh! Yani kacheka tu kakata simu kwani wakike au wakiume?’’ “Ni mwanamke kibaya zaidi nampigia hapa hapatikani sijui ndio nini’’

“Si ulimsevu jina lake?’’ “Hapana number yake ni ngeni’’ “basi usitake kuumiza kichwa sana chakufanya embu jaribu kucheki jina lake yani ufanye kama unamtumia pesa hivi iwe Tigo pesa au M-pesa utaliona jina lake’’ binti akatoa ushauri huo basi Hafidhi nae akafanya hivyo ghafla akashtuka na kuitupa simu chini sijui kaona nini “Vipi mbona umeshtuka kuna tatizo au, binti akauliza huku akiyokota simu na kuitazama “mmh! Kumbe mtu mwenyewe anaitwa Yusra Yasri yani double (Y) hakika lilikuwa jina la marehemu Hafidhi akabaki kujiuliza ni nani kasajili line kwa kutumia kitambulisho cha Yusra, hakutaka kujiuliza sana akaingia chumbani kwake sekunde si nyingi akatoka na kumwambia yule binti “nisuuzie vyombo vyangu mi natoka kidogo kisha akaondoka kwa mwendo wa haraka bila shaka kuna kengere ya hatari imeweza kugonga kichwani kwake isijekuwa kama yale mambo ya Chanduka Nusraty aliporudi kutoka kuzimu. Kumuachia chumba binti yule ilikuwa kama kumuachia marehemu Amina basi binti akaosha vyombo na kuingia zake chumbani mtoto wakike alikuwa akihishi nyumba ya jilani tu akavua dera lake na chupi kisha akajifunga upande wa kanga aliokuwa nao kisha akatoka kwenda kuoga waliomuona wakabaki kumshangaa tu.

“Huyu Saida kwa kujishauwa utasema mganga kaona jogoo yani kuambiwa asuuze vile vyombo ndio kaona ajiachie kabisa’’ mmoja kati ya wapangaji wa nyumba hiyo alimwambia mwenzake, “wee muache tu usikute jamaa kapigiwa simu na demu wake kuwa yupo stendi ndio kaenda kumfata hivyo mbona huyu mwehu atakoma, kila mmoja akaangua kicheko cha kishambenga, sauti zao ziliweza kumfikia vyema Saida ambaye alikuwa bafuni akijimwagia maji nae hakujali kama yuko chooni akaangua kicheko cha nguvu kwa kugonga gonga bati la choo “hahahaha,,,halloo,,,halloo ,,,,pyeee,,,nimepewa lift wacha nipige na honi kama limewauma kanyeni matikiti’’,,,, kauli ya Saida ikawafanya wale wamama wawe kimya siku zote Saida ni binti ambaye anajiamini sana kutokana na kaka zake wawili ni wacheza karate kwenye dojo la Mbagala kuu wakati kaka yake mwengine ni Mwanajeshi yani ikitokea siku ukampiga au kumchokoza mtu mmoja kutoka familia hiyo utajuta kuzaliwa yani kuanzia babu, bibi, baba, mama yani hadi virembwe wote watakuja mtapigwa nyumba nzima kwakifupi ni binti ambaye wanaume wengi wamemshindwa tabia, wakati Saida akiwa bado yupo chooni ghafla sauti ya kishindo ikaweza kusikika puhuu, zikifatiwa na kelele za mwiziii,,, jamani mwiziii sijui huyo mwizi kaingia muda gani chumbani kwa mzee wa nyapu yani wale wamama walishtukia mtu akitoka ndani mule kwa kuwaruka na kukimbia mbio mgongoni akiwa kabeba begi ndipo wakapaza sauti kwa kumuitia mwizi, bibiye Saida akatoka chooni mbio mbio akiwa na mapovu kichwani.

Sema akakuta watu washaingia vichochoroni kumkimbiza mwizi nae hakutaka kujiuliza akaingia ndani na kukuta mlango wa chumba alichoachiwa upo wazi binafsi hakuweza kufahamu mapema kama mwizi ndio kaingia ndani ya chumba hicho je kaiba kitu gani, akajipangusa mapovu na kuvaa nguo zake na kutoka kufika nnje akakutana na kikundi cha watu wakiwa wanarudi akauliza,

“Vipi jamani huyo mwizi kapatikana au?’’ hakuna aliye mjibu zaidi ya mwenye kubeba jiwe kutupa chini mwenye panga au sururu kuingia nalo chumbani kwake, “Yani Yule kijana anakimbia utasema kiberenge maana tumefika pale kwa mama Shego akaruka ule ukuta mrefu vijana kwa wazee tumeshindwa kuruka pale kwa dharau akatuonyeshea kidole cha kati na kupotelea upande wa pili’’ alisikika binti mmoja akisimulia hivyo mpaka hapo Saida akatambuwa kumbe mwizi kakosekana swali la kujiuliza kichwani kwake kaiba nini’’,,,,

“unataka kusema karuka ule ukuta wa pale!’’ “ndio maana yake sisi wakati tunamkimbiza tulipoona akikimbilia kule tukajuwa tunaweza kumshika tu kwasababu kule hakuna njia kumbe mwenzetu ndio anaenda kutuacha’’ “kwani kaiba nini?’’ Saida akauliza swali, “Hata sijui kaiba kitu gani sema mgongoni alikuwa kabeba begi bila shaka ndio mzigo aliouwiba,

Saida akavuta pumzi kwa ndani na kuzishusha hakika alitambuwa ni uzembe wa kuacha chumba cha mtu wazi ndio umepelekea kuibiwa je atamueleza kitu gani mwenyewe mpaka amuelewe sema akajipa moyo familia yake ipo, Hakuweza kufahamu kama familia yake si chochote si lolote mbele ya mwanaume huyo wa shoka.

Hafidhi nae baada kuondoka nyumbani kwake akapanda daladala mpaka Buguruni rozana na kushuka akavuka barabara na kuelekea maeneo ya kwa Madenge yani alikuwa anatembea haraka haraka sauti ya honi ndio ikamshtua na kumfanya akae pembeni kidogo

“Pisha njia mtoto wa malaya wewe yani unatembea njia nzima utafikili ya baba yako punga wee’’ alikuwa dereva bodaboda aina ya boxer akiongea hivyo na kumwita Hafidhi mtoto wa malaya yani bora wakati anaongea maneno hayo angeondoka si akasimama “Unasemaje wee jamaa mimi nani?’’ Hafidhi akauliza swali huku akimsogelea yule kijana ilikuwa kufumba na kufumbuwa kijana yule akirushwa hewani baada kutandikwa zinga la teke na kutupwa kule barabara kisha mwanaume akaondoka na pikipiki, yani kilikuwa kitendo cha haraka mno kijana akabaki kupiga kelele “jamani pikipiki yangu!’’

“pole sana kijana siku zote unaambiwa dawa ya kiburi jeuli hakika leo umeipata kiboko yako wewe ndio ulitaka kumgonga yule jamaa baada kumuomba samahani ndio kwanza ukamtusi sasa unaona kilichokutokea, kakupa teke moja tu kama vile Vann damme kwenye movie ya bloosport kamtandika Bolo younk pole ehee’’ Alikuwa mzee mmoja muuza kahawa na kashata katika maeneo hayo,

Unaweza kusema yupo kwenye mashindano au anafukuzwa na mapolisi kwajinsi alivyokuwa akiendesha ile pikipikki kwa kasi watu waliokuwepo maeneo ya sokoni wakabaki kutukana matusi na kulaani kitendo cha dereva yule kutokuwa mstaarabu yani watu walikoswa koswa kugongwa na pikipiki ile si akaingia nayo kwenye vichochoro vya Madenge mitaa ambayo kila wanaonyesha video show biashara za chipsi sambusa kachori ice cream zimejazana.

Mbele ya nyumba moja hivi ndipo akafunga bleak na kushuka akabisha hodi na kukaribishwa na mzee mmoja wa kiarabu kama tunamkumbuka ndio baba mzazi wa marehemu Yusra “Karibu sana mkwe bila shaka ujio wako ni wa neema kubwa sana kwetu’’

“Kwanza Assalam alaykum mzee wangu naona umeanza maneno kabla ya salamu’’

“Waaleykum ssalam kijana hivi unadhani hata salamu naweza kuikumbuka kweli maana kijana umetutenga kabisa yani sikuoni tena maana kile ambacho ulikuwa ukikifata hakipo tena’’ “Hapana mzee wangu si unajuwa mambo mengi kijana wako naangaika kila kukicha kumsaka muuwaji wa kipenzi changu’’

“ohoo basi vyema kijana kama bado unaendelea kufanya hizo harakati lakini naomba utambuwe kitu kimoja tu mpaka sasa muuwaji wa mwanangu nae yupo kuzimu. Ni kauli ambayo ilimshangaza sana Hafidhi na kujiuliza amejuwaje kama yule kijana kashauwawa tayari sema hakutaka kuonyesha mshangao wake wakaenda kukaa kwenye sofa dakika si nyingi kuna binti akaingia yani kitendo cha Hafidhi kumtia machoni tu moyo wake ukashtuka hakika binti alikuwa kafanana kila kitu na Yusra “Assalam alaykum ewe kaka yangu’’,,, yule binti akatoa salamu huku akimpatia kiganja cha mkono mwanaume akaitikia huku akiwa kashikana nae sema katikati yule binti aliweka kitambaa kama sheria ya dini ya kiislam inavyosema ni haramu kwa mwanamke na mwanaume kugusana nyama kwa nyama asiekuwa halali kwako,

“Waaleykum ssalam mzee wa nyapu akaitikia hivyo. Huku akikitumia kidole chake cha kati akimtekenya kwa style ya uchokozi bibiye akang’ata ripsi za midomo yake kuonyesha jinsi gani anajisikia msisimko wa ajabu yani kutekenywa kidole tu kwenye kiganja chake cha mkono mototo kapagawa

“Vipi mbona mmeshikana kwa muda mrefu hivyo?’’ Ikabidi baba aulize swali. “Ahaa hapana mzee unajuwa namfananisha huyu mwanao na Yusra hakika wanafanana sana’’ Hafidhi akazuga kwa kusema hivyo huku akimuachia mkono’’

“Ndio huyo ni mdogo wake anaitwa Sumaiya wamepishana mwaka mmoja na nusu tu,’’ “Duhuu yani wee mzee ni nom a sana mwaka mmoja na nusu ukawekeza kitu kipya hahahaha’’
Kila mmoja akacheka
“Sumaiya embu nenda kaandae chakula shemeji yako si unamuona ana maneno
Utasema yupo bungeni.
Sumaiya akaondoka mbavu hana kwa kicheko akaingia chumbani kwake na kujitazama mkononi na kujibusu
“kwa style hii siwezi kukukosa
Shemeji hakika wewe ni wangu, nichukuwe Mimi niwe kiburudisho chako kama alivyokuwa akikuburudisha Dada
Nami nitakufanyia hivyo hivyo".......

Wakati bibiye Sumaiya akimuwazia kumpata shemeji yake kama usemi unavyosema
Sijui hainaga ushemeji tunakulaga, huku
Sebuleni mazungumzo baina ya
Hafidhi na mkwewe yalikuwa yanaendelea.
“sasa mzee wangu mimi nimekuja kuna tatizo kidogo linanitatiza"

“Tatizo gani tena kijana?"
“Dahaa sijui hata niseme nini kwakifupi leo
Nikiwa nyumbani kwangu simu yangu ikaita kuitizama number ngeni basi nikafanya kuipokea ajabu
Aliyepiga simu ile akaanza kucheka yani akacheka sana mwishoe akakata simu,
Nikajalibu kuiangalia ile number kwa tigo pesa ajabu jina limetokea
Yusra Yasri"

NAOMBA SAPOTI, KUNA MATANGAZO(ADS) YANAJITOKEZA KWENYE APP YETU, LIMOJA LINAJAA KWENYE KIOO CHAKO JINGINE LINANG'ANG'ANIA HAPO CHINI KABISA, BONYEZA JAPO MARA 2 AU 3 KILA UKIFUNGUA SIMULIZI HIYO ITANIPA NGUVU YA KUENDELEA ZAIDI NA SIMULIZI ZETU🙏🙏

TAZAMA KICHEKESHO HIKI KISHA BONYEZA SUBSCRIBE ILIYOPO CHINI YAKE WAKATI TUKIELEKEA KWENYE MUENDELEZO



USIKOSE SEHEMU YA HAMSINI NA TANO

Maoni, Ushauri na Chochote Share Namimi Katika Mawasiliano Haya:
+255 718 274 413 Ipo WhatsApp
+255 764 339 438
ZephilineEzekiel@Gmail.Com
10 Mtaa wa Tatu Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni