Notifications
  • MY DIARY (3)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TATUTULIPOISHIA...Nazani sasa unanielewa ninaposema nilikuwa sina ndugu kwani baba yangu hakuwa na ndugu yeyeote zaidi ya marafiki ambao na wao kwa sasa ndio hao wameshagawana mali zote. Nimebaki mimi na dunia yangu hivyo basi nilimwomba rafiki yangu wa kufa na kuzikana kwa jina Joyce anisaidie kunisitiri nyumbani kwao.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Likizo ilipoisha tulirusi shuleni na…
  • MY DIARY (2)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA PILITULIPOISHIA...Kwa ufupi japo sitaki kueleza historia yake ila kwa sasa ni shoga na teja. Baba yetu alitupenda sana na alihakikisha tunapata elimu nzuri na bora. Mimi na kaka yangu wote tulisoma International school ya hapo Moshi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Baadaye kaka yangu alianza kuvuta bangi kitu ambacho kilimtia hofu baba yangu na kuamua kumpeleka kusoma nje ya nchi.Alikosea sana…
  • MY DIARY (1)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KWANZANilikuwa juu ya jukwaaa nikifanya vitu vyangu ili hali nikijua kabisa watu wote waliokuwa wakinitizama walikuwa wanaumia roho kutokana na mvuto wa umbo langu niliokuwa nao. Nilisikia mijibaba miwili ikiulizana hivi lile wowoo ni la kwake au ni la mchina? Mmoja wao akaropoka “wee kitu original hicho,kwani umemsaahau huyu binti tulishakutana nae kule Arusha mpaka tukambatiza jina la soda kubwa tena ya fanta yaani BAMBUCHA.?” Yeah nimekumbuka alidakia…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (18)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA NANETULIPOISHIA...“Mamaaaaaaaa!” Anna akapiga kelele na kutereza vibaya, miguu yake ikaliacha daraja, Seidon akawahi kukaza mikono na kumzuia, lakini miguu yake tayari ilikuwa imeacha daraja na sasa ikining’inia chini ya daraja. Anna akalia kwa uchungu sana, akijua kuwa mwisho wake sasa umefika.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...“Jipe moyo Anna, tumefika mwisho sasa,” Seidon…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (17)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA SABATULIPOISHIA...Amatagaimba kabla ya kuondoka akachukua maji kutoka kwa Seidon na kumpa Anna, akayanywa kwa fujo na kuyamaliza. Nguvu zikamrejea. Anna akapanda juu ya farasi na Amatagaimba akatua nyuma yake, safari ikaanza.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Seidon akapiga mbio kwa ustadi akipita vijilima vilivyo ndani yake, “Amatagaimba, Sherhazad na Wafuasi wake…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (16)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA SITATULIPOISHIA...Seidon alikuwa katika hali mbaya sana, kama ni kupambana basi alikuwa kapambana na jitu la kutisha linalowaka moto kila upande. Ilikuwa ni wakati wa kumaliza kazi aliyotumwa, akasikia radi zikipiga huku na huko, yule malaika wa moto akashtuka na akajua kwa vyovyote mvua itapiga hapo muda si mrefu, na kweli alipogeuka ulikotokea mlio ule.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (15)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA TANOTULIPOISHIA...Amatagaimba akarudisha upanga wake na kumpa mkono, akamwinua.“Wewe ni nani?” Amatagaimba akauliza.“Anna, naitwa Anna, Anna Davis,” akajitambulisha kwa sauti ya kukwamakwama.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...“We umeingiaje huku?” Amatagaimba akauliza tena mara hii kwa mshangao zaidi.“Nilikuwa na wenzangu, tulikuja ah, sijui hata kufanya nini, mimi nika,…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (14)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA NNETULIPOISHIA...Seidon alisimama kwa taabu, akaliendea fuvu lile lililokuwa chini katika mchanga, lakini kabla hajaliokota alibaki kinya wazi, pale lilipoangukia mchanga wote uliondoka na kufanya duara, kisha lile fuvu likaonekana likiwa juu ya kitu kama jiwe jeupe safi ambalo halikuwa na hata chembe ya vumbi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Seidon aliinama na kuokota…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (13)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA TATUTULIPOISHIA...“Nimeiona shida yako, nimesikia kilio chako lakini jambo moja ninaloweza kukwambia ni kwamba, nguvu zetu na nguvu za huku ni kinzani sana, nikikuahidi kukuvusha katika daraja la pepo nitakuwa mkaidi mbele ya watu wangu, kwa kukusaidia ewe shujaa wetu, nitakuonesha njia ya kuzunguka ambayo itakufikisha katika lango la Hamunaptra,IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (12)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA MBILITULIPOISHIA...“Seidon na Amatagaimba, nilikuwa nikiwasubiri kwa hamu kubwa mfike hapa, niliwaona tangu mbali na nia yenu njema, nifuateni,” Yule mzee akawaambia, Amatagaimba na Seidon wakatazamana kisha wakapeana ishara ya kumfuata wakaenda pamoja naye.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Mbele kidogo wakaingia kwenye piramidi moja dogo lakini lililoonekana kumegekamegeka…

HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (15)


SEHEMU YA KUMI NA TANO
TULIPOISHIA...
Amatagaimba akarudisha upanga wake na kumpa mkono, akamwinua.

“Wewe ni nani?” Amatagaimba akauliza.

“Anna, naitwa Anna, Anna Davis,” akajitambulisha kwa sauti ya kukwamakwama.

IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI

TUENDELEE...
“We umeingiaje huku?” Amatagaimba akauliza tena mara hii kwa mshangao zaidi.

“Nilikuwa na wenzangu, tulikuja ah, sijui hata kufanya nini, mimi nika, nika, ah, sikumbuki, kwani wewe ni nani?” Anna alijibu lakini alionekana kupoteza kumbukumbu. Amatagaimba alimtazama binti huyu aliyekuwa kachafuka mwili mzima kwa vumbi, nywele zote zilikuwa hazitamaniki jinsi zilivyo timtim. Alimuona wazi kuwa hawezi hata kusimama sawasaw kwa jinsi alivyochoka. Amatagaimba akamsaidia kunyanyuka.

“Nina kiu,” akamwambia Amatagaimba. Eneo hilo lote hakukuwa na maji Amatagaimba akapapasa kibuyu chake na kugundua kuwa hanacho, akajishika kiunoi lakini hakukata tama, kw akutumia pete yake ya ajabu aliiomba imletee maji, mara wakasikia radi kubwa ikipiga na sauti kama sauti ya maji ilisikika upande wa chini. Amatagaimba akamshika mkono Anna na kuondoka nae eneo lile, walielekea upande wa kaskazini nahuko wakakuta ngazi ndefu zikielekea chini, wakateremka nazo na huko walikuta maji yaliyokuwa yakitembea, maji yam to ambayo hayakuonekana yatokako wala yaendako. Anna aliyavamia na kunywa kwa pupa mpaka akapaliwa, mara akataka aoge kabisa, lakini Amatagaimba akamzuia kuwa hapo si mahala pake. Kila mtu aliporidhika wakapita kandokando yam to ule na kutokea upande mwingine ambako kulikuwa na ngazi nyingi zikipanda kuelekea juu, wakazikwea taratibu, Anna akiwa mbele na Amatagaimba akiwa nyuma. Baada ya kupanda ngazi kadhaa hawakusikia tena ule mto wa maji kama mwanzo. Ila walianza kusikia kelele za popo wengi waliokuwa ndani humo. Amatagaimba akamwambia Anna asimame, naye akasimama kisha yeye akaenda mbele na kutazama popo wale kwa makini sana, hawakuwa wakitikisika lakini walikuwa wakipiga kelele kama wanaoongea jambo Fulani. Amatagaimba akamgeukia Anna akamtazama kifuani, alikuwa amevaa kidani cha jiwe Tanzanite na hereni zake.

“Vua kidani, na hizo hereni pia,” Amatagaimba akamwambia Anna, naye akafanya hivyo bila kujua kwa nini anaambiwa hivyo.

Kisha wakaendelea kwenda mbele wakivuka lile eneo lenye popo wengi. Anna alijitahidi kumfuata Amatagaimba kila anakonkwenda, wakapita ndani ya mapango mengi mengine ya kutisha sana, walikutana na viumbe vya ajabu ajabu kila wapitapo, kwingine waligeuza njia, kwingine walijitahidi kupita hivyo. Ilikuwa ni kazi ngumu kuona njia ya kutokea nje.

“Tutatokaje humu Amatagaimba?” Anna akauliza huku akihema sana.

“Humu ndani hatutoki kwa kutumia njia za kawaida kama huko duniani…” Amatagaimba alianza kueleza.

“Sijakuelewa unasemaje?” Anna akauliza kwa mshangao.

“Nimesema, humu ndani hatutoki kama huko duniani, unajua sasa hivi upo miaka mingi nyuma! Mimi nilikotoka ni miaka 1200 iliyopita, na nilipotea kimiujiza kama wewe, hivi wewe sasa kama ulitoka duniani mwa elfu mbili na kitu basi sasa upo mwaka elfu moja na kitu, hivyo kutoka humu ni kupata miaka iliyobaki,” Amatagaimba alieleza lakini Anna hakuelewa kabisa somo hilo, “Ili kutoka humu inabidi ukumbuke mwaka uliotoka duniani halafu tupate dira ya kutuonesha uelekeo, na dira hiyo ipo kwenye mnyama hatari, mnyama ambaye ndiye anayeshika pande nne za dunia,” Amatagaimba alimuelea Anna vitu vya ajabu ambavyo kwake vilionekana kama havina maana.

“Kwani wewe umetoka wapi?” Anna akauliza.

“Mimi nimetoka duniani miaka mingi sana, nikaingia ulimwengu huu wa chini ya dunia tangu nikiwa katika msitu wa Solondo nilipotoka sikuweza kurudi kwani njia yangu ya kurudi imekuwa ngumu mno,” Amatagaimba akaeleza.

“Msitu wa Solondo!!!” Anna akashangaa kwa kusikia jina hilo.

“Ndiyo vipi unaufahamu?” Amatagaimba akauliza huku akimtazama binti huyu usoni.

“Siufahamu, na wala sijawahi kuuona kwa macho, ila nimeusoma kwenye kitabu cha riwaya kikibebwa kwa jina hilo, simulizi ya zamani sana hata mimi sikuwa nimezaliwa,” Anna akaeleza. Amatagaimba alimtazama mwanamke huyu mrefu, mwenye umbo shupavu.

“Ni nini kitabu hicho kimeeleza?” Amatagaimba akauliza huku akiwa amemshika mabegani Anna, wakitazamana uso kwa uso.

“Sasa ndiyo naelewa,” Anna akajibu na kuitoa mikono ya Amata kwa ghafla mabegani mwake, ‘Mzimu?!’ akajiuliza, Anna akaanza kutimua mbio.

“Anna!” Amatagaimba akaita, mara kuta zikaanza kutikisika, Amatagaimba akaanza kutimua mbio kumfuata Anna, akamfikia, kila alipojaribu kumshika mkono, Anna alijitoa katika mikono ya Amatagaimba na kutimua tena mbio, Amatagaimba hakumuacha, naye alimkimbiza, wakiwa katika kukimbizana kwenye ngazi hizo, mara lile jengo likaanza kutetemeka kana kwamba kuna kitu kizito kikipita juu yake. Amatagaimba akasimama na kutazama huku na kule wakati Anna aliingia kwenye mlango mmoja ulioonekana wazi. Alipoingia tu mlango ukajifunga, Anna akabaki ndani, hana ujanja, aliuendea mlango na kuanza kuupigapiga huku akilia na kuita.

“Amatagaimbaaaaaaaa!!!!! Nisaidie,” aliita kwa nguvu zote.

Haikuwa rahisi kwa Amatagaimba kuingia, mlango mkubwa wa jiwe ulikuwa umejikita, Amatagaimba, akajisjika kiuno hakujua la kufanya, akatazama huku na kule bado hakuweza kujua la kufanya. Mtikisiko ulikuwa ukiendelea, Amatagaimba ikambidi atoke eneo lile na kwenda upande mwingine, mbele kidogo tu dude la ajabu likatua mbele yake, shetani si shetani, jinni si jinni, lilikuwa ni kiumbe kikubwa kilichosimama kwa miguu miwili yenye kwato, mikono miwili yenye vidole vitatu kila mmoja, alikuwa mkubwa mara tano ya binadamu, na alionekana kuwa na uzito mkubwa, midomo yake ilikuwa kama ya bata na macho yenye kung’aa sana, katika tumbo lake kulikuwa na kitu kama goroli kubwa lililokuwa likitoa mionzi mbalimbali. Amatagaimba akarudi nyuma taratibu, akiweka nafasi kati yake na mnyama yule, huku akiangalia kile kitu mfano wa goroli.

Mara moja aligundua kuwa kitu kile ndicho hasa anachokitafuta ili kuweza kutoka nje ya shimo lile kubwa, kwani kinaweza kukuelekeza njia ya kutokea kutokana na nguvu yake iliyoshika pande nne za dunia. Lile limnyama likawa linamfuata polepole, lakini alichoshangaa halikuwa na nia ya kumdhuru. Amatagaimba akajikuta akiugonga ukuta nyuma yake, ikambidi kusimama, lile limnyama likamfuata mpaka pale, na kumuinamia, nyuso zao zikakutana, lile limyama likamtazama Amatagaimba, halikumfanya chochote. Mara kelele za Anna zikawa zina sikika kwa mbali, lile limnyama likageuka kuangalia kule zinakotokea kelele, kisha likamwangalia Amatagaimba, akatoa ukelele mkali ambao uloifanya vumbi litimke mle ndani, Amatagaimba akaanguka chini kwa woga. Lile limnyama likaanza kuvuta hatua kuelekea kule aliko Anna, Amatagaimba hakujua nini cha kufanya akatulia kusubiri aone. Kwenye ule ukuta kulikuwa na masanamu ya ya vichwa vya samba kuzunguka kote, lile limnyama likashika kichwa kimojawapo na kukikandamiza chini, mala lile lango la jiwe pale kwenye tundu alipoingia Anna likafunguka, Anna akatoka kwa kasi na kumkumbatia Amatagaimba aliyekuwa tayari amesimama wima akiangalia tukio lile.

“Anna,” Amatagaimba alipiga kelele huku akiwa amemdaka. Kisha wote wakageuka na kumtazama yule mnyama. Yule mnyama akaanza kuwasogelea tena tarataibu mpaka pale waliposimama, likawainamia na kunyanyua mkono wake mpka kwenye shingo ya Anna na kuushika mkufu wake wenye kito safi cha Tanzanite ya buluu, akaukata na kukitazama kwa makini kile kito, akatikisa kichwa, akatenganisha kito na mkufu, akachukua kito tu, kisha akamtazama Anna ambaye alikuwa ametulia tuli, kabla hajafanya lolote, Amatagaimba akamvua Anna heleni zake nazo zilikuwa na kito hichohicho akampa yule mnyama, yule mnyama akanguruma na kutikisa kichwa chake kisha akageuka kuondoka kwa hatua zake nzitonzito za kutisha. Amatagaimba na Anna walikuwa wamesimama, baada ya hatua kama tano hivi alikuwa amefikia ukuta ule mkubwa, akasimama na kugeuka nyuma akawaona Anna na Amatagaimba wakiwa palepale, akaunguruma na kuwapa ishara wamfuate, wakafanya hivyo.

Wakasimama palepale aliposimama, radi moja kubwa ikapiga kwa nguvu ndani mwote mkajaa mwanga, akamuonesha Amatagaimba jiwe kubwa lililojitokeza kama pande la tofari, Anna akapanda kisha yule mnyama akatikisa sanamu linguine na mawe ya mtindo ule yakatokeza mengi na kuyfanya ngazi kwenda upande wa juu, Anna na Amata wakazukwea kuelekekea juu ya shimo lile, akawapa ishara ya kuwa waondoke wakati yeye amekandamiza lile sanamu kwa mkono wake. Amatagaimba na Anna wakakwea kwa kukimbia kuelekea juu, zilikuwa ngazi nyingi ambazo unatakiwa uzipande kwa uangalifu sana. Muda si mrefu walijikuta wanatoikea mahala pendine kabisa. Anna alipotoka kwenye zile ngazi akaangukia kwenye mchanga mwororo ambao ulikuwa kama mchanga wa jangwani.

“Tumepona Amatagaimba,” Anna akamwambia Amatagaimba ambaye alikuwa akijvuta pale mchanagani nae akiwa hoi.

“Uhhhh!!!! Bado, kazi sijamaliza,” Amatagaimba akamwambia Anna, “Rafiki yangu sijui yuko wapi,” akajisemea.

“Rafiki?! Rafiki gani?” Anna akauliza.

“Ha, we unafikiri huku nimekuja peke yangu? Niko na mwenzangu, na tuko na kazi maalumu nab ado hatujaimaliza, sasa yapata nimtafute popote alipo ili tukamilishe misheni hiyo,” Amatagaimba alisema.

“Nyanyuka twende zetu hatutakiwi kulala hapa, tuko hatarini sana,” Amatagaimba akamwambia Anna na kisha wote wakaanza safari ya kutembea kwenye mchanga kuelekea wasikokujua.

§§§§§

Zamarad aliendelea kumtazama huyo kiumbe akimkabidhi fuvu lile Sherhazad, naye akawa akilipokea huku akitabasamu.

“Humsaing tuuunggg, seiduss seiduss” Zamaradi alitamka maneno hayo ambayo kwa kiwango chao katika ulimmwengu huo, ungeweza kujigeuza na kuwa kiumbe yoyote yule.. Mara upepo mkali ukaanza kuvuma ndani ya jengo lile. Zamaradi akageuka mwewe, akachomoka pale alipo na kulinyakuwa lile fuvu na kutoka nalo dirishani kwa kasi.

Sherhazad alitamani kulia kwa kuona Zamarad amemzidi ujanja katika hilo, akanyoosha mkono wake na kupewa uta wake wa kichawi, akaweka mshale juu yake na kuuvuta kwa nguvu, akautuma kwa maneno yasiyoeleka kwa lugha yake ya kijini, ule mshale ukaondoka kwa kasi kumfuata yule mwewe.

Seidon alikuwa katika hali mbaya sana, kama ni kupambana basi alikuwa kapambana na jitu la kutisha linalowaka moto kila upande. Ilikuwa ni wakati wa kumaliza kazi aliyotumwa, akasikia radi zikipiga huku na huko, yule malaika wa moto akashtuka na akajua kwa vyovyote mvua itapiga hapo muda si mrefu, na kweli alipogeuka ulikotokea mlio ule.

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU IJAYO
67 Hamunaptra Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni