Notifications
  • MY DIARY (6)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA SITATULIPOISHIA...Akanambia kuwa wamemwambia wapo East Africa Pub na tayari wamaeshaagiza mkuu wa mbuzi. Mmmmhhhh kusikia mguu wa mbuzi mate yalinijaa mdomoni. Basi kwa harakaharaka nikamwambia naomba niende niende nyumbani nikachukue viwalo vya club kisha nitawakuta hapo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alinambia mbona hizo nguo ulizofaa zipo poa tu wewe twende hivyo bhana si upo na…
  • MY DIARY (5)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TANOTULIPOISHIA...Akanisimamisha na kuanza kuiuliza maswali mengi yasiyo na maana huko akionekana kutojiamini. “samahani dada, sijui unaelekea wapi”? Nikamjibu dukani. Akavuta pumzi ndefu na kuniambia ok, nisaidie namba zako za simu. Nikamwangalia juu na chini nikwambaia nimezisahau na simu nimeiacha ndani nikirudi ndani nitakuletea..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Akaishiwa pozi akanambia,…
  • MY DIARY (4)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA NNETULIPOISHIA...Uchambuzi huu ulinigusa sana kwani hata mimi nilijihisi kuwa sikuwa na utando huo yaani bikira japo nilikuwa sijawahi kujamiana na mwanaume wa aina yeyote zaidi ya ile michezo ya utotoni ya kula mbakishie baba au ile ya kibabababa na kimamamama. Alianza kunishika mapajani na kunifanya nianze kusisimuka ajabu kwani japo alikuwa ni mwanaume mikono yake likuwa ni milani sana kama ya mtoto wa kike.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media…
  • MY DIARY (3)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TATUTULIPOISHIA...Nazani sasa unanielewa ninaposema nilikuwa sina ndugu kwani baba yangu hakuwa na ndugu yeyeote zaidi ya marafiki ambao na wao kwa sasa ndio hao wameshagawana mali zote. Nimebaki mimi na dunia yangu hivyo basi nilimwomba rafiki yangu wa kufa na kuzikana kwa jina Joyce anisaidie kunisitiri nyumbani kwao.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Likizo ilipoisha tulirusi shuleni na…
  • MY DIARY (2)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA PILITULIPOISHIA...Kwa ufupi japo sitaki kueleza historia yake ila kwa sasa ni shoga na teja. Baba yetu alitupenda sana na alihakikisha tunapata elimu nzuri na bora. Mimi na kaka yangu wote tulisoma International school ya hapo Moshi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Baadaye kaka yangu alianza kuvuta bangi kitu ambacho kilimtia hofu baba yangu na kuamua kumpeleka kusoma nje ya nchi.Alikosea sana…
  • MY DIARY (1)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KWANZANilikuwa juu ya jukwaaa nikifanya vitu vyangu ili hali nikijua kabisa watu wote waliokuwa wakinitizama walikuwa wanaumia roho kutokana na mvuto wa umbo langu niliokuwa nao. Nilisikia mijibaba miwili ikiulizana hivi lile wowoo ni la kwake au ni la mchina? Mmoja wao akaropoka “wee kitu original hicho,kwani umemsaahau huyu binti tulishakutana nae kule Arusha mpaka tukambatiza jina la soda kubwa tena ya fanta yaani BAMBUCHA.?” Yeah nimekumbuka alidakia…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (18)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA NANETULIPOISHIA...“Mamaaaaaaaa!” Anna akapiga kelele na kutereza vibaya, miguu yake ikaliacha daraja, Seidon akawahi kukaza mikono na kumzuia, lakini miguu yake tayari ilikuwa imeacha daraja na sasa ikining’inia chini ya daraja. Anna akalia kwa uchungu sana, akijua kuwa mwisho wake sasa umefika.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...“Jipe moyo Anna, tumefika mwisho sasa,” Seidon…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (17)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA SABATULIPOISHIA...Amatagaimba kabla ya kuondoka akachukua maji kutoka kwa Seidon na kumpa Anna, akayanywa kwa fujo na kuyamaliza. Nguvu zikamrejea. Anna akapanda juu ya farasi na Amatagaimba akatua nyuma yake, safari ikaanza.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Seidon akapiga mbio kwa ustadi akipita vijilima vilivyo ndani yake, “Amatagaimba, Sherhazad na Wafuasi wake…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (16)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA SITATULIPOISHIA...Seidon alikuwa katika hali mbaya sana, kama ni kupambana basi alikuwa kapambana na jitu la kutisha linalowaka moto kila upande. Ilikuwa ni wakati wa kumaliza kazi aliyotumwa, akasikia radi zikipiga huku na huko, yule malaika wa moto akashtuka na akajua kwa vyovyote mvua itapiga hapo muda si mrefu, na kweli alipogeuka ulikotokea mlio ule.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (15)
    Jina: HAMUNAPTRAMtunzi: Richard MwambeSEHEMU YA KUMI NA TANOTULIPOISHIA...Amatagaimba akarudisha upanga wake na kumpa mkono, akamwinua.“Wewe ni nani?” Amatagaimba akauliza.“Anna, naitwa Anna, Anna Davis,” akajitambulisha kwa sauti ya kukwamakwama.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...“We umeingiaje huku?” Amatagaimba akauliza tena mara hii kwa mshangao zaidi.“Nilikuwa na wenzangu, tulikuja ah, sijui hata kufanya nini, mimi nika,…

HAMUNAPTRA - MJI ULIOPOTEA (14)


SEHEMU YA KUMI NA NNE
TULIPOISHIA...
Seidon alisimama kwa taabu, akaliendea fuvu lile lililokuwa chini katika mchanga, lakini kabla hajaliokota alibaki kinya wazi, pale lilipoangukia mchanga wote uliondoka na kufanya duara, kisha lile fuvu likaonekana likiwa juu ya kitu kama jiwe jeupe safi ambalo halikuwa na hata chembe ya vumbi.

IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI

TUENDELEE...
Seidon aliinama na kuokota fuvu hilo kisha akalitia katika mfuko ule na kujifunga tena vizuri kabisa. akamsaidia na Amatagaimba kutembea kwa maana misuli ya mguu wake ilishtuka katika anguko lile. Orion hakuonekana tena, lakini hakuna aliyeamini kuwa kiumbe huyo kaisha waliona ni muujiza au kiini macho tu.

Wakiwa njiani kwa mwendo wa taratibu, mara kimbunga kikali kiwatokea mbele yao, vumbi na upepo wa kisulisuli ukawatenganisha wawili hawa, Seidon alikuwa mbele na Amatagaimba alikuwa nyuma, katikati yao palikuwa na vumbu jingi na upepo mkali.

“Tupatie hilo fuvu, haraka!” sauti kali ya kike ilimwambia Seidon.

“Hilo haliwezekani,” Seidon alikataa huku akiufuta upanga wake na kuukamata kwa nguvu kwa mikono yake miwili. Sauti kali ya muungurumo kama wa radi ikatawala pande zote. Seidon akiwa tayari kajiandaa kwa lolote, mara kwa mbali aliona vumbi jingine likitimka lakini hili lilikuwa dogo tu, kutoka katika vumbi lile alimuona mtu aliyepanda farasi akija kwa kasi sana upande wake. Mara utulivu mkubwa ukatawala eneo lile, akageuka nyuma.

“Amatagaimbaaaaa!!!!!” aliita bna kuita, lakini hakumuona Amatagaimba wala hakusikia sauti ya kuitika kwake. Walikuwa wametenganishwa katika njia ya kutatanisha. Seidon aliushusha upanga wake na kuupachika alani mwake. Msichana mrembo mwenye nywele ndefu kichwani mwake alisimama mbele ya Seidon akiwa juu ya farasi. Akamtazama Seidon kisha akateremka juu ya farasi huyo, alipotua chini katika ardhi, Seidon alihisi kama ardhi ikitikisika hivi, kisha ikatulia. Yule msichana akatabasamu, alijua kosa alilolifanya ambalo lingemgharimu baadae.

“Ewe kiumbe wa dunia? Ni wapi uendako hata udiriki kuvuka katika nchi hii isiyo yako?” Yule msichana akmuuliza.

“Ni nani wewe, hata kuniuliza swali kama hilo?” Seidon akajibu kwa swali.

“Sikiliza, hapa ulipo si sehemu salama kwako, nakuhurumia kwani hatari inayokukabili ni kubwa, panda kwenye farasi nikuvushe kisha nikuache uende zako,” yule msichana akamwambia Seidon bila kumjibu swali lake. Seidon akatulia kimya, akainama chini kisha akainua uso wake.

“Hapana, nitakwenda mwenyewe ninakotaka kwenda ama la jitambulishe kwangu kwanza hapo nitatimiza matakwa yako,” Seidon alimwambia Yule msichana.

“Mimi ni Zamaradi, kutoka mlima wa tatu kati ya mitano uionayo, nchi inayoishiwa na wasichana tu ambao wote ni bikra kwa kuwa hakuna mwanaume kwetu, napenda nikukaribishe kwetu ili uishi nasi japo kwa kipindi kifupi kisha nitakuonesha njia fupi ya kufika utakako,” Yule msichana alijitambulisha kwa Seidon kuwa yeye ni Zamaradi. Yule msichana akamsogelea Seidon jirani kabisa, harufu ya manukato aliyojipulizia yaliziburudisha pua za Seidon hata kuanza kujisahau.

“Kwani wewe unajua ninakokwenda?” Seidon akmuuliza.

“Sisi, ndiyo tunaotawala mawazo yote ya binadamu, naliiona nafsi yako tangu ikianza safari ya kuja huku, yuko wapi mwenzi wako? Tazama upepo mbaya umemchukua na hutomuona tena, yuko wapi Orion? Adui aliyewazuia njia, usikifikiri ni ninyi mliyempoteza bali ni jeshi kubwa lililokuzunguka nyuma yako, ambalo ndilo limemchukua rafiki yako wa safari, hapa limetulia kwa kuwa linaniogopa mimi, nikikuacha tu nawe utakuwa katika hali mbaya,” Zamaradi alimwambia Seidon, akageuka nyuma hakuona mtu.

“Mbona sioni chochote?” Seidon akamuuliza Zamaradi.

“Macho yenye damu hayawezi kuona kilichopo katika giza nene,” Zamaradi akajibu akamshika mkono Seidon na kukitazama kiganja chake, “Ooooh Hamunaptra, una safari ngumu sana kufika hamunaptra, nitakuonesha njia fupi zaidi,” akasema na kumuachia mkono wake.

Seidon alihisi kama anapigwa kwa shoti ya umeme, aliona vimulimuli vya radi kali vikipita mbele yake pale aliposhikwa mkono na Zamaradi.

‘…mshikane mkono na kiumbe chochote…’

Seidon alirudiwa na maneno hayo, na hapohapo akaona kosa alilolifanya. Zamaradi akamchukua na kumpandisha katika farasi wake kisha kupiga mbio pamoja nae.

Walipokuwa njiani Zamaradi akaingiwa na kitu kingine, yeye aliagizwa na Sherhazad akafanye hila ya kumpata Seidon baada ya kusaidiwa kutengenishwa watu hao, Zamaradi katika uwepo wake hakuwahi kuona mwanaume wa kibinaadamu, na sehemu anayoishi ni wanawake tupu, ulimwengu wa chini, akatamani kuonja mapenzi ya binadamu, akapiga mbio na kupita karibu na kabisa na miamba mikubwa sana ambayo haikuwa mbali na lango la Hamunaptra, pembezoni tu mwa Ikweta. Akasimamisha farasi wake.

“Na tupumzike hapa!” akamwambia Seidon huku akitangulia kwa hatua zake za ajabu mpaka ndani ya jiwe kubwa akaketi, “Keti hapa karibu nami,” akamwambia Seidon. Zamaradi alimtazama Seidon kwa jicho la uchu, akaanza kumshikashika shingoni, Seidon akaanza kuhisi raha ya ajabu ambayo hajawahi kuihisi maishani mwake, akatulia akiiruhusu mikono ya Zamaradi ifanye inachotaka.

Sheria au utaratibu wan chi ya Soria iliyopo katika ulimwengu wa chini, kunakoishi wanawake wengi ni kuwa hutakiwi kufanya mapenzi na mwanadamu ijpokuwa kwao ilikuwa ni kitu cha kifahari sana kama ukifanikiwa hilo. Wengi wao walipokujwa kwenye matembezi yao ya kificho walikuja duniani na kuwakwaza wanaume wengi kwa kuwapa utajiri mwingi lakini kwa sharti moja tu la kufanya nae mapenzi, na walikuwa na mapenzi mazito nay a dhati kuliko wanawake wa dunia hii, walikuwa na utamu usioelezeka katika kufanya mapezni walijua kumridhisha mwanaume kwa kila hali, watakufanya ukojoe kadiri unavyotaka na usijisikie kuchoka, sharti lao kwako ni moja tu, usimwambie mtu kama wao si binadamu na wala usiwe tena na mapenzi na binadamu wa kike, ukitimiza hayo watakupa kila kitu, wivu kwao ulikuwa ni ugonjwa. Lakini hawakutakiwa kufanya mapenzi na mwanadamu katika ardhi yao, hilo ndilo lilikuwa baya zaidi na hata hivyo hakuna mwanadamu aliyekanyaga ardhi yao bila idhini.

Zamaradi alitamani kuonja kile alichokisikia kwa wengine waliowahi kufanya hivyo, kutokana na umri wake na ubikira wake alisahau kabisa sharti moja la kutofanya mapenzi katika ardhi ile kwani unaitia najisi.

Akamfanyia maandalizi Seidon, maandalizi ya nguvu, Seidon alishangaa kwa raha inayoufunika mwili wake, sasa nay eye akatamani ale tunda hilo la ajabu, akamkumbatia kwa nguvu Zamaradi, lakini akashangaa vazi lake likitoweka na kubaki kama alivyo, Seidon akiwa katika shughuli nzito alihisi kama anapaa kwa jinsi alivyokolezwa na Zamaradi, naye Zamaradi hakuamini anachokipata kwani aliona raha isiyo kifani. Miguno na milio vya mahaba ikatawala, sauti ya Zamaradi ikazidi ile ya Seidoni, ikaanza kuwa sauti ya kutisha sana, sauti kama ya mnyama mkali mwenye uchu wa nyama, Seidon alipomtazama lo, alikuwa amekumbatia mnyama mbaya wa kutisha, mwenye meno makali na marefu, ulimi kama nyika uliogawanyika vipande viwili, miguu ya ng’ombe yenye manyonya yaliyosimama kama miba ya nungunungu, pembe mb I zenye ncha kali. Seidon aliogopa lakini alijikuta hawezi kubanduka kwa Yule mnyama, aliendelea kufanya mapenzi, raha ya penzi hakupotea, iliongezeka mara dufu.

Mara tetemeko la ardhi likaanza kuitikisa ardhi ile, likazidi na kuzidi, vipande vya mawe vikaanza kuwaangukia Seidon na mnyama Zamaradi, mara donge la moto likaja kutoka kusikojulikana, likavamia ndani ya pango lile, Zamaradi akatoa yowe kali la kutisha lililozidisha lile tetemeko, Seidon akaanguka kutoka kwa Yule mnyama na kutua chini kwa nguvu, fahamu zikamjia akatafuta huku na kule fuvu hakuliona lilikoelekea, akahisi kuchanganyikiwa, mara kwenye ule moto akatokea farasi mkubwa wa moto na juu yake kulikuwa na malaika wa moto, mwili wake ulitangenezwa kwa ndimi za moto, mikononi mwake alishika upanga wa moto. Sauti ya Zamaradi bado ilikuwa ikisikika kwa nguvu na ilikuwa ya kutisha kuliko mwanzo.

§§§§§

“Zamaradi umeniuzi, umekiuka masharti ya kazi niliyokutuma, adhabu yako unaijua, nitaiteketeza roho yako na kuitupa katika dimbwi la tope la ukaidi, huko utaishi milele kwa mateso na dhiki,” ilikuwa sauti ya Sherhazad ikimwambia Zamarad. Zamarad alimtazama Sherhazad kwa woga, akamwangukia na kumuomba msamaha lakini hakukuwa na kitu kama hicho, Zamaradi alikwishajua mwisho wake umefika, kwa kuwa alijua pia ambacho Seidon atafanyiwa na wenzake pindi akichukuliwa na malaika wa moto, akajaribu kuona cha kumsaidi kabla hajatupwa katika dimbwi hilo ambalo hukiingia hutoki tena kwani roho yako inageuka kama uji na kukutana na roho zingine za kale katika shida na dhiki kuu.

Wakati hayo yakiendelea, Zamarad alimuona kiumbe mwingine akimkabidhi fuvu lile Sherhazad alilolichukua kwa Seidon.

§§§§§

Mwaka 2010

Katika mapiramidi

Amatagaimba alianguka vibaya katika shimo kubwa lenye giza nene, akabwagika mchangani. Ilikuwa ngumu kwake hata kusimama baada ya shambulizi hilo alilolipata kwa ghafla kutoka kwa kiumbe ambacho hakukiona kwa macho, ila alikuwa akihisi tu mara anabebwa na mara anabwagwa chini, akatumbikizwa kwenye shimo refu na kujikuta huko. Alijaribu kujinyanyua lakini ilishindikana.

Alibaki pale chini akihema kwa nguvu na mhemo wake ulikuwa ukisafiri ndani ya shimo hilo kubwa, hakuwa na jinsi, macho yake yalipotulia akaona muali mwembamba wa nuru ya mwanga, akatambaa kama mtoto kuuelekea mwanga huo, Amatagaimba hakujua ni wapi alipo, aliendelea kutambaa huku akihema kwa nguvu, kiu nayo ilikuwa ni sehemu nyingine ya mateso yake.

Amatagaimba akafika katika ule muali wa mwanga, mara tu alipoufikia mkono wake ulikutana na ule mwanga ile pete yake ikang’aa na kufanya nuru katika shimo zima. Amatagiamba akasimama kwa miguu yake, akatzama huku na kule asipajue alipo.

“Niko wapi?” aliongea kwa sauti ya chini lakini ilionekana kusikika kila mahali, michoro iliyokuwa katika kuta za shimo lile ilianza kufungua vinywa vyao na kucheka kwa sauti kali iliyosababisha kuta zile kutikisika. Amatagaimba katika kona moja ya kuta za shimo lile aliona kama kitu kilichojikunja au mtu, hakujua hasa ni nini anachoiona. Akaufuta upanga wake na kujikongoka taratibu mpaka kwenye ile kona, macho yake hayakumuongopea, alikuwa mtu, mwanamke, akamshtua, na Yule mtu akageuka kumtazama ijapokuwa alikuwa na woga machoni pake. Amatagaimba akarudisha upanga wake na kumpa mkono, akamwinua.

“Wewe ni nani?” Amatagaimba akauliza.

“Anna, naitwa Anna, Anna Davis,” akajitambulisha kwa sauti ya kukwamakwama.

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU IJAYO
67 Hamunaptra Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni