Notifications
  • THE NIGHTMARE (9)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA TISAILIPOISHIA...“mmenifananisha, mimi ndio kwanza naigia ofisini mida hii.” Aliongea yule afande na kuigia kituoni.“sasa aliyekuwa anatuhoji ni nani kama sio huyo?”Alijikuta anajiuliza mwenyewe swali lililompa utata mkubwa kichwani mwake.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Wakati wakiwa hawajui hili wala lile, walishangaa kuona maaskari wakijazana pale na ambulance ikafika…
  • THE NIGHTMARE (8)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA NANEILIPOISHIA...Walipofika feri, walipewa nahodha mwingine tofauti na yule aliyemuota na boti ilikuwa ndogo tu ya kawaida tofauti na ile aliyoiota.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Sharji alijikuta anapiga makelele baada ya kumuona Balqis akiwa amejaa damu mdomoni huku ametoa makucha yake akimfata kwa nia ya kumdhuru.“AAAAAAAAAAAGH”Sharji alipiga kelele na kukurupuka.…
  • THE NIGHTMARE (7)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA SABAILIPOISHIA...“kha!!!!”Ulikua mshangao mkubwa kwa watu karibu wote baada ya kumuona Sharji akiwa na taulo akitoka chumbani kwa Balqis.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Wengine walicheka na kaka yake alionekana kutoifurahia hali ile.“sasa wewe unatutia wasi wasi bure, si ungesema tu kama unaenda kulala kwa huyu dada?” aliongea kaka yake na kukirudia kile chumba alichompangia…
  • THE NIGHTMARE (6)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA SITAILIPOISHIA...“toa loud speaker bwana.”Aliongea Balqis baada ya Sharji kubonyeza kitufe cha kupaza sauti.“kwanini hutaki nisikie maongezi yenu?” aliongea Karimu kwa sauti ya ukali kidogo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...“kwani kuna ubaya mimi nikiongea private na mdogo wako?” alijibu Balqis baada ya kuisikia sauti ya Karimu.“hakuna ubaya.” Alijibu Karim kwa sauti ya…
  • THE NIGHTMARE (5)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA TANOILIPOISHIA...Alijikuta outomatic akijisemea kwa mshangao baada ya kumuona dada mmoja mrembo mwenye asili ya kiarabu akiingia mule ndani. Hakuvaa ushungi kama alivyowazoea kuwaona waarabu wengi ambao alikutana nao. Huyu alivaa suruali ya jeanz nyeusi na juu akiwa na kikoti chake cheusi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Kati kati kulikua na nguo Fulani nyeupe iliyonakshiwa…
  • THE NIGHTMARE (4)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA NNEILIPOISHIA...Aliongea Khalidi na kuufungua mkanda wa suruali yake na kuanza kumtandika Karim.“unanipiga mimi?...utaona!”IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Aliongea Karim na kuondoka huku analia.*****************************Zilipita wiki mbili bila ya Karim kuonekana nyumbani kwao. Sabra alisikitika kidogo kutokana na kuwapenda sana watoto wake japokuwa huyo mtoto mkubwa hakuwa…
  • Fumanizi la Mchepuko Mwizi😂 | Comedy
    Mume amefuma viatu vya mchepuko wa mke wake mlangoni lakini akakosea kuingia ndani kabla aweke umakini kwenye hivyo viatu mwisho wa siku akaibiwa na vyake😂Hili tukio lazima lichukuchekeshe sana hata kama ulikuwa haujataka kuchekaItazame kisha nipe like na ukinipa maoni kwenye comment nitashukuru sanaUsisahau kubonyeza Subscribe kama haujajiunga na fungua #ChekanaZephiline kupata video zangu zote ambazo zipo mtandaoniNashukuru sana kwa wewe ambaye unanipa nguvu ya kuendelea kuwaletea kazi nzuri…
  • THE NIGHTMARE (3)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA TATUILIPOISHIA...Akiwa hewani akikata mawingu kurudi Tanzania, kichwa chake kilikua na mawazo mengi sana juu ya mume wake. Aliikumbuka siku waliyofunga ndoa.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Pia alijua kwanini mume wake alipendelea kufanya kazi uingereza na yeye kumfungulia ofisi huku huku Tanzania. Hakujua kuwa kazi anayoifanya mumewe ni ile ya kutembea na tajiri mkubwa…
  • THE NIGHTMARE (2)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA PILIILIPOISHIA...Khalidi alishangaa kuitwa na mtu asiyemfahamu. Alitoka na kwenda kumuangalia huyo mtu maana kiukweli hakua na ndugu aishie hapa Dar hata mmoja anayemfahamu..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈ENDELEA...Alipigwa na butwaa baada ya kumuona Sabra pale.“ahsante mungu.” Aliongea Khalidi baada ya kumuona tu yule binti pale.“pole sasa kaka yangu, nisamahe mie.” Aliongea Sabra kwa…
  • THE NIGHTMARE (1)
    Jina: THE NIGHTMAREMtunzi: Hussein O MolitoSEHEMU YA KWANZANi kipindi cha mvua za masika. Upepo mkali, na mvua kubwa iliendelea kunyesha kwa kasi kila kona ya nchi ya Tanzania.Ipo mikoa iliyofurahia mvua hizo kwa kuwa walikua wanaisubiria kwa hamu kwa ajili ya kilimo. Lakini ipo mikoa iliyokua inapata shida kwa uharabifu wa mazingira na mengineyo mengi.Moja ya miko hiyo ni Dar-es-salaam. Watu wanaoishi katika mkoa huo walichukia mvua mfululizo kutokana na sababu mbalimbali. Biashara nyingi…

MY DIARY (33)

Jina: MY DIARY
Mtunzi: __

SEHEMU YA THELATHINI NA TATU
TULIPOISHIA...
Nilikuwa nachanganya staili za kijamaika na hizi za kwetu, sikuacha pia zile za Nigeria hapo nikapata vitu vyangu vya tofauti kabisa. Basi baada ya kujihakikishia kuwa nipofiti kwa mastahili yangu hayo nilisubiri siku ya shindano ifike nikafanye yangu. Siku ya shindano ilifika na mimi nilikuwa miongoni mwa washiriki walioingia tatu bora.

IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI

TUENDELEE...
Basi ilivyofika zamu yangu ya kufanya vitu vyangu nilipanda jukwaani huku nikiwa nimevalia kivazi ambacho kilitosha kabisa kunipa ushindi kwani ukumbi wote ulizizima kwa makelee ya kunishangilia.Nilivyovyaa kwa kweli ilitosha kuwachengua mashabiki ambao wengi walikuwa ni wanaume tena wenye uchu wa mambo hayo ya kukata mauno.Sikutaka kupoteza mda nilianza kazi yangu kwa makeke ili hali nikijua kabisa watu wote waliokuwa wakinitizama walikuwa wanaumia roho kutokana na mvuto wa umbo langu niliokuwa nao.

Nilisikia mijibaba miwili ikiulizana hivi lile wowoo ni la kwake au ni la mchina? Mmoja wao akaropoka “wee kitu original hicho, kwani umemsaahau huyu binti tulishakutana nae kule Arusha mpaka tukambatiza jina la soda kubwa tena ya fanta yaani BAMBUCHA.?” Yeah nimekumbuka alidakia mwanaume wa tatu waliokuwa nao.

Akaongeza basi huyu tusimwite tena BAMBUCHA bali tumpe jina la bia kwani inaonesha thamani yake ni kubwa zaidi. Basi wote kwa pamoja wakacheka.

Wakati nikiendelea kutingisha makalio yangu ambayo kiukweli yalikuwa yakitetemeka kama mawimbi ya bahari, yule aliyetoa hoja akapendekeza jina linalofanana na bia eti kutokana na uzuri niliokuwa nao aliniita HAINKEN WOWOWO.

Ilinibidi nicheke kwa nguvu kitu ambacho kiliwashitua mashabiki wangu waliokuwa wakinifuatilia, hawakujua nilikuwa nikicheka nini wakajua labda nilifurahishwa na ule wimbo wa kanga ndembendembe laki si pesa. Wakati nikiendelea kuzungusha nyonga yangu kwa ufundi wa ajabu niliokuwa nao niliendelea kufuatilia mazunguzo ya wale watu waliokuwa wamekaa meza ya karibu na jukwaa. Niliendelea kuzungusha nyonga na kwa wale ambao ndo ilikuwa ni mara yao ya kwanza kuniona walishangaa sana.

Lakini kwa wale ambao walishaniona kwenye shindano la miss bonge kule Arusha wasingeshangaa sana kwani kile ndo kipaji nilichojaliwa na mwenyezi Mungu. Nilizungusha kisawa sawa huku nikirembua macho yangu kitu ambacho siku zote kilikuwa nikiwaumiza wanaume wenye tamaa. Kwa ufundi wa ajabu nilio kuwa nao niliendelea kufuatilia wimbo niliowekewa huku nikilitegeza sikio langu moja kwenye ile meza iliyokuwa karibu yangu. Wale wanaume waliendelea kunitumbulia macho huku wakiendelea kubishana juu ya jina gani wangenibatiza kulingana na uzuri wangu.

Nilibahatika kumsikia mmoja akimwita muhudumu kwa fujo na kumwambia “inaelekea wewe hujui majukumu yako, mbona bia imeisha na umekaa mbali?

Dada kwa heshima kubwa na kutambua kuwa walikuwa wameanza kulewa alimjibu kwa kumwambia samahani kaka” Sitaki samhani yako niletee bia inayofanana na huyo dada kwenye jukwaa. Yule muhudumu alibaki ameduwaa asijue nini cha kufanya. Akauliza jamani kaka mbona sikuelewi nikuletee kinywaji gani? Kaka kwa ukali akamwambia kinachofanana na huyo dada.

Muhudumu akaenda kaunta na alipokuja alikuja na soda kubwa iliyojazia yaani BAMBUCHA. Watu wote kwenye meza yao walishangaa yaani mtu alikuwa anakunywa bia na sasa ameletewa Bambucha. Ili bidi wapigwe na butwaa, yule jamaa akamuuliza yule muhudumu kwanini umeleta hii soda? Muhudumu kwa kujiamini alisema ‘Ni kwa sababu huyo dada anaitwa BAMBUCHA.Basi watu wote pale mezani waliangua kicheko.

Basi kwa kuwa kila mtu alipewa nyimbo tatu kuonesha maujuzi ya kuzungusha nyonga na kuchezesha makalio, hivyo mimi niliwekewa wimbo wangu wa mwisho. Huku nikibadilisha staili na kucheza ile matata ya kulala chini kisha kuzungusha kama vile upo juu ya mwanaume. Nilimsikia yule mteja akimwambia muhudumu niletee HAINKEN WOWOWO na wakati Yule dada akitafakari Heinken wowowo ni ipi, kwa macho yangu ya wizi nilimwona yule kaka akifungua pochi yake na kutoa hela na kila kwenye noti ya elfu kumi alikuwa akiandika kitu.

Sikujua alikuwa akiaandika nini nitakwambia nikishuka jukwaani. Basi nikaamua kuendelea kufanya yangu na nilikuwa namalizia na ile staili ya mdembwedo.

Hii staili ni mbaya sana kwani unakuwa kama unajizalilisha, hapa wapambe wangu walinimwagia maji kwenye makalio hivyo kuwa ndembendembe. Nilitumia vizuri vidole vyangu kuviingiza sehemu ambazo kwa kweli naogopa kusema. Yule kaka akashindwa kuvumilia akanifuata na kunimwagia zile noti za elfu kumi kumi.

Sikujua alinipa shiling ngapi kwa kuwa haikuwa kazi yangu kuokota hela ila kwa utundu wangu niliivuta moja kwa kutumia vidole vya miguu yangu. Nilifanya hivyo kwa sababu mara nyingine huwa tunazulumiwa na pia nilitaka kujua yule kaka aliandika nini kwenye zile hela.Mda wa mimi kuendelea kukaa jukwaani ulimaliika basi nikashuka chini huku mashabiki wakinipigia mayowe na makelele ya shangwe

Nilikwenda moja kwa moja kwenye chumba cha kubadilishia nguo na wasiriki wengine waliendelea kufanya mambo yao.Baadaae washiriki wote walimalizika na muda wa kutangaza mshindi ulifika. Nakulikuwa hakuna haja ya kupepesa macho mimi nilitangzwa mshindi jambo ambalo lilifanya ukumbi uzizime kwa kuraha. Ikabidi mashabiki waniombe nicheze wimbo mmoja ambao ungewafurahisha nakusindikiza ushindi wangu.Kinyume na walivyotarajia mimi sikuwekewa tena wimbo wa taarabu bali niliwekewa wimbo wa kinaigeria nakuanza kufanya vitu vyangu.Maneno ya wimbo ule ndo huwa unanipa maksi sana “ baby pull over, show me your particular, revese, back, right. Left and front”

Hapo sasa mimi kweli nikawa naonesha vitu vyangu vya mbelee, nyuma kushoto na kulia ili mradi kumtukuza mungu kwa kazi nzuri ya uumbaji.Kweli mungu alinipa kipaji maana staili yangu yauchezaji iliwafanya watu kufungua pochi zao na kuja kunitunza. Nlipata hela nyingi sana ambazo hata mimi mwenyewe sikuzitarajia. Tamasha likaisha kihivyo na kila mtu akaendlelea na ratiba zake.Leah alipewa hela zake zote alizotunzwa pale jukwaani akaendelea na furaha ya yake ya kushangilia ushindi.Kabla sijaondoka nikakumbuka zile noti za kwanza ambazo nilipewa na yule kaka ambaye alinibatiza jina la Heinken wowoo badala ya Bambucha. Kweli kuna watu wana akili huku duniani kwa sababu zile noti ziliandikwa namba za simu.Niliziangalia zile noti nikatabasanmu na kujisemea kweli wanaume wana mbinu nyingi sana duniani.

Basi mara baada ya kuhakikisha kuwa zile hela zangu na cheque niliyopata ipo sehemu salama niliamua kumtafuta yule kaka. Nilichukua simu yangu na kumpigia simu yake iliita mpaka ikakata bila kupokelewa.Nikaamua kumtumia ujumbe mfupi wa maneno “mshindi wa mwanamke nyonga hapa” Yule jamaa mbona alipiga simu mwenyewe na swali la kwanza aliloniuliza ni kuwa nipo wapi.Ilibidi nimjibu kuwa nipo nyumbani.Yule kaka ambaye mimi nilikuwa namjua kabisa kuwa ni star wa bongo movie aliniuliza kuwa eti tunaweza onana usiku huo kwa sababu kesho anaondoka alafu alikuwa na jambo la muhimu sana kuhusu maisha yangu.Yaani kusikia jambo muhimu kuhusu maisha yangu kwa kweli nilichanganyikiwa. Ilibidi nimjibu kinyonge sasa tuataonana wapi usiku huu. Basi Yule mkaka akanambia kuwa wanaelekea club na kama sitojali niungane nao kwa kuwa anaamini kuwa huko tutapata mda wa kuongea zaidi.Kwa kuwa mimi nilitambua ustaa wa kaka yule nikaona hakuna haja ya kulaza damu huwezi jua labda anataka kuniingiza kwenye tasnia ya filamu. Nilimuhadi kuwa nitafika maeneo hayo tuliyokubaliana mda mfupi baadaye.

Kwa kuwa nilikuwa na hela nikaona isiwe tabu ngoja niende zangu home nikaweke hela kisha nivaee nguo za club nikale raha mie mtoto wa watu. Nilichukua tax kwa kiburi ya hela zile za kutunzwa. Uzuri safari hii nilikuwa naishi katikati ya mji.Mimi jamani napenda sana mziki kwa sababu ndo ilikuwa ni starehe yangu ninayoipenda hivyo msinishangae kabisa mimi kukubali kwenda club kirahisi hivyo. Nilijipara kisha nikaondoka zangu na kwenda eneo la tukio na nilivyofika bado sikutaka kutumia hela yangu kulipa kiingilio.

Basi nilimwandikia sms na kumuueleza kuwa nilishafika eneo la tukio.Sikuwa mbali sana na fikra zangu kwa maana baada ya dakika mbili tu mwanaume huyo alitoka na kuja nje mahali ambako nilikuwa nimesimama.Hakutaka kupoteza mda akanilipia kiingilio kisha tukaingia ndani. Tulipitia kaunta na akanambia nichkue kinywaji ninachopenda. Tulikwenda pembeni mafichoni kidogo sehemu ambayo tungeweza kuongea bila kuwakera wengine. Tulikaa sehemu ambayo sauti ya mziki ilikuwa sio kubwa ili tuweze kuongea. Naitwa Mark alianza kwa kujitambulisha staa huyo wa filamu hapa nchini.Na mimi nikamwambia naitwa Leah japo wengine wananifahamu kwa jina la Bambucha.

Hatukuweza kuongea sana kwani kampani ya Mark ilisogea karibu yetu hivyo tukawa wengi na stori zikabadilka na kuanza kupiga storiza club na mziki. Na kwa bahati nzuri wanaume hao wote walikuwa na mademu zao kwa hiyo aliyefurahishwa na mziki aliamka na kwenda kucheza. Na wengine walicheza palepale pembeni ya meza. Mark nae hakujivunga alinipa mkono na kwenda kusasambua. Kama kawida yangu ikija swala la kucheza mziki basi ndo ujue kuwa umenifikisha mahali pake. Sikujivunga kwa kweli nilionesha yale maujuzi yangu na hivyo nikawa kivutio cha watu waliofika eneo hilo. Ilifika wakati watu wote waliacha kucheza na kunitazama mimi nikifanya vitu vyangu. Mambo yaliendelea na Dj uzalendo ulimshinda ikabidi atoe tu zawadi.Sikushangaa kwa sababu haikuwa mara yangu ya kwanza kupewakuponi ya kuingia bure club mara baada ya kutawala stage

Baadaye mda ulienda sana na nilikuwa nimechoka sana hivyo nilimuaga Mark kuwa nahitaji kuondoka na kwenda kupumzika.Cha ajabu Mark alikata kuwa nisondoke na aliniomba tuende kulala nae kwa sababu alikuwa bado hajaniambia kitu ambacho yeye alitaka kuniambia na pia isitoshe yeye kesho anaondoka na kwenda Nairobi kwa ajili ya kazi zao hizo za filamu. Aliniweka njia panda kwa kweli kwa sababu ndo ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kukutana na mwanaume huyo kivipi nitamwamini na kuenda kulala nae.

Nilimueleza ukweli kuwa hiyo ndo siku yetu ya kwanza kukutana sasa ni kwa vipi tunaweza aminiana na kwenda kulala wote. Pamoja na vikwazo vyote hivyo bado Mark alisisitiza kuwa kuna jambo la muhimu anataka kuongea na mimi. Hapo nikakumbuka kuwa zile zana zangu za kazi nilikuwa nazo ni vile vifaaa vya kupimia ukimwi ambavyo huwa navitumia kabla ya kukutana na mwanaume yeyote nisiyemfahamu. Nikaamua kumkubalia huku nikiamini kuwa hiyo ndo kinga yangu pekee iliyobaki kama mwanaume huyo atataka kuzini na mimi usiku huo.

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU IJAYO
68 My Diary Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni