SORRY MADAM (77)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA SABINI NA SABA
ILIPOISHIA...
Nikaitega mikono yangu usawa wa sehemu anayo ning’inia Dorecy, nikahesabu moja hadi tatu, Dorecy akajiachia na kutua kwenye mikono yangu, cha kushukuru MUNGU ametua vizuri kwenye mikono yangu, nikamsimamisha chini na kumuacha akiendelea kuhema kwa nguvu, kama bata mzinga.NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Nikaanza kupiga hatua za kuondoka katika eneo hili pasipo kusubiria asante ya Dorecy huku moyoni mwangu nikijikuta nikianza kusamehe kuhusiana na madini yangu, kwani hakuna uwezekano wowote wa mimi kuyapata kutokana na Khalid kujizatiti vizuri katika swala la ulinzi
“Edd….y”
Nilisikia sauti ya Dorecy ikiniita kwa unyonge nyuma yangu, nikasimama pasipo kutazama nyuma, nikashusha pumzi nyingi na kugeuka taratibu, nikamuona Dorecy akianza kukaa chini taratibu huku akiwa amelishika tumbo lake
“Eddy nakufa mimi, tumbo langu”
Dorecy alilalamika huku akiwa amelishika rumbo lake, nikaanza kupata mstuko baada ya kagauni kake ka kulalia alicho kivaa kukiona kikiwa kimelowa kwa damu sehemu zake za siri.Machozi ya uchungu yakaendelea kumtoka Dorecy, vilio vya Dorecy vikazidi kuongezeka, ikanilazimu kurudi kwa haraka katika sehemu alipo
“Eddy mtoto anatoka”
Dorecy alizungumza huku akipanua mapaja yake, wazo la kwanza kunijia kichwani mwangu, ni kukata nguo ya ndani aliyo ivaa Dorecy, macho yangu yakaendelea kumtazama Dorecy jinsi anavyo toa mayowe ya uchungu
“Eddy mwanangu uwiiiiiii”
“Yupo wapi?”
Nikastukia kofi zito ikitua kwenye shavu langu, kutoka kwa Dorecy ambaye anaonekana kukasirika, macho yake ameyatoa huku jasho jingi likimwagika kutoka na maumivu makali anayo yapata.
“Jikaze uzae”
Nilizungumza huku nikiishikilia miguu ya Dorecy ambayo ameichanua kwa kiasi fulani, nikaendelea kumuhimiza ajitahidi kumsukuma mtoto, kwani nilisha anza kuona dalili ya majimaji yanayotangulia kabla ya mtoto kuzaliwa.Taratibu nikaanza kuona kichwa cha mtoto kikianza kuchomoza
“Push kwa nguvu”(Sukuma……)
Nikaendelea kumuhimiza Dorecy kwa sauti ya juu, akaendelea kujitahidi kumsukuma mtoto wake atoke nje, nikaiweka mikono yangu karibu na kichwa cha mtoto na kuanza kukipokea kichwa chake taratibu
“Endelea mama, mabega yameshaanza kuchomoza”
Hadi mimi mwenyewe jasho likaanza kunitoka kwani si kazi ndogo ya kumzalisha mwanamke
“Eddyyyyyyyyyyyyyyyy”
Dorecy alizungumza kwa nguvu, huku akijikamua kwa nguvu zake zote na kumfanya mtoto wake kutoka na kuangukia mikononi mwangu, sikuisikia tena sauti ya Dorecy, katoto kake ka kiume, kenye mwili mdogo kakaanza kutoa kimlio kwa mbali, nikajikuta nikifurahi mimi mwenyewe, huku jasho likiendelea kunimwangika uso mzima, nikabaki nikimtazama mtoto huku kitomvu chake kikiwa bado kimeshikana na mama yake, ambaye amepotezafahamu kutokana na maumivu makali ya kujifungua
“Huyu mtoto amezaliwa kabla ya siku zake”
Nilijisemea kimoyo moyo huku nikiendelea kumtazama mtoto kwani ni mdogo kupindukia, kwa elimu yangu ya sayansi watoto wa aina hii huwa tunawaita njiti kutokana hajatimiza umri halisi wa yeye kuzaliwa kama watoto wengine wanaotimiza miezi tisa
Nikamtazama Dorecy kwa macho yaliyo jaa uchovu mwingi, kifua chake kwa mbali kinanyanyuka taratibu na kurudi chini, nikamsogelea na kumtingisha kidogo, ila hakuzinduka
“Hichi kitovu kinakatajwe?”
Nilijiuliza swali huku nikikitazama kitovu kilicho ungana kati ya mama na mtoto, nikamuweka vizuri Dorecy na kumlaza chali, nikamuweka mtoto wake juu ya tumbo lake kisha nikanyanyuka na kuanza kutafuta ni wapi ninapoweza kupata kitu chenye ncha kali cha kukikata kitomvu cha mtoto, kutokana kumesha pambazuka vuzuri ninaweza kuona kila kitu ambacho kinaweza kuwa chini, nikazunguka aneo la karibu na alipo Dorecy ila sikuona kitu kinachoweza kunisaidia kwa muda huu.Ikanilazimu kurudi sehemu nilipo muacha Dorecy, macho yangu yakangonana na macho ya chui, ambaye yupo hatua chache kutoka sehemu alipo lala Dorecy, ambaye muda wote hajitambui kutokana nakupoteza fahamu
“Mungu wangu”
Nilijisemea kimoyo moyo huku nikiendelea kumtazama chui ambaye anatoa mingurumo ya chini chini huku akilamba lamba mdomo wake wenye meno makli yenye ncha kali sana, nikachuchumaa chini taratibu pasipo kuyapepesha macho yangu, nikimtazama chui huyu, nikaokota kipande cha jiwe ambacho nimekikanyanga kwa mguu wangu wa kushoto, kisha nikasimama huku nikiendelea kumtazama chui huyu
“Shiiiii”
Nilitoa mlio huo, nikimfukuza chuki huyu ambaye taratibua alichaanza kupiga hatua za kumfwata Dorecy na mwanaye katka sehemu ambayo wamelala chini, chui akasita kidogo na kunitazama kwa macho yake makali
“Toka opo”
Niliendelea kuzungumza huku nikimtishia kwa jiwe ambalo nimelishika mkononi mwangu, mwili mzima ukaanza kunitetemeka baada ya chui kubadilisha muelekeo wake na kuanza kunifwata mimi kwa mwendo wa madaha katika sehemu ambayo nimesimama, kikataka kupiga hatua moja nyuma, gafla nikajikuta nikianguka chini kama mzigo, kitendo cha kujaribu kunyanyuka tayari Chui amenirukia kifuani kwangu, kichu cha kwanza kukiwahi katika kukishika ni shingo yake, nikakizuia kichwa chenye mdomo wake ulio jaa meno makali, usinidhuru kwenye mwili sura yangu.
Chui huyu akaendelea kunikwaruza na kucha zake, sehemu mbali mbali za mwili wangu, huku akijitahidi kuushusha mdomo wake kuing’ofoa pua yangu, nikaendelea kujikaza kwa juhudi zangu zote, uzito wa chui huyu ni mara mbili ya uzito alio nao mke wangu Phidaya, mikono yangu ikaanza kutetemeka kwa kuchoka, huku taratibi nikiendelea kujikaza kizuia shingo ya Chui huyu.
“Mungu wangu nisaidie mimi”
Niliendelea kuzungumza, huku mikono ikianza kuchuka taratibu chini, ikizidiwa uzito na kichwa cha chui huyu anaye onekana ananjaa kali, sikujali jinsi anavyo nikwaruza sehemu za mwili wangu kwa kutumia miguu yake ya nyuma na yambele yenye kucha kali sana, kikubwa ni kujitolea maisha yangu kwa ajili ya Dorecy na mwanaye niliye mzalisha
“Siwezi kufa kijinga”
Nikaanza kujitutumua kiume, huku nikiipandisha mikono yangu juu nikijitahidi kumtoa Chui huyu mwilini wangu, juhudi na nguvu zangu taratibu zikaanza kuzaa matunda, kwani nikafanikiwa kumgeuza chui na kumuegemesha kando.Mwili wangu mzima unavuja damu kataika sehemua alizo nikwaruza chui huyu, mikono yangu sikuiruhusu kutoka mikononi mwa chui huyu.Nikaanza kukidundiza kichwa chake chini, kwenye jiwe kubwa.Chui akazidi kupandisha hasira na kutoa pumzi kali iliyo anza kuyafanya macho yangu kumwagika machozi mithili ya mtu aliye pigwa bomu la machozi na askari wa kutulizaghasia
“Eddyyy”
Niliisikia sauti ya Dorecy ikiita kutoka katika sehemu alipo lala, nikageuza shingo yangu kumtazama sehemu alipo, nikamuona amekaa chini huku amemshika mwanaye, kitendo cha mimi kumtazama Dorecy kikawa ni kosa kubwa kwangu kwani chui, akanibinua kwa nguvu zake zote akaanza kunikwaruza huku meno yake akijaribu kuyakita kwenye paja langu la mguu wa kulia.Maumivu yasiyo na kifani yakaanza kuutesa mguu wangu, machozi ya uchungu yakanimwagika.Nikaokot kipande cha jiwe lilicho chongoka na kuanza kumkita nacho Chui cha kichwani mwake
Chui akazidi kuyakita meno yake kwenye paja langu, nia yake kuu ikiwa ni kunikata mguu wangu, nikazidisha kumbabiza kwa jiwe langu nililo lishika, kelele za maumivu zikaniendana na kasi yangu ya kukikita kicha cha chui kwa ncha ya kipande cha jiwe, kichwa cha Chui kikaanza kufumuka damu huku fuvu lake la kichwa likipasuka na ubongo wake kutoka nje, ikawa ni mwisho wa maisha yake
“Ahaaaa”
Nilizungumza huku nikilia kwa uchungu mkali, nikaushika mdomo wa Chui na kikauachanisha mdomo wake wenye meno yaliyo kita kwenye paja langu, japo maumivu ni makali sana ila nikajitahidi hivyo hivyo hadi paja langu nikalitoa kwenye kinywa cha Chui na kujilaza pembeni,Nikamtazama Dorecy sehemu aliyo kaa nikamuona akijitahidi kusota kuja sehemu niliyo jilaza mimi, huku sura yake ikiwa imejaa machozi mengi
“Usije”
Nilizungumza kwa sauti iliyo kwaruza sana huku nikimnyooshea mkono asifike katika sehemu nilipo mimi, nikajinyanyua taratibu huku damu zikendelea kuvuja kwenye paja langu.Chakumshukuru Mungu, Chui huyu meno yake, hayakufanikiwa kukutana na kutoa kipande cha nyama kwenye paja langu, au kuukata kabisa mguu wangu, nikaanza kutembea huku nikiuburuza mguu wangu ulio jeruhiwa hadi nikafika sehemu alipo kaa Dorecy
“Mtoto yupo hai?”
Nilimuuliza Dorecy huku nikimtazama mtoto wake aliye yafumba macho yake
“Ndio”
“Ohhh asante Mungu”
Nilizungumza kwa sauti ya kukwaruza sana huku damu zikiendelea kunimwagika mwilini mwangu, machozi yafuraha yaliyo changanyikana na uchungu yakaendelea kunitiririka usoni mwangu
“Eddy ninakupenda sana, samahani kwa yale yote niliyo kufanyia, ninaamini kwamba mimi ni binadamu ninaye weza kuhadaika kwa vitu vidogo sana.Sikustahili unisaidie, ilikuwa ni haki yangu kutafunwa na huyo chui mimi na mwanangu, ila wewe uliweza kujitolea maisha yako kwa ajliya yangu na mwanangu”
Dorecy alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake, nikamtazama kwa muda jinsi anavyo endelea kulia kwa uchungu sana
“Usilie, nimekusamehe muda mwingi sana, hali yangu inazidi kuwa mbaya na hapa niporini, ninjua sinto weza kutoka nikiwa hai, kifo kitakuwa juu yangu, ninakuomba umtafute msichana mmoja anaitwa Phidaya, anamimba yangu nakuomba unisaidie kwa hilo pale nitakapo kuwa nimeshakufa”
“Hapana Eddy, huwezi kufa nakuomba usizungumze hivyo”
“Dorecy, damu nyingi inanitoka nilazima….”
“Edddyyuuu tazama nyuma yako”
Sauti kali ya Dorecy ikaniomba kugeuka nyuma na mimi nikafanya kama alivyo niambia, ila tayari nimeshachelewa risasi mbili kutoka kwa watu wa Khalid waliofika kwenye eneo hili, zikatua kifuani mwangu, na taratibu nikaanza kwenda chini, nikapiga magoti na kumtazama Dorecy, aliye yatoa macho yake huku akishangaa, kuto kuamini kitu anacho kiona
“Bye….”
Nikaanguka chini, huku nikilalia tumbo na giza nene taratibu likaanza kuyafunika macho yangu, na kwambali nikaanza kuisikia sauti ya Dorecy ikiliita jina langu kwa uchungu
“bye….”
Nikaanguka chini, huku nikilalia tumbo na giza nene taratibu likaanza kuyafunika macho yangu, na kwambali nikaanza kuisikia sauti ya dorecy ikiliita jina langu kwa uchungu
Endelea
Sikuweza kusikia kitu chochote kinacho endelea kwenye masikio yangu
Kwa mbali nikaanza kuhisi sauti za watu wakizungumza taratibu, nikajaribu kuyafumbua macho yangu kutazama ili nione ni kina nani, ila ukungu mwingi uliojaa machoni mwangu sikuweza kuwaona vizuri.
“eddy”
Nilisikia sauti ikiniita masikioni mwangu, ambayo inaendana na sauti ya mke wangu phidaya, nikageuza shingo yangu kutazama sehemu inapo tokea sauti hiyo, nikawaona watu wawili wakiwa wamesimama huku mmoja akiwa amevalia mavazi meupe huku wapili nguo zake zikiwa na rangi mchangayiko.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni