Notifications
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (15)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA TANOTULIPOISHIA...Amatagaimba akarudisha upanga wake na kumpa mkono, akamwinua.“Wewe ni nani?” Amatagaimba akauliza.“Anna, naitwa Anna, Anna Davis,” akajitambulisha kwa sauti ya kukwamakwama.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...“We umeingiaje huku?” Amatagaimba akauliza tena mara hii kwa mshangao zaidi.“Nilikuwa na wenzangu, tulikuja ah, sijui hata kufanya nini, mimi nika,…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (14)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA NNETULIPOISHIA...Seidon alisimama kwa taabu, akaliendea fuvu lile lililokuwa chini katika mchanga, lakini kabla hajaliokota alibaki kinya wazi, pale lilipoangukia mchanga wote uliondoka na kufanya duara, kisha lile fuvu likaonekana likiwa juu ya kitu kama jiwe jeupe safi ambalo halikuwa na hata chembe ya vumbi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Seidon aliinama na kuokota…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (13)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA TATUTULIPOISHIA...“Nimeiona shida yako, nimesikia kilio chako lakini jambo moja ninaloweza kukwambia ni kwamba, nguvu zetu na nguvu za huku ni kinzani sana, nikikuahidi kukuvusha katika daraja la pepo nitakuwa mkaidi mbele ya watu wangu, kwa kukusaidia ewe shujaa wetu, nitakuonesha njia ya kuzunguka ambayo itakufikisha katika lango la Hamunaptra,IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (12)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA MBILITULIPOISHIA...“Seidon na Amatagaimba, nilikuwa nikiwasubiri kwa hamu kubwa mfike hapa, niliwaona tangu mbali na nia yenu njema, nifuateni,” Yule mzee akawaambia, Amatagaimba na Seidon wakatazamana kisha wakapeana ishara ya kumfuata wakaenda pamoja naye.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Mbele kidogo wakaingia kwenye piramidi moja dogo lakini lililoonekana kumegekamegeka…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (11)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA MOJATULIPOISHIA...“Orion,” Seidon akamwambia Amatagaimba huku akikimbia. Amatagaimba akasimama na kugeuka nyuma huku tayari akiwa na upanga wake mkononi, Seidon alizidi kukimbia bila kutazama nyuma. Amatagaimba alipigwa kikumbo kikali kabla hajautumia upanga wake, kwani kasi ya Yule farasi alishindwa kabisa kuidhibiti kwa upanga wake huo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (10)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMITULIPOISHIA...akaeuka ghafla na kukaa upande wa Seidon tayari upanga wake ulikuwa umekwishaondoa kichwa cha Yule jamaa, vurugu ikazuka kati ya watu wale na akina Amatagaimba, mapigano makali yakazuka, kila walipowakata kata na panga zao wale watu walizidi kuwa wengi na makelele yao yalikuwa yakiwasumbua masikio ya Amatagaimba na Seidon.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (9)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA TISATULIPOISHIA...“Seidon, hapa kuna kazi,” Amata ga Imba alimwambia Seidon, akageuka kumtazama akamuona ametulia kimya kama mtu anayetafakari kitu fulani. “Seidon, unawaza nini?” akamuuliza.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...“Amata ga Imba, tutafika hii safari kweli, maana naona vikwazo ni vingi sana, na ninaanza kukata tamaa,” Seidon alijibu.“Usikate tamaa, hakikisha unafika…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (8)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA NANETULIPOISHIA...Amata ga Imba alipoona giza hilo akajua kumekucha, akapiga mbinja kali na muda mfupi tu, farasi wale wawili walikuwa tayari wamefika, Seidon akarukia juu ya mmoja wapo na Amata vilevile kisha wakapiga mbio kuelekea upande wa kusini. Nyuma yao jeshi lilikuwa likija kwa kasi na farasi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...“Amatagaimba! Wanatufuata….” Seidon alipiga…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (7)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA SABATULIPOISHIA...“Amata, nakualika katika hili, ufuatane nami tukakamilishe kazi hii, tuondoe laana katika jamii na baraka za Klakos zitumwagikie kama umande wa asubuhi” Seidon alimtupia ombi Amata kwa lugha ya kushawishi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...“Hamna shaka, ombi lako limefika panapostahili, bega kwa bega tutakamilisha hilo, mimi nitakusindikiza kwa jua na mvua, kwa…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (6)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA SITATULIPOISHIA...Sauti za watu wakisali katika lugha isiyoeleweka zilisikika, Anna alitazama vyema na kuona viumbe kama watu wapatao kama ishirini hivi wakiwa wamezunguka kitu kama kitanda na katikati yake kulikuwa kumelazwa mwili wa binadamu ambao Anna aliutambua vyema, mwili wa rafiki yake kipezi Nesta.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Anna alibaki kakodoa macho akiangalia tukio…

HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (6)


SEHEMU YA SITA
TULIPOISHIA...
Sauti za watu wakisali katika lugha isiyoeleweka zilisikika, Anna alitazama vyema na kuona viumbe kama watu wapatao kama ishirini hivi wakiwa wamezunguka kitu kama kitanda na katikati yake kulikuwa kumelazwa mwili wa binadamu ambao Anna aliutambua vyema, mwili wa rafiki yake kipezi Nesta.

IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI

TUENDELEE...
Anna alibaki kakodoa macho akiangalia tukio lile lilivyoendelea kule chini, wale viumbe walipiga magoti wakisali na mmoja aliyeonekana kama kiongozi wao alisimama upande wa miguu wa ule mwili akiwa na kisu kikubwa mkononi mwake, alikuwa akimwagia unga Fulani juu ya mwili ule kuanzia miguuni kuelekea kichwani huku akisema maneno kwa kurudiarudia na alipofika kichwani alijaza unga ule usoni mwa mwili ule na kukiinua kisu chake tayari kwa kukata shingo.

Anna alipiga kelele za nguvu mara kuta zote zilianza kutikisika, na wale viumbe walionekana kukatisha ibada yao, walisimama na kutawanyika wakipandisha ngazi kuelekea juu alipokuwapo Anna, Anna alipogeuka akimbie alitandikwa kofi moja la nguvu lililompepesua na kumuangusha chini kwa haraka alinyanyuka na kusimama wima, mbele yake kulikuwa na ukuta na katika ukuta huo kulichorwa picha ya skeleton ya binadamu, hakujua ni nani aliyemchapa kofi lile, aliendelea kushangaa na hapo ndipo alipoushuhudia mchoro ule ukipata uhai, ukajitikisa na kujibandua pale kwenye ukuta na kukanyaga chini, kwa mwendo wa kustaajabisha ulianza kutembea kumuelekea Anna pale alipo.

Hamna la kufanya Anna kwa kujihami aliuchomoa mwenge uliokuwa umepachikwa katika moja ya kuta zilizopo hapo na kumtishia kiumbe huyo aliyeonekana kusimama kwa kuogopa. Anna alisikia vishindo vya wale viumbe wengine wakipanda ngazi zile kwa kasi akaona sasa hapo si pa kukaa tena lakini hakujua ni wapi hasa aelekee. Alitazama huku na huku akaona viumbe wale wanazidi kukaribia pale alipo, alijaribu kukimbia, lakini alipogeuka tu alipigwa kofi lingine la kisogoni lililomfanya ayumbe na kujigonga katika ukuta, aligeuka na kukabiliana na skeletoni ile ambayo ilikuwa ikitembea kuelekea alipo msichana huyu, Anna hakuwa na silaha zaidi ya mwenge ule uwakao aliurusha kumtupia kiumbe yule ambaye kabla hata hajafikiwa na moto ule alijizungusha na kugeuka mchanga uliotimka na kufanya vumbi jingi ndani mle. Anna aligeuka kukimbia lakini mbele yake wale viumbe waliotoka kule ibadani walikwishamfikia, walimzunguka.

Kutokana na urefu wa Anna aliweza kuwaona vizuri jinsi walivyo wafupi wenye macho ya kutisha na midomo iliyokuwa ikimwagika udenda mweusi mzito kila mara, Anna alichota mchanga na kuwamwagia kitendo kilichowafanya watawanyike, Anna aliokota tena ule mwenge uwakao na kuanza kukabiliana nao, aliushika kwa mikono miwili na kuuzungusha kwa kasi kitendo kilichofanya kuwapiga viumbe kama watatu kwa mfululizo na kuviangusha chini lakini bado vilikuwa vikija tena, alifanya tena kama mwanzo na kushuhudia kimojawapo kikilipuka kwa moto ule na kingine kikadaka mlipuko ule, Anna hakuona haja ya kuchelewa alipita katikati yao na kutimua mbio, bila kugeuka nyuma akiwa katika kasi hiyo mara mbele yake aliona ardhi ikifunguka na kwa kuwa alikuwa akikimbia alishindwa kusimama ghafla, alijaribu lakini alishindwa alijikuta akimezwa na shimo lile, akitumbukia ndani ya shimo hilo ambalo kwalo hakuona mwisho wake.

Alijibwaga kwenye lindi la mchanga, mahali asipopajua, aliketi akiegemea ukuta mkubwa nyuma yake, miguu yake aliikutanisha na tumbo lake na kujikunyata akitweta bila kujua la kufanya.

Seidon alidondoka katika mandhari tulivu, udongo laini ulifanya vumbi sawa na la saruji lililomfanya seidon kupiga chafya kadhaa, alitazama huku na kule na taratibu kuvuta hatua, mbele yake kulikuwa na mlango mkubwa na ndani yake aliona mwanga mkubwa uliojaza chumba hicho, Seidon kwa mwendo wa tahadhari alinyata na alipoukaribia mlango ule alisikia mlio wa kwato za farasi ukija upande wake alipogeuka alikutana na kamba nene inayoikaribia shingo yake aliinama na kamba hiyo ikamkosa, alipojiinua aliiona ncha ya mkuki ikimlenga kifuani akaepa, na mkuki ule ukajichomeka mchangani. Orion alikuwa amefika eneo hilo, Seidon akauwahi mkuki ule lakini kabla hajaushika aliona ukiwaka moto, akaamua kuuacha, kabla hajageuka alijikuta akikanyagwa na miguu ya mbele ya farasi wa Orion ambaye alikuwa amejinyanyua na kusimama kwa miguu miwili.

Seidon alidondoka mchangani na kutambaa kama mtoto, alitulia kidogo ili kumvuta Orion, Orion alisogea pale akiwa juu ya farasi wake, alimwangalia Seidon akiwa pale chini, Seidon alitulia kimya. Mara ghafla aligeuka na na kusimama bila kuchelewa aliuvuta upanga wa Orion kutoka kiunoni mwake na kuuzungusha kwa ustadi kitendo kilichosababisha farasi wa Orion kukatika miguu ya mbele kwa makali ya upanga ule. Orion alianguka chini na alipojiinua hakumuona Seidon. Seidon aliingia ndani ya chumba kile, mwanga uliojaa humo ndani ulimfanya kufinyafinya macho maana alishindwa kuuvumilia, kwa tabu aliliona fuvu la Cleopas limewekwa mahali na ndilo hasa lililokuwa likifanya mwanga ule, Seidon alilikimbilia na akajifungua kitamba chake cha kiuno ambacho kilikuwa na mfuko na kufunika fuvu lile, mara giza nene likatawala chumba kile.

Seidon alimuona Orion kwa mbali akiwa anaingia kwenye ule mlango, Seidon akajibana kimya kabisa, Orion aliingia mpaka ndani kabisa ya chumba kile lakini alimpita Seidon bila kumuona. Kwa mwendo wa taratibu Seidon aliulekea mlango, alihakikisha hafanyi kelele yoyote ili asimgutushe Orion, alifanikiwa kutoka nje na akapiga mbinja kali ya mtindo wake mara farasi wake akafika eneo lile, bila kuchelewa Seidon akapanda farasi na kuanza kutimua mbio, aliamua kupuuzia maagizo yote ya Sherhazad malkia wa Soria, na kuondoka kwa kupitia lango la maghalibi.

Mishumaa mikubwa yapata arobaini na saba ilikuwa imewashwa na kufanya mwanga wenye joto la kipekee ndani ya kasri la Sharhazad, malikia wa Soria, akiwa kwenye dirisha lake la ajabu, aliweza kuona ulimwengu wote isipokuwa upande wa nyuma yake, aliona kila kitu alichokifanya Seidon na jinsi alivyomgeuka, akasikitika na kusema, “Seidon ameamua kutugeuka, sasa ntamuonesha mimi ni nani,” Sherhazad alitoka kwenye dirisha lake la ajabu na kuketi kwenye kiti cha enzi akapiga makofi matatu na mara wazee wane wakaingia na vikorokoro vyao vya kichawi. Walipofika mbele yake wakaanguka kifudifudi na kutoa salamu hiyo ya heshima, Malkia wa Soria akawatazama na kuwaamuru wainuke, wakafanya hivyo, “Niwewaita, kuna kazi ngumu inatukabili mbele yetu, Cleopas, nataka fuvu la Cleopas, yule kijana niliyempa uwezo na maagizo ametugeuka, sasa nataka mumshughulikie na lile fuvu tulipate hapa haraka,” akasimama kutoka katika kiti chake na kujishika kiuno huku akiziruhusu nywele zake kumwagika sakafuni, akavuta hatua tano mpaka kwa mmoja wa wale wazee, akamshika bega na klumwambia, “Nataka kimbunga upande wa Maghalibi,”

Vumbi kubwa lilitimka, upepo wa kisulisuli ulinyanyua kila kitu, Seidon alipambana na upepo huo ambao ulitaka kumfanya farasi wake ashindwe kuendelea, lakini kadiri ya ujasiri wa Seidon alimuendesha farasi yule kwa ustadi kiasi kwamba upepo ule haukumsumbua.

Sherhazad akiwa kwenye dirisha lake la ajabu, alikasirika kwa kuona Seidon hapati shida na kimbunga kile, alisonya sonyo refu na kimbunga kile kikakatika ghafla, akageuka kumtazama mzee mwingine, “Mvua ya mawe” aliamuru tena. Mara anga likatanda wingu nene na mvua kubwa ya mawe ikaanguka, Seidon akiwa katika mwendo kasi aliiona mvua ile ikinyesha kumzunguka lakini alipo yeye hapakuwa na chochote, radi nazo zilijitahidi kupiga lakini wapi Seidon aliendelea kupiga mbio.

“Inaonekana Seidon kawa jeuri sasa, nampa pigo la mwisho, na hasara iwe kwetu sote. Wape akili waamke, Wahamsud na Wakalban”

Ndipo Seidon alipohisi anakimbizwa na watu wengi wenye farasi.

Amata alimtazama Seidon kwa huruma sana, akampa kikoto cha maji ya kunywa, Seidon akayanywa na kidogo akaonekana kupata nguvu.

“Seidon” Amata aliita. Seidon aliinua kichwa kuashiria itiko. Amata akanyanyuka kutoka pale alipokaa na kuelekea kwenye ukingo wa korongo kubwa sana, akageuka na kutazama pale alipomuacha Seidon, akafungua kinywa chake na kumueleza Seidon,

“Ninyi wote hamjui mnachopaswa kutenda, kulileta hilo fuvu la Cleopas kwenye ardhi yako ni kuongeza mikosi.”

Seidon aligutuka, akamkazia macho Amata,

“Amata, we wa wapi? Inaonekana hujui lolote juu ya fuvu hilo” Seidon alimueleza Amata huku akimtolea macho. Amata akacheka kidogo, akaitazama pete yake iliyokuwa iking’aa kwa rangi tofauti tofauti, akaushusha mkono wake.

“Seidon, fuvu la Cleopas linatakiwa lirudi kwa Cleopas. Kwa hiyo mwenye kupata baraka za Klakos ni yule atakayerudisha lile fuvu pale” Amata alimeza mate aliinua kibuyu chake cha maji na kugugumia mafunda kadhaa, akamuendea Seidon na alipomfikia akachuchumaa mbele yake, akamuuliza.

“Sikia, Unaijua Klakos ni nini?” Amata alimtupia swali Seidon, na Seidon alionesha ishara ya kwamba hajui.

“Vizuri sana, na wote hamjui, wote kabisa hamjui siri ya fuvu la Cleopas, sasa sikiliza, Cleopas na wenzake sita ndio walikuwa wakiiendesha dunia ya chini, dunia ya wafu, dunia ya waliolala, wao daima wamejipanga kwa mtindo huu, kushoto wapo watatu Aminus, Petrius na Segidus na kulia wapo watatu Sagitarius, Hesmepitus na Sectogamus, Cleopas yupo mbele katikati yao, ukiwaweka wote hivo ndio ule mkao wao unaitwa Klakos sasa waingereza miaka ile waling’oa fuvu la Cleopas ndiyo wakaleta ukame duniani maana chemchem, mito, mimea vyote si vinaota kutoka chini ni baraka za Klakos. Laana aliowapa ndio ile vita ya dunia huko Ulaya na matatizo mengine” Amata alimwangalia Seidon ambaye alionekana kukodoa macho tu.

“Umenielewa?” alimuuliza Seidon ambaye alibaki midomo wazi, “Sasa unatakiwa uchukue lile fuvu ulirudishe kule kwa Cleopas kwenye mji uliopotea, mji wa wafu, Hamunaptra, mji ulio chini ardhini”.

Seidon alishusha pumzi ndefu na kujiweka vizuri baada ya kusikia habari hiyo mpya.

Aligeuka pembeni na kuutazama upanga wake, upanga wa Vernad, akauinua na kuubusu

“Sikulijua hilo, na hakuna aliyewahi kuniambia” Seidon alimueleza Amata, aliuinua mkono wake na kuuweka begani kwa Amata “Wewe unatoka wapi?”

“Mimi natoka Bara la Giza, nchi isiyo na mwanga, Amata ga imba, shujaa wa msitu wa Solondo,” Amata alijitambulisha kwa ubabe huku akijipigapiga kifuani. Seidon alimtazama kwa makini kijana huyu mweusi aliyejiamini kuliko vile alivyo.

“Amata, nakualika katika hili, ufuatane nami tukakamilishe kazi hii, tuondoe laana katika jamii na baraka za Klakos zitumwagikie kama umande wa asubuhi” Seidon alimtupia ombi Amata kwa lugha ya kushawishi.

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU IJAYO
66 Hamunaptra Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni