MTAA WA TATU (37)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA THELATHINI NA SABA
Akiwa ndani ya gari ghafla kwenye siti ya pembeni kukaanza
kufuka moshi kwanza alishtuka tena akashtuka zaidi baada kutokezewa na kiumbe chenye sura ya baba
yake yani Mzee J Ikram
NIOMBE SAPOTI, BONYEZA TANGAZO LINALOKUJA NA KUJAA KWENYE SIMU YAKO WAKATI UKIFUNGUA SIMULIZI AU LILE LINALOKUWA KATIKATI YA SIMULIZI ZETUKABLA HAUJAIFUNGUA NDANI, PIA KUNA LILE LINAKUJA NA KUNG'ANG'ANIA HAPO CHINI, BONYEZA WALAU MARA 3-4 HIVI HIYO NDIO SAPOTI YAKO KWANGU, TAFADHALI NIPE NGUVU NAKUTEGEMEA SANA MSOMAJI WANGU
SASA ENDELEA...
Akafunga breaki ya gari ajabu gari haikuweza kusimama mwanaume akatamani
hata kuruka sema mlango wa gari haukufunguka wala vioo kila kitu kilijilock,
“Hafidhi kijana wangu embu punguza presha tambuwa kitu kimoja mimi ndio Baba yako wa ukweli ndio
ninae tumia nguvu zangu na maarifa yangu siku zote kukulinda wewe popote ulipo nimeweza kuifanya
sura yako isiweze kutambulika mbele ya wabaya wako, na wakutambuwe wale wenye nia nzuri tu juu
yako, Hafidhi naomba nikwambie kitu kimoja tu huyo binti alie kupigia simu anaitaji kukuuwa kisa na
mkasa umempa mimba nae hataki hicho kitu sasa basi kuwa makini huko uwendako’’……
Baada kuongea hivyo kiumbe kikapotea Hafidhi akajalibu kufunga blek gari ikasimama akatesti
kufunguwa mlango ukakubali.
Mwanaume ikabidi avute pumzi na kuzishusha “opsiii’’ na kuona kumbe ni kweli yeye si kiumbe cha
kawaida akaitowa simu yake na kumpigia Mariam na kumwambia “kusema kweli mpenzi huko sitoweza
kufika maana gari yangu imechemsha hapa Kigogo njia panda hapa. Kumbe ulikuwa uwongo mtupu yeye
katokea Kinondoni studio na hapo alipo yupo Kinondoni (B)
“please Rich naomba ufanye kila njia uweze kufika hakika nina shida muhimu sana na wewe!!!
Mariam akasisitiza zaidi akitaka Hafidhi afike viwanya vya Biafra.
Hafidhi akakata simu kwa kusema neno moja tu siwezi kufika"....
Mariam baada kuona simu imekatwa akaitaji kumpigia sema haikuweza kupatikana
Akabaki kusema ohoo shit! Huyu mpumbavu amekataa kuja ipo siku yake shenzi
time".....
“Mariam kwanini unataka kumuuwa Rich hivi hujui au hufahamu kama yule ni kipenzi changu mume wangu mtarajiwa
Baba wa mtoto wangu, ni kitu gani kakukosea?"
Binafsi Mariam akashtuka si kidogo baada kumuona Vivian kafika pale na kuongea maneno hayo kwa uchungu huku machozi yakimtoka,
Akashindwa amjibu kitu gani,
Akabaki kuweweseka,
“nijibu kitu gani amekukosea Niue mimi kwanza kisha yeye ndio afate niambie kosa lake huwenda nitaweza kukusaidia kumuuwa niambie please mdogo wangu!!!
Vivian akamkunja na kumtikisa Mariam nae akaanza kulia
“nisamehe Dada yangu ni kweli naitaji kumuuwa Rich na hakuna chaguwo lingine lazima afe!!!
“ndio afe kwa kosa gani sasa niambie niweke wazi kwanini afe"....
Mariam akabaki tena kimya
Vivian akaona kule kumtikisa haitoshi akaanza kumchapa vibao
Yani alimpiga makofi ya maana,
Umati wawatu ukajazana kushuhudia jinsi ugomvi wa mabinti hao
Yusra nae akafika na kuja kumzuia Vivian asiendelee kumpiga mwenzake kwa kifupi
Mariam alibaki kama zezeta fulani hivi hakuitaji kumzuia wala kumrudishia
Hafidhi nae akaingia kwa style ya kishindo ilikuwa ni mbinu moja wapo ya kuwakumbusha wao ni kina nani
Yani upepo ulivuma kila kona vumbi likatimka, huku watu wakiwa hawaamini kukiona kiumbe
Yule yani Ninja Short wakashikwa na taharuki hata Mariam akashtuka kutoka kwenye kutojielewa na kukaa sawa,
Kwa sauti ya kicheko na dharau kubwa
Hafidhi akaongea
“ha!ha!ha! Vivian- Yusra- Mariam nyinyi ni Wanawake mashupavu sana sijawai kuona mfano wake lakini mnataka kuipoteza sifa hiyo kwa vitu vya kipumbavu msijisahau
Kazi bado mbichi come on watoto wazuri njooni kwa mpenzi wenu niwanyonye midomo"......
Yani lilikuwa bonge la tusi kuambiwa vile kila mmoja akanyoosha mikono yao kumuelekezea Ninja yule
Bastora zikiwa mikononi mwao
“nyamaza mpumbavu mkubwa wewe ushatuona sisi mabibi zako mpaka umeanza kututania sio na huu ndio mwisho wako nyoosha mikono yako juu"....
Vivian kwa sauti ya ukali akazungumza hivyo na kutowa amri,
Hafidhi kwa upande wake hakutishika ndio kwanza akazidi kucheka
3Sisters wakatizama na kuamuwa kufyatuwa Risasi vyuma vya moto vikaanza kumfata Mwanaume akachumpa na kufanya kuzikwepa risasi zile kimbembe kikawa kwa wambea kama kule Kariakoo"...
Risasi zikatuwa miilini mwao
Wakati mrengwa akizikwepa na kupotea katika eneo hilo baada kupora pikipiki aina ya boxer Vivian nae akaiwai pikipiki yake aliyokuja nayo,
Wakati Yusra na Mariam wakiingia kwenye gari moja aliyokuja nayo Yusra ndani ya wilaya ya Kinondoni kulikuwa hakutoshi kabisa,
Hafidhi akiwa na ile pikipiki akachanja mbuga mpaka JKT na kutokea Kawe ukwamani akanyoosha na kuingia Lugalo
Tena ilikuwa siku ya Ijumaa jeshini kuna usafi,
Mwanaume akaingia kwa speed ya ajabu na kutokezea geti lingine yani karudi tena Kawe sokoni
Wanajeshi wakaona wee usitutanie umekuja kufanya fujo ndani ya kambi utajuta kutufahamu
“Yusra kwani huyu Hafidhi j Ikram amewezaje kutufahamu majina yetu maana ametutaja pale?"
Mariam akauliza swali sema hakuweza kujibiwa kwani mwenzake alikuwa makini kwenye usukani baada kutokezea geti lingine.
Hafidhi kwa speed ya ajabu akazidi kuchanja mbuga
Ghafla kitu kama bomu hivi kikaweza kusikika huku Hafidhi akirushwa hewani
yani pikipiki
Akatupwa kule baada taili ya mbele kupasuka Mwanaume akaenda kujibamiza kwenye ukuta wa nyumba moja hivi
Akaanza kuona kizunguzungu sijui kihindi hindi
Mwishoe akapoteza fahamu
Wanajeshi wakafika kina Vivian nao hao
wakamuweka mtu kati wakati mwenzao hajitambui kabisa
Hakika ajali kazini mwanaume leo kanaswa
Vivian ndio akawa wa kwanza kumsogelea akihitaji kumvua mask,,,,,,
Vivian akaweza kukisogelea kile kiumbe na kuishika ile Mask na kuivuwa.
Kila mmoja akashikwa na mshangao, kisha wakaanza kufurahi kwa pamoja.
Nikweli alikuwa ni yeye Hafidhi j Ikram huku sehemu ya kichwani kukivuja damu,
Wanajeshi wakataka kumchukua ili waende kumshukhulikia wao.
Sema kikosi cha 3Sisters wakapinga vikali kuhusu swala hilo yani haiwezekani waondoke nae polisi nao kutoka kituo cha Kawe wakafika eneo la tukio kwa mbwembwe zote, na kutaka kuubeba mwili wa Hafidhi uliokuwa umelala chini
Sijui amekufa au laa,
Kukawa na utata fulani hivi kila mmoja akihitaji kuondoka na mtuhumiwa
“embu tuacheni mzozo usiokuwa na faida cha umuhimu naomba tuwe makini
Na huyu kiumbe hatari sana
kwanza tumpeleke hospitali
Kisha tutajuwa nani wenye haki ya kubaki na huyu mtu"....
Vivian akatowa wazo hilo
kitendo bila kuchelewa Hafidhi akafikishwa ndani ya hospitali ya Lugalo akiwa hajitambui kabisa
Akapatiwa kitanda na kufungwa pingu kama akizinduka asiweze kukimbia.
Yani taarifa za kukamatwa kwake zilisambaa kama vile umeme au upepo wa kimbunga
“Ibnuwasi mwanangu nini unafanya wewe imekuwaje ukamuacha mjukuu wangu akaingia kwenye mikono ya watu wabaya?"
Bibi yake Hafidhi upande wa Ujinini akuliza hivyo kwa hasira
maana mjukuu wake kashikiliwa na serikali.
“hapana Mama, mjukuu wako
hakupata ajali ile kwa bahati mbaya ile ajali kajitakia mwenyewe"....
“Ibnuwasi unamaanisha nini kusema hivyo hivi kuna mtu anaependa ajali za kujitakia hakuna kitu kama hicho ndio kwanza nakusikia wewe ukisema kuna ajali za kujitakia"...
Yani bibi mtu alikuwa anaongea kwa kubwata huku macho yake yakifuka moshi yani yamekuwa mekundu si mchezo
“Mama naomba nikwambie kitu kimoja mjukuu wako
Ajali ile kajipangia kwa nia ya kuwapa heshima wazazi wenzie tu".....
“wazazi wenzie kivipi embu niweke wazi"
“Hafidhi kuna mabinti kama wawili kaweza kuwapa mimba na hao mabinti ndio wapo serikalini siku ya tukio walikuwa wakimfukuza yeye akajifanyisha kupata ajali na kuzimia kumbe hakuna chochote
Anawachora tu!"
“hahahaha kweli mjukuu wangu ni Kommando naomba nikuulize kitu Ibnuwasi nilikupa kazi gani na unafanya nini mpaka unamuacha
Hafidhi anatia mimba binaadamu?"
“nakumbuka ulinipa kazi ya kuchukuwa vizazi vya wanawake wote atakao tembea nao Hafidhi nina hakika kazi hiyo niliweza kuifanya vyema
kwa kuchoropowa mimba za wanawake wengi tu,
Mpaka ikafikia kuondoka na uhai wa binti mmoja anaeitwa Amina, nikaona kuanzia sasa inatosha wacha azae na binaadamu tu".
“sitaki kusikia kitu kama hicho yani haiwezekani azae na binaadamu wakati yeye ni Jini,
“hivi mama umesahau kama yeye ana homoni nyingi za kibinaadamu kuliko za kijini wacha nikampe msaada huko hospitali"
Kisha Ibnuwasi akapotea
Pembeni kidogo ya hospitali ya Lugalo
3Sisters walikuwa wamekaa wakiongea hili na lile kikubwa kuhusu kufanikisha kazi yao ngumu maana walishaanza kukata tamaa,,,,,"
Kuhusu kumnasa mtuhumiwa.
Vivian akatowa simu yake na kumpigia sijui nani
Ghafla simu nyingine ikaita nayo ilikuwa mfukoni mwake.
“Mbona nampigia simu Richard ajabu inaita hii ya muuwaji"
Vivian akaongea akiwa haamini kabisa akaitizama vizuri ile simu na kutaka kuanguwa kilio
“hapana haiwezekani yani huyu mshenzi awe kamuuwa Rich wangu kipenzi changu, baba watoto wangu, kisha kaichukuwa simu yake kudadeki wacha nikamtwange risasi"....
Vivian akaichomoa Bastora yake na kuanza kupiga hatua kadhaa kulisogelea jengo la hospitali, Yusra na mwenzake wakawai kumshika na kumzuia huku wakimsihi
Asifanye kitendo kama hicho kwani wapo kwenye imaya ya watu wengine,
Wasije wakafanya uvunjifu wa amani na kupindisha sheria
Vivian akatulia kimya huku akipanga kitu ndani ya moyo wake
Magari sijui bajaji na pikipiki ziliweza kupishana wote ulikuwa umati wawatu ukitaka kumuona huyo muuwaji kina Salma nao wakafika
sema hawakupata hata nafasi moja ya kumuona Hafidhi, kwani mwenzao alikuwa chini ya ulinzi mzito
wanajeshi walijazana mpaka utasema hiki nini kuna magaidi au,
“Beatrice shogaangu sasa itakuwaje juu ya shujaa wetu kunaswa"
Zay aliuliza hilo swali
“mi hata sijui cha kufanya hapa nilipo nimechanganyikiwa na huu mtumbo wangu"
“hivi Beatrice unataka kusema hii mimba ya Kambona kweli au?"
Salma nae akamuuliza swali Beatrice
“mmh! Kambona wapi hii mimba ya Hafidhi kwani aliweza kunipa mimba hii miezi kama miezi saba kabla hajaondoka kule mtaa wa tatu
Nikaona nimbambikie nani aweze kulea huu mzigo ndipo nikampata kambona.
Nikafanya haraka kukutana nae kimwili baada wiki nikamwambia Nina mimba yake basi akafurahi huyo
na kuahidi kunijengea nyumba kumbe kweli Wanaume wengine mazuzu"...
Kila mmoja akaanguwa kicheko cha kishambenga
“ha!ha!ha! Hallooo,,,hallooo endelea kushika mapembe maziwa anakamuwa mwingine
Hahahaha"....
Sauti nzito ndio ikawashtuwa ikiwaambia
“nyie mabinti acheni kelele zenu za uswahili tambuweni mpo wapi hapa shenzi zenu
Kisha yule mjeshi akaishia zake,
“mmh Salma umeona sura ya yule mkaka imekaa kama
Makalio yako ehee huwo mdomo kama mpododo wako unataka kunya eheee"
Zay alianza kumchokoza Salma
“Zay tuheshimiane ohoo mbona usemi buti lake kama ngozi ya kikwapa chako
mifuko ya shati lake imeshuka kama kitumbuwa chako".....
NAOMBA SAPOTI, KUNA MATANGAZO(ADS) YANAJITOKEZA KWENYE APP YETU, LIMOJA LINAJAA KWENYE KIOO CHAKO JINGINE LINANG'ANG'ANIA HAPO CHINI KABISA, BONYEZA JAPO MARA 2 AU 3 KILA UKIFUNGUA SIMULIZI HIYO ITANIPA NGUVU YA KUENDELEA ZAIDI NA SIMULIZI ZETU🙏🙏
TAZAMA KICHEKESHO HIKI KISHA BONYEZA SUBSCRIBE ILIYOPO CHINI YAKE WAKATI TUKIELEKEA KWENYE MUENDELEZO

USIKOSE SEHEMU YA THELATHINI NA NANE
Maoni, Ushauri na Chochote Share Namimi Katika Mawasiliano Haya:
+255 718 274 413 Ipo WhatsApp
+255 764 339 438
ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Maoni, Ushauri na Chochote Share Namimi Katika Mawasiliano Haya:
+255 718 274 413 Ipo WhatsApp
+255 764 339 438
ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni