Notifications
  • MY DIARY (37)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA SABATULIPOISHIA...Hapo alitulia tulii kama mtu aliyeaamia dunia ingine. Kimoyo moyo nikawa najisemeha kama amehamia dunia ingine na kuanza kuwaza ujinga sahuri yake mimi nipo kazini bwana acha nitafute hela. Ndio ni lazima nifanye kazi kwa utaalamu na utundu wa hali ya juu ili waendelee kusimuliana huko mjini ili niendelee kupata hela.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Wewe…
  • MY DIARY (36)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA SITATULIPOISHIA...Sasa wewe fikiria mimi niliyeletewa zawadi sikujua ni zawadi gani lakini yeye tayari alishafungua na kuchungulia na kujua nini kilifungwa huko ndani.Basi nikaendelea kumuhudumia yule mama huku na yeye akiniambia kuwa itabidi nikimmaliza hizo zawadi tusifungue hapo hapo na waniimbie wimbo wa happybirthday.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Tuliendelea na stori mbili…
  • MY DIARY (35)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA TANOTULIPOISHIA...Tatu niliambiwa kuwa ndugu zake na wazazi wake walihusika kwenye mipango hiyo hivyo walibariki kabisa huyo binti kuniacha mimi mumewe wa ndoa na kuamua mtoto wao aolewe upya. Nne ni kwamba huyo mzungu amewaamishia wazazi wake mjini na amewajengea nyumba ya kifahari.Kwa hiyo mimi ninavyowapigiana simu na kuwajulia hali kumbe wenzangu huwa wananichora tu.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (34)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA NANETULIPOISHIA...Hapo nikakumbuka kuwa zile zana zangu za kazi nilikuwa nazo ni vile vifaaa vya kupimia ukimwi ambavyo huwa navitumia kabla ya kukutana na mwanaume yeyote nisiyemfahamu. Nikaamua kumkubalia huku nikiamini kuwa hiyo ndo kinga yangu pekee iliyobaki kama mwanaume huyo atataka kuzini na mimi usiku huo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi tuliondoka na kwenda sehemu…
  • MY DIARY (33)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA TATUTULIPOISHIA...Nilikuwa nachanganya staili za kijamaika na hizi za kwetu, sikuacha pia zile za Nigeria hapo nikapata vitu vyangu vya tofauti kabisa. Basi baada ya kujihakikishia kuwa nipofiti kwa mastahili yangu hayo nilisubiri siku ya shindano ifike nikafanye yangu. Siku ya shindano ilifika na mimi nilikuwa miongoni mwa washiriki walioingia tatu bora.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (32)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA MBILITULIPOISHIA...Lakini kuchepuka kwangu na kuingia mgombani haikumaanisha kuwa sheria ingeniacha hivi hivi.Ilifika mahali ikabidi nizime gari na kutulia tulii kusikilizia nini kitafuata.Tayari nilikuwa nimezungukwa na mapolisi ambao walikuwa wakinifuatilia kwa kutumia pikipiki.Kwa bahati nzuri dereva wa lile gari na yeye alishafika hapo na alishawaambia polisi kuwa mimi naugua ukichaa na nilifufuka kutoka mochwari.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA…
  • MY DIARY (31)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA MOJATULIPOISHIA...“marehemu pia alinieleza kuwa ana miliki duka la vitu vya urembo wa kike ambalo pia Leah analisimamia ila hilo apewe mdogo wake Marry ambaye yupo hapa. Mama mdogo huyo mara baada ya kuyasema hayo alikaa zake chini. Baba mdogo ambaye hakurizika na maelezo hayo alisimama na kusema “kwa hiyo kama marehemu alijua kuwa atakufa hivi karibuni kwani nini hakufuata taratibu za kisheria za kuandika wosia na kurithisha mali.IKIWA UNASOMA…
  • MY DIARY (30)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINITULIPOISHIA...Baada ya hapo Nnilimwomba mama mdogo ajikaze na kuwatarifu ndugu wengine habari hizo za msiba.Tulisaidiana hivyo hivyo maana sio siri kila mmoja alikuwa na uchungu sana kutokana na mazingira ya kifo hicho. Habari zilizidi kusambaa kwa kasi na majirani walianza kukusanyika hapo kwa mama mdogo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Msiba ni msiba tu na ukitaka kujua binadamu…
  • MY DIARY (29)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TISATULIPOISHIA...Hapo sasa nikazidi kuchanganyikiwa ikabidi nimuulize mama huyo alikuwa akifanyia shughuli zake za kujipatia kipato sehemu gani.? Yule dada akanambia kuwa anafanyia soko la ndizi huko Korongoni. Sikuwa na jinsi nilimuomba anipeleke lakini na yeye alisita sita kwa madai kuwa alikuwa na kazi nyingi za kufanya na bado anatakiwa ampeleke mtoto shule.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (28)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NANETULIPOISHIA...Sisi tumesomea mambo haya bhana waliendela kuzungumza wale walinzi huku wakishuka ngazi kwa polepole. Hapo na mimi nikawa nimejifunza kitu kuwa kumbe unaweza kuingia na mtu guest akakuzuru kisha akaondoka zake.Sasa sijui kwenye zile guest zetu za uswahilini kama wanalijua hili.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi nilala japo usingizi ulikuwa hautaki kuja kwa…

SUZAN WANGU (2)

Mwandishi: Michael Michael

SEHEMU YA PILI
Baaada ya kumaliza kuongea na boss wake alirudi kitandani na kulala huku akiwa na mawazo sana, baadae alikata shauri na kuendelea na kazi ndogondogo za nyumbani huku akimsubiri Michael aje ili amueleze kilichomkuta….
**** **** ******
Siku zote katika maisha sio kila mtu atafurahi kuona mafanikio yako

SASA ENDELEA...
Wengine huchukia na kutamani ushuke na uwe masikine wa kutupwa, hivyo ndivyo ilivyokua kwa michael, sio kila mtu pale anapofanyia kazi alifurahia mafanikio yake japo ni wachache ambao hawakufurahishwa na mafanikio yake, wengi walimpenda hasa kutokana na ucheshi wake pamoja na upole wake, mbali na hilo pia michael alikua ni mshauri mzuri sana pale ofisini kwa wafanyakazi wenzake, endapo mfanyakazi yeyote alimfata na kumuomba ushauri, michael alimshauri vizuri na hata wakati mwingine kama mfanyakazi alikua anamatatizo, michael alidiriki kutoa pesa katika mshahara wake na kumsaidia huyo mfanyakazi ili atatue matatizo yako, havyo ndivyo jinsi michael alivyoishi na wafanyakazi wenzake.
Mbali na vyote hivyo vizuri ambavyo michael alikua akiwafanyia wafanyakazi wenzake, hali ilikua tofauti kwa Joel ambae alikua ni muhasibu msaidizi, alimchukia sana michael, tena alimchukia kupita kiasi, siku zote hakupenda mafanikio ya michael, alitamani mafanikio yale yawe kwake, siku zote aliweka tabasamu feki alipokua na michael, lakini moyoni mwake alimchukia kupita kiasi, uzuri ni kwamba michael alilitambua hilo na siku zote alijifanya kama haelewi kinachoendelea, alimpenda joel na alihuzunika pia kwanini joel alimchukia vile.
Siku hiyo walipomaliza kazi alimsubiria boss wake mr Alex ili amwambie kinachoendelea kati yake yeye na joel ili siku likija kutokea tatizo basi wajue pakuanzia. Alipomaliza maliza kupanga kazi zake alitoka na kwenda kwenye ofisi ya Mr Alex na kugonga mlango, aliruhusiwa kuingia….
“Ooo karibu mwanangu”
“Asante baba pole na kazi”
“Nashukuru pole na wewe”
“Aaaa baba nilikua na maongezi na wewe kidogo kama hutojali”
“Ebu keti kwanza hapo ngoja nimalizie hii kazi hapa halafu tuongee, kwani ni maongezi marefu sana?”
“Hapana ya kawaida tu na mafupi pia’
“Okay subiri kidogo”
Michael alisubiri na baada ya dakika kumi mr Alex alimaliza kazi zake…
“Sasa mwanangu tunaweza tukaongea”
“Baba ni kuhusu joel”…

“Joel yupi, yule muhasibu msaidizi?”
“Ndio baba”
“Enhe kafanyaje tena”
“Baba joel amekuwa akinichukia sana tangu mlivyonizawadia nyumba pamoja na magari, sasa nahofia siku ya siku anaweza akafanya jambo ambalo linaweza likaniweka mimi katika wakati mgumu au akaiweka ofisi katika wakati mgumu”
“Eeee kumbe kijana mbaya sana yule, kwanini akuchukie mwanangu, wewe umezawadiwa vile kutokana na utendaji wako mzuri wa kazi,sasa kwanini akuchukie, ngoja nitamfukuza kazi”
Hakika Mr Alex alichukia sana, hakupenda kuona mtu akimkwaza michael, kwani alimpenda kama mwanae…
“Hapana baba usimfukuze mwache tuu, jaribu kumuita na kumshauri itakua bora zaidi ya kumfukuza”
Mbali na yote mr alex alimsikiliza sana michael kwani alimuona pia ni mtu mwenye busara…
“Sawa nimekuelewa mwanangu, unaweza kwenda”
“Sawa baba jioni njema,msalimie mama”
“Usijali zimefika, kuwa muangalifu”
“Okay bye” Michael alimuaga bosi wake na kutoka nje kwakua muda wa kazi ulikua umeisha, alienda mpaka parking ya magari akaingia kwenye gari, akawasha gari lake na safari ya kuelekea nyumbani kwake ilianza…
******** ***** ********
Kutokana na foleni iliyokuwepo siku hiyo ya jumatatu, michael alifika nyumbani kwake mida ya saa moja na nusu, kama kawaida alitoa kirimoti kidogo katika mfuko wa suruali yake kasha akakibonyeza na geti lilifunguka, hapo alikanyaga mafuta taratibu na kuingiza gari lake aina ya prado, alibonyeza tena kirimoti na geti lilijifunga, alisogeza gari mpaka sehemu ya parking na kuliweka sehemu yake, na baada ya hapo alifunga vioo pamoja na milango ya gari na alipomaliza alielekea upande ambao ndiko ulipo mlango wa kuingilia ndani kwake, alifungua mlango na kuingia ndani lakini alishangazwa na ukimya uliokuwepo hapo ndani, alipita sebuleni na kukuta chakula kipo mezani lakini alipojaribu kumuita mpenzi wake suzan bado kuliendelea kuwa na hali ya utulivu, alitoka hapo sebuleni na kuelekea katika chumba chake, hapo alipigwa na butwaa baada ya kumuona suzan akiwa amelala na jinsi alivyoonekana ilionesha wazi kuwa hakutoka siku hiyo, michael alipatwa na wasiwasi na kudhani huenda kuwa mpenzi wake anaumwa, michael alisogea mpaka karibu na kitanda alicho lala mpenzi wake na kumuamsha kwa ustaarabu, suzan aliamka kivivu, alikutana na tabasamu murua la michael na bila kutarajia alijikuta akimrukia na kumkumbatia kwa nguvu, baada ya muda wa kama dakika moja huku suzan akiwa bado amemkumbatia michael, suzan alianza kudondosha machozi kuonesha kwamba kuna kitu kinamsumbua, michael aligundua kuwa suzan atakua analia baada ya kuhisi shati lake alilokuwa amelivaa limenza kupata hali ya ubichi, alijitoa katika kumbatio lile na hapo alikutana na uso wa suzan ukiwa umependezeshwa na machozi, michael alipagawa na asijue mpenzi wake amepatwa na nini, mambo mengi sana yalipita katika kichwa chake na kuhisi huenda tayari kuna vijidudu watu washaingia katika penzi lake na hapo tayari mpenzi wake ashapewa maneno ya uongo kuwa yeye kuna mtu anatembea nae, alitoka katika dimbwi hilo la mawazo baada ya suzan kuanza kulia kilio cha kwikwi, michael alimfuta machozo mpenzi wake na kumuuliza ni kitu gani kinamsibu, suzan hakuongea bali alitoa simu yake aina ya Samsung galax s6+ na kufungua sehemu ya ujumbe mfupi (message) hapo alitafuta ujumbe aliotumiwa na bosi wake na baada ya hapo alimkabidhi michael ile simu,michael aliipokea ile simu na kuanza kuusoma ule ujumbe mfupi, na hapo macho yalimtoka pima baada ya kuona ujumbe ule…
“Kuanzia leo sitaki kukuona katika ofisi yangu, nimekufukuza kazi kwasababu zangu binafsi, na wala usijisumbue kuja katika ofisi yangu kama unajipenda maana unaweza ukaozea mahabusu, ila kama utakua tayari kunivulia nguo yako ya ndani na kunipanulia mapaja yako unaweza ukapata kazi, kwa kifupi nalihitaji penzi lako ili uokoe kazi yako”
Michael alishusha pumzi ndefu baada ya kumaliza kusoma ujumbe huo, alimtazama mpenzi wake ambae alikua akilia taratibu huku akivuta kamasi jembamba ambalo lilikua likitaka kutoka, michael alisikitika sana na alichukia kupita kiasi kwani hakupenda hata siku moja kumuona mpenzi wake akipata tatizo lolote kipindi ambcho yeye yu hai, alimpenda na alimthamini kuliko kitu chochote chini ya jua, licha ya suzan kuwa mpenzi wake pia alikua akimchukulia kama ndugu, licha ya suzan kuwa mpenzi alimchukulia kama mtu wa karibu kwake na pia alimchukulia kama mshauri wake mkubwa, alimtazama suzan ambae bado alikua akilia na hapo alipatwa na uchungu mkubwa moyoni mwake, alifikiria ni jinsi gani atamsaidia mpenzi wake, alifahamu fika kwamba suzan hana baba wala mama, hana kaka wala dada, hana mjomba wala shangazi, hana ndugu yeyote ambae alikua akimtegemea katika maisha yake, nguzo zake zote muhimu tayari alishazizika, na hapo michael ndipo alipogundua kuwa jukumu la kumsaidia suzan ni la kwake yeye mwenyewe, alitambua kuwa yeye ndiye nguzo pekee ambayo suzan anaitegemea, aliirudisha simu mahala pake na kisha alivua nguo zake na kupanda kitandani, alimvuta suzan karibu yake na kumlaza katika kifua chake….
“Suzan mpenzi wangu, yakupasa utambue kwamba katika maisha kuna changamoto nyingi sana ambazo binaadamu huwa tunakutana nazo, na ili ufanikiwe huna budi kupambana na changamoto hizo kwa nguvu zako zote ili ufanikishe malengo yako, kufukuzwa kazi wewe haimaanishi kwamba ndio mwisho wa maisha yako, yakupasa kukaa chini na kumshukuru mungu wako kwa kila jambo kwani huwezi jua mungu amekuepushia nini katika kampuni hiyo”
“Unayo yasema michael ni sawa sijakataa ila kwanini litokeee kwangu, mbona kila siku mimi ndo nakuwa napatwa na matatizo, nilipoteza wazazi wangu kipindi nimefikisha miaka miwili tuu, ndugu zangu siku bahatika kuwajua hata mmoja niliishi kama chokoraa mpaka nilipokuja kupata msaada kutoka kwa wasamaria wema ambao walinipeleka katika kituo cha kulelea watoto yatima ambao ndio walionigharamikia mpaka mimi kufikia hapa halafu leo mtu ananifukuza kazi kisa anataka afanye ngono na mimi, kwanini mimi? Eee mungu nimekukosea nini mpaka unanitenda haya, nibora uichukue roho yangu kuliko kuniacha hivi na kunipa mitihani kila siku”
“Paaaaa” ulisikika mlio wa kofi, naam ni kofi mwanana kabisa kutoka kwa michael lililotua vyema katika shavu la suzan, suzan hakuamini, tangu wajuane na michael na kukaa katika mahusiano kwa muda wa miaka mitatu hakuna hata siku moja ambayo michael aliwahi kumpiga hiyo ndo ilikua mara yake ya kwanza kupigwa na michael, alishika shavu lake na kukutana na sura ya michael ikiwa na makunyanzi huku macho yake yakiwa mekundu utadhani ametoka kuvuta bangi, hii ilitosha kabisa kumjulisha suzan kuwa michael alikuwa ana hasira kupita kiasi, licha ya suzan kupigwa kofi hilo hakuthubutu kuinua mdomo wake, alikaa kimya na kusubiri kusikia Michaela ataongea nini na ni kwasababu gani michael ampige kofi…

“Wakati mwingine uwe unalalamika lakini usivuke mipaka kiasi cha kumkufuru mungu namna hiyo, haijalishi nimangapi umeyapitia na mangapi utayapitia, kinachotakiwa ni wewe kumshukuru mungu kwa kila hatua unayopiga kwani huwezi jua mungu amekuandalia nini mpaka wewe upitie katika magumu hayo au huwezi kujua mungu amekuepusha na nini mpaka akaamua upitie hayo magumu, hivyo ni bora ukamshukuru mungu wako kwa kila hatua unayopiga katika maisha yako” michael aliunguruma kwa sauti nzito kiasi, suzan alikaa na kuyatafakari maneno hayo na kuona kwamba ni wazi atakua amemkosea bwana mungu wake, alifunga macho yake na kuanza kuomba kwa imani….
“Baba katika jina yesu, nakuja mbele za uso wako saa na wakati kama huu, tazama baba mimi ni mkosaji mbele zako, naomba unisamehe kwa niliyoyafanya na kutenda baba, tazama baba katika neno lako umesema samehe saba mara sabini na mimi ni mkosaji nahitaji msamaha wako, nakwenda kumfunga muovu shetani akae mbali katika maisha yangu, naomba unitakase kwa jina lako, unilinde kwa damu ya yesu, uniweke mkono wako wa kuume baba yako, nikatika jina la yesu mnazareti mwana wa mungu aliye hai nikiomba na kushukuru, aaamen”
Baada ya kumaliza maombi yale, suzan alishuka kitandani na kupiga magoti huku machozi yakimtoka..
“Michael mpenzi wangu, najua nimekosea, halikuwa kusudio langu kumkufuru mungu, nilikua najaribu tuu kuelezea hisia zangu na kuonyesha ni mambo mangapi mimi nimepitia”

KUNA MATANGAZO YANATOKEA KWENYE APPLICATION YETU HIVYO UKIYAONA NAOMBA BONYEZA HAPO NDIO UNANIPA SAPOTI MIMI, UKIBONYEZA UNAWEZA KUCANCEL SIO LAZIMA UENDELE ULIKOPELEKWA, KIKUBWA UBONYEZE HATA MARA 2-3 KILA UKIFUNGUA APP YETU


TAZAMA KICHEKESHO HIKI KISHA BONYEZA SUBSCRIBE ILIYOPO CHINI YAKE WAKATI TUKIELEKEA KWENYE MUENDELEZO

11 Simulizi Suzan Wangu
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni