Notifications
  • MY DIARY (12)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA MBILITULIPOISHIA...Niliamua kufanya ziara ili nijue pakoje na mwisho wa siku niliamini kuwa kutokana na umaarufu wa marehemu baba yangu isingekuwa kazi sana kulipata shamba lake..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi nilitembea kijiji hadi kijiji huku nikijaribu kuuliza kwa wenye viti wa mtaa kama walikuwa wakimjua marehemu Bura. Kwa kweli kazi ilikuwa ngumu sikuweza kuvimaliza vijiji…
  • MY DIARY (11)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA MOJATULIPOISHIA...Wakati akiongea maneno hayo mara mtarimbo ukaanza kusimama nikajisemeha nimeshakosea nilitakiwa niondoke nilivyoona kimelele tu, nikajua hapo lazima atanitafuuna bila huruma. Basi akaingia bafuni akachukua sabuni akajipaka ili kujisisimua ngoma isimame vizuri.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Yaaani nilichanganyikiwa na huko bafuni nilisikia maneno ambayo yalinichekesha…
  • MY DIARY (10)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMITULIPOISHIA...Nikamwambia Joyce ndo maana mimi nakupendaga. Nikamwambia “nitakuapa feedback ngoja nimpigie asije akaja na makufuli yake leo hii. Nikampigia baba mwenye nyumba eti kwa kujiamini kabisa akapokea nakusema “ Halow mrembo” Nikamwambia Yes mpenzi kitu ambacho kilimfurahisha sana..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Kuokoa hela ya vocha nikamwambia nimekubali ombi lako alafu nikakata…
  • MY DIARY (9)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TISATULIPOISHIA...Basi Dj wangu aliendelea na mautundu yake akaniwekea mambo ya pwani na hapo ndipo uvumilivu ulipomshinda akaja kunibambia na mimi sikuona haja ya kumbania kwa kuwa ni mali zake mwenyewe. Nilizungusha nyonga na kiuno mpaka nikachoka nikajitupa kitandani ili nipumzike. Nafsi yake ilikuwa imeridhika kwani hakutka tena penzi bali alichukua lap top yake na kuanza kunionesha picha na vitu vingine ambavyo vilinipa raha.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA…
  • MY DIARY (8)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA NANETULIPOISHIA...Sijui hata haya maneno yalitoka wapi, fahamu zilinitoka na Ticha aliamua kuninyanyasa maana nilishajikojolea zaidi ya mara tano. Basi na yeye kwa kutafuta mbwembwe alianza yale mambo yao ya katerero, siunajua tena mwalimu John alitokea pande za Bukoba.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alinichezea sana na baadaye nilishangaa kukuta jamaa ameshaingiza kunako. Sikujielewa kwa…
  • MY DIARY (7)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA SABATULIPOISHIA...Kwaito zilivyonoga uzalendo ulinishinda nikajikuta na mimi nashuka ngazi kuelekea chini sehemu ya kuchezea.Nilizijua kwani shuleni tulikuwa tunazicheza sana hasa kwenye yale madisco yetu ya mwisho wa mwezi.John wangu alibaki juuu akiniangalia jinsi nilivyokuwa nikicheza vizuri.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Yeye alishindwa kushuka akiofika kile kitu kukaliwa na watu…
  • MY DIARY (6)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA SITATULIPOISHIA...Akanambia kuwa wamemwambia wapo East Africa Pub na tayari wamaeshaagiza mkuu wa mbuzi. Mmmmhhhh kusikia mguu wa mbuzi mate yalinijaa mdomoni. Basi kwa harakaharaka nikamwambia naomba niende niende nyumbani nikachukue viwalo vya club kisha nitawakuta hapo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alinambia mbona hizo nguo ulizofaa zipo poa tu wewe twende hivyo bhana si upo na…
  • MY DIARY (5)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TANOTULIPOISHIA...Akanisimamisha na kuanza kuiuliza maswali mengi yasiyo na maana huko akionekana kutojiamini. “samahani dada, sijui unaelekea wapi”? Nikamjibu dukani. Akavuta pumzi ndefu na kuniambia ok, nisaidie namba zako za simu. Nikamwangalia juu na chini nikwambaia nimezisahau na simu nimeiacha ndani nikirudi ndani nitakuletea..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Akaishiwa pozi akanambia,…
  • MY DIARY (4)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA NNETULIPOISHIA...Uchambuzi huu ulinigusa sana kwani hata mimi nilijihisi kuwa sikuwa na utando huo yaani bikira japo nilikuwa sijawahi kujamiana na mwanaume wa aina yeyote zaidi ya ile michezo ya utotoni ya kula mbakishie baba au ile ya kibabababa na kimamamama. Alianza kunishika mapajani na kunifanya nianze kusisimuka ajabu kwani japo alikuwa ni mwanaume mikono yake likuwa ni milani sana kama ya mtoto wa kike.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media…
  • MY DIARY (3)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TATUTULIPOISHIA...Nazani sasa unanielewa ninaposema nilikuwa sina ndugu kwani baba yangu hakuwa na ndugu yeyeote zaidi ya marafiki ambao na wao kwa sasa ndio hao wameshagawana mali zote. Nimebaki mimi na dunia yangu hivyo basi nilimwomba rafiki yangu wa kufa na kuzikana kwa jina Joyce anisaidie kunisitiri nyumbani kwao.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Likizo ilipoisha tulirusi shuleni na…

DHAMANA (30)

Jina: DHAMANA

SEHEMU YA THELATHINI
TULIPOISHIA...
Jambo ambalo wanadamu hawa hawakulitambua ni kwamba dawa waliyompa Farida kila siku usiku ilikuwa inapunguzwa na Faimu na hapo Farida hurudi katika akili na hukutana kimwili na Faimu kwa kipindi hicho chote huwa alikuwa anamjia kwa njia ya ndoto, hadi huyu bwana hapa anamposa Farida baada ya kumuweka chini yake kwa kutumia nguvu za kichawi tayari huo mchezo Faimu alikuwa anaendelea na ndiyo katika kipindi hicho akawa anamuona anaweweseka na hata alipokuja kuacha tayari Farida alikuwa ana ujauzito wa Faimu huyu bwana akidhani ni wake.

KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA CnZ Media APP INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
Jamadin alipozaliwa Faimu alikuwa yupo makini sana katika kumlinda mwanae kuliko kitu kingine chochote pia alimpatia mkufu wenye kidani kinachoitwa Dainun ili umlinde na hadi hawa mabwana wanataka kumtoa kafara Jamadin kipindi hicho akiwa na miaka mitano hapa duniani na mmoja kwamujibu wa mila za kijini ambazo miaka mitano ya kwanza ya mtoto huhesabiwa ni mwaka mmoja . Faimu alishajua hilo na alifika eneo hili akiwa na jazba sana.

Alifanya hila ya kutengeneza upepo nje ili aharibu kazi yao kisha aliingia ndani akiwa yupo kama kimbunga ndipo alipojikuta amenasa kwa kuzungushiwa damu ya hedhi ya mwanamke akawa hawezi kutoka kwani ina madhara sana kwake kama akiisogelea, hapo ndipo mabwana hawa wakamchoma kwa pamoja visu vilivyochovya kwenye damu ya hedhi katika mwili wake na kumfanya apate jeraha kubwa.

Faimu aliishiwa nguvu na alizama chini ya ardhi mimi nikaja kumtoa nikampeleka kwa mtukufu mfalme ili apatiwe matibabu kwa jereha hilo, kuanzia siku hiyo Faimu alikuwa mtu wa kukaa kitandani kwani mkufu wenye Dainun ambao ni mali yake ndiyo ungeweza kumponya tu. Baada ya mwaka mmoja Faimu alifariki akitoa tamko mwanae ndiye aje kukaimu nafasi yake ya ufalme atapofariki baba yake, agizo jingine alilotoa ni kisasi chote kilipwe na mwanae tu. Kiongozi Zalabain au Faimu alipokuja kupatikana taji lilimkataa mpaka upatikane huu mkufu na kisasi kulipwe kwani hawa ndugu ndiyo chanzo kuzaliwa watoto waliodumaa katika himaya yetu kutokana na kutoonekana kwa usiku kwa muda mrefu".

Mzee Mubarak alimaliza simulizi yake iliyomliza sana Bi Farida baada ya kusikia kuwa Faimu kwa muda huo ni marehemu, mzee Buruhan aliposikia hiyo habari hasira zilimzidi maradufu na akasimama wima huku akihema kwa nguvu.

"Mzee mwenzangu tulia basi walsu kidogo tumalizie" Mzee Mahmud alimsihi rafiki yake.

"Sihitaji hata kuendelea kumuangalia huyu mwanaharamu na sina mtoto kama yeye ngoja niondoke nje mkimaliza mtanikuta" Mzee Buruhan alisema kwa jazna kisha akaanza kutembea kuelekea nje.

"Baba usifanye hivyo" Shafii alilalamika kumsihi baba yake.

"kelele wee! Shaytwani mkubwa usiniite baba yako na sina mtoto kama wewe mtoto wangu ni Ally tu" Mzee Buruhan aliongea kwa ukali kisha akatoka nje akamuacha Shafii akilia kwa uchungu, muda huo huo Ally naye akainuka akamtazama Shafii kisha akamtazama na Salma halafu akamtazama Hamida kwa huruma sana.

"Salma naomba unipatie mwanangu niondoke naye" Ally aliongwa kwa ustarabu halafu akamuangalia Mzee Mahmud akamuambia, "Baba huyu mwanamke ni zaidi ya shetani yaani kanitumikisha kama mtumwa wa ngono kwa miaka mingi baada ya ule mkufu kunifanya niwapende na ushenzi wao, sijaoa wala kuwa na mke na umri huu matokeo yake napata mtoto kupitia huyu malaya tena mke wa mtu. Hebu muulizeni Hamida ni mtoto wa nani".

Ally alipoongea maneno hayo hadi Shafii aliweka mkono kinywani kwa ujinga alioufanya Salma ambaye aliishia kuona aibu tu, aliinamisha kichwa chini kutokana na fedheha iliyomkuta hadi wanae wakawa wanamuona ni binadamu wa ajabu.

"Salma huyo Hamida ni mtoto wa nani?" Mzee Mahmud aliuliza taratibu huku akimuangalia Salma kwa Macho ya ukali sana, Salma alishindwa kujibu na akakaa kimya akiwa ameinamisha macho chini hadi alipokaripiwa.

"wa A....A..Ally" Salma alijibu huku akitazama chini kwa aibu na kupelekea mwanae mkubwa Jamal asimame akawa anaenda alipo Ally ambapo ni jirani na mlango wa kutoka mje ili aondoke, Salma alimshikilia miguu mwanae lakini alijikuta akisukumwa kwa nguvu.

"Bora ningezaliwa na shetani kuliko wewe" Jamal aliongea kwa hasira halafu akatoka nje huku akilia kwa uchungu, Hamida naye alinyanyuka kisha akaanza kumtazama mama yake huku machozi yakimtoka kwa uchungu. Salma alipotaka kumkumbatia miguuni alimsukuma kwa nguvu halafu akaenda halipo Ally akawa anamtazama huku machozi yakimtoka, Hamida alimkumbatia baba yake kwa mara ya kwanza huku akilia na Ally naye alimpokea mwanae huku machozi yakimtoka kwa alichofanyiwa.

"Baba samahani naondoka humu nikiwa nina mwanangu, sina kaka humo" Ally alizungumza kwa hasira halafu akatoka nje akiwa na Hamida, Salma alipotaka kuwafuata alijikuta hawezi kuinuka kabisa.

"Shafii nadhani unakumbuka jana jioni nilikuambia leo ndiyo utapata nafuu ya tatizo lako, sasa basi napenda utambue kuwa sikumaanisha litatuliwa basi nafuu yenyewe ndiyo hii ya kuwaona Bi Farida na Zayina ila si kukusaidia zaidi kutokana na udhalimu mlioufanya. Niliwaonya msifanye hivyo tangu mnaenda kumuwekea dawa Farida lakini hukusikia kwa ubishi wako, sasa mwanangu donda la kujitakia halihitaji pole uguza bila msaada wala pole. Nadhani Zalabain Jamadin ana mengi ya kuongea na wewe mkiwa wewe na Salma sasa mtazungumza naye wawili, mimi sisaidii madhalimu kama nyinyi" Mzee Mahmud naye aliongea kisha akanyuka akasema, "lengo langu ilikuwa kumnasua Ally maana naye angekumbwa na balaa lisilomuhusu na nimefanikiwa sasa nawatakia mazungumzo mema na Zalabain".

Mzee Mahmud alitoka nje akazidisha machungu sana kwa Shafii ambaye alilia sana pia Salma naye alijuta kwa yote aliyokuwa akiyafanya kwani hakuwa na muda wa kurekebisha tayati alishachelewa kabisa.

Mzee Mubaraka, Bi Farida pamoja na Zayina nao walinyanyuka wakabakisha watu watatu tu waliobaki humo ndani na walianza kutembea kwataratibu kuufuata mlango ulipo.

"Mke wangu, mwanangu" Shafii aliita huku akinyoosha akiwa anazidi kulia sana kwani hakuwa anaweza hata kunyanyuka, maneno yake yalimfanya Bi Farida asimame kisha akamsonya kwa nguvu halafu akasema, "mkeo nani kwa ndoa ipi? Sina mume kama wewe".

Bi Farida alipimaliza kuongea hayo maneno alitoka nje kwa hasira akiwa amemshikilia Zayina aliyekuwa analia tu kutokana na kilio cha baba yake lakini alimuacha apate adhabu kwa uovu wake

Zalabain alipohakikisha mtumishi wake,mama na dada yake wametoka nje alimama wima akiwa na macho yaliyojaa ghadhabu sana akawasogelea Shafii na Salma, alimuangalia Salma kwa macho makali halafu akamsogelea karibu zaidi na kusababisha Salma atokwe na haja ndogo papo hapo.

"Wakati unatoa damu yako ya hedhi iliyosababisha baba yangu afe mbona hukujikojolea, ulijua na mimi itaniua wakati mnanichanja na visu vyenu nilikuwa nina Dainun shingoni mwangu. Sasa leo zamu yako" Zalabain aliongea kisha akaushika shingo ya Salma akaiminya kwa nguvu hadi mishipa ikapasuka damu zikaanza kuvuja, alishika na kichwa akakivuta akakichomoa kabisa halafu akamgeukia Shafii akamwambia "nipe".

Shafii kwa uoga aliokuwa nao aliposhuhudia Salma alivyouawa aliweka mkono kifuani mwanga ukatokea na hapo mkufu ukaonekana ukiwaka halafu ukazimika ghafla, kuzimika kwa mkufu kulimfanya Shafii ashangae sana akabaki akimuangalia Zalabain huku akitetemeka.

"He! Ulijua hiyo Dainun itatoa mwanga uniue nayo, kwa taarifa yako nguvu kubwa ya Mzee Mahmud inaizuia hiyo isifanye kazi. Nipe!" Zalabain aliongea huku akimsogelea Shafii akiwa na jazba, Shafii hakuwa na ujanja aliivua Dainun akampatia Zalabain huku akitetemeka.

Zalabain aliichukua Dainun akaivaa shingoni mwake na kusababisha Dainun ipige mwanga mkali ulioenda juu kisha ikaanza kung'aa, alitoa tabasamu kisha akanyooshea Shafii kidole akamuambia, "umenipatia kimoja bado kingine tumalizane kabisa".

"Kipi?" Shafii aliuliza huku akitetemeka

"roho yako" Zalabain alijibu na macho yake yakaanza kutoa machozi ya damu tabasamu likawa limefutika usoni

"hapana" Shafii alisema huku aliweka mikono ishara ya kuomba msamaha lakini haikusaidia kitu kwani Zalabain alijigeuza kimbunga kikali kikamvaa Shafii kikawa kinamzungusha na kupelekea Shafii atoe mayowe ya maumivu yaliyosikika hadi nje, taswira mbaya ya kuruka kwa damu pembeni wakati akizungushwa ndiyo ilionekana na kisha vipande vya mifupa vvikaruka pembeni vikiwa na damu tupu. Muda huo tayari Shafii alikuwa ameaga dunia kutokana kupata mshahara kwa kile alichokifanya miaka mingi iliyopita.

****
Watu wote waliokuwa nje walisikia kelele za Shafii lakini hakuna hata oja aliyethubutu kumsaidia na makelele yalipotulia haukupita muda mrefu nyumba yote ikaanza kuporomoka yote kisha ardhi yake ikafunguka kifusi chote kikazama na huo ndiyo ukawa mwisho wa Shafii, watu waliona kitendo hicho walisikitika sana wengine walitokwa na machozi kwani ingawa kafanya mabaya bado alikuwa na nafasi kwa baba yake na mtoto wake.

Kulipotulia kabisa Zalabain alitokea akiwa ana Dainun shingoni mwake akamchukua mama yake na dada yake pamoja na mtumishi wake wakaondoka, waliobaki walitafita nyumba za kulala hapo Mpirani usiku huo baada ya kushuhudia mwisho wa dhahama ya kujitakia

****

Miale ya Dainun iliyopiga angani ilisababisha mwangaza wa kawaida kurejea katika himaya ya Majichungu, ndelemo na vifijo kutoka kwa majini wa aina mbalimbali ndiyo zilisikika na siku iliyofuata sherehe ilifanywa katika viwanja vya kasri la kifalme. Zalabain alivikwa rasmi taji la ufalme ambalo halikumkataa lilikaa kwenye kichwa chake vizuri kabisa, sherehe kubwa ilifanywa ilishuhudiwa na dada yake pamoja na mama yake wakiwa na furaha kama alivyokuwa yeye ana furaha.

MWISHO

Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
58 Dhamana Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni