DHAMANA (16)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
Mwandishi: Hassan O Mambosasa
SEHEMU YA KUMI NA SITA
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
"njoo unisaidie kumuweka kitandani mjomba wako" Bi Farida alimuambia yule mtu aliyemuita huku akikisukuma kiti cha matairi kuelekea chumbani kwake, muda huo Shafii alikuwa bado ameuma akiweka maumivu yake ya kuigiza ili azidi kumchota mke wake akili ajue ni kweli ameumia.
KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA CnZ Media APP INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO
SASA TUENDELEE...
"Sawa shangazi nakuja sasa hivi" Sauti ya Jamal ilisikika kisha mlango wa chumba kimojawapo ukafunguka na akatoka kijana aliyefanana sana sura na Hamis kaka yake Bi Farida na shemeji yake Shafii, Jamal alitembea upesi akamfikia shangazi yake akachukua kiti alichokalia Shafii akaanza kukiburuza yeye kukiingiza katika mlango wa chumba kimojawapo ambacho kimejitenga sana na vyumba vingine ndani ya nyumba hiyo, alipoingia ndani alikiburuza kiti hadi mahali kilipo kitanda cha kisasa kilichotengenezwa kwa mtindo wa kipekee na kunakshiwa kwa mapambo mbalimbali. Jamali alipofika hapo alimbeba mjomba wake kwa uangalifu akamlaza kitandani halafu akatoka chumbani kwa mjomba wake upesi kutokana na heshima aliyonayo kwao ambayo haimpasi kukaa humo ndani muda mrefu kama alikuwa tayari amemaliza kile kilichomfanya aitwe.
Bi Farida alichukua dawa za kutuliza maumivu akampatia mumewe pamoja na maji, Shafii alizinywa hizo dawa kisha akajilaza huku akiuma meno vilevile na baada ya muda alijifanya kapitiwa na usingizi ili kutuliza wahka aliyokuwa nao mkewe juu yake kwani wasiwasi ulikuwa mkubwa sana kila akimuangalia anavyouma meno kwa hasira. Bi Farida baada ya kumuona Shafii kalala alimfunika na shuka vizuri halafu akambusu usoni, alitoka chumbani akaelekea sebuleni akamkuta Jamali anaongea na simu ya mezani ambapo alipofika tu mpwa wake huyo alisema, "eeh huyu hapa ongea naye".
Jamal alimkabidhi mkonga wa simu shangazi yake kisha akaenda kukae sebuleni kwenye kochi, Bi Farida alichukua mkonga wa simu akauweka sikioni na kuongea " ndiyo ni mama yake hapa.......hapana hajarudi nyumbani tangu muhula wa masomo ulipoanza.......nyinyi mnasema tulimtuma mtu aje kumfuata sisi hatukutuma ingawa ni kweli kulikuwa na matatizo huku nyumbani.....sawa toa taarifa ya kutoonekana kwake nyumbani wala chuoni".
Baada ya kuongea hayo maneno kwa njia ya simu aliikata simu kisha akaanza kulia kwa sauti ya chini kutokana na taarifa aliyopewa, Jamali aliinuka akaenda kumbembeleza shangazi huku akimuuliza jambo lililomfanya alie.
"Jamal binamu yako hajaonekana chuo tangu siku ile ya msiba wa wajomba zako na huko chuoni kwao walikuja watu wakasema wametumwa na baba Zayina kumfuata arudi kwa ajili ya msiba jambo ambalo siyo la kweli kabisa" Bi Farida alieleza huku akilia kwa uchungu sana.
"Shangazi usilie sasa inabidi wewe ndiyo upange mkakati wa kumtafuta kwani mjomba hali yake ndiyo hiyo unaiona na hii taarifa akipewa itamletea matatizo zaidi, naamini Zayina yupo salama tu na hajadhurika hivyo tuanze kumtafuta haraka iwezekanavyo bila hata kumuhusisha mjomba"Jamal alimuambia shangazi yake.
"Jamali mwanangu mimi jamani, sijui wamemkosea nini mpaka wamafanyie hivyo. Oooh! Yarrabi nisaidie mimi" Bi Farida alizidi kulalamika kwa sauti tofauti na awali.
"Shangazi sauti hiyo mjomba ataamka na asikie iwe mengine nafikiri unajua jinsi anavyompenda sana Zayina, hebu fikiria akiamka utamuweka katika hali gani kama akijua. Inabidi tutoe taatifa kwa wajomba wengine na baba ila yeye tu asiambiwe ili wasaidie katika hili" Jamali aliongea kwa upole tena kwa kusihi hadi Bi Farida akatulia akawa anafuta machozi hadi aliponyamaza.
"Sawa nimekuelewa anko, ngoja nimpikie baba yako na shemeji Hassani ili tuje tujadili hili suala" Bi Farida alimuambia Jamali halafu akanyanyuka akaenda mezani alipoiacha simu yake ya mkononi akawapigia wahusika aliowahitaji katika kujadili hilo suala.
Baada ya nusu saa Hamis na Hasaani walikuwa tayari wameshawasili nyumbani kwa Shafii na kikao cha watu wanne kikawekwa eneo la bustanini na wahusika wa kikao hicho wakawa ni Bi Farida, Hamis, Hassani na Jamali. Kikao kilianza kwa Bi Farida alifungua kikao kwa kueleza kils kitu juu ya taarifa aliyoipata kutoka kwa uongozi wa chuo kikuu cha Dar es salaam kisha akaeleza ushauri alioupata kutoka kwa Jamali wa kuwaita wao ili waweze kulitatua tatizo hilo.
"Umefanya vizuri sana mwanangu kwa kumshauri shangazi juu ya hili suala" Hamis alimpongeza Jamali kisha akaendelea, "dada hili suala kwa jinsi unavyolieleza ni zito sana na linahitaji tufikirie kwa kina haswa maana huyo mtu aliyemfuata Zayina akamwambia mnamuita nyumbani anajua nini anafanya na ametumia taarifa ya msiba huu kuwa ni njia ya kumnasa".
"Shemeji Hamis naungana na wewe katika suala hili itakuwa huyu mtu ni adui namba moja wa kaka sasa inabidi huu msako tutume watu wenyewe wauendeshe kwani tukitumia vyombo vya dola itakuwa tunaharibu tu maana hatuwezi jua huyu mtu ana nguvu gani katika serikali. Kumbuka Zayina kusoma chuo kile tulifanya siri kwa wanafamilia tu kwani tunatambua mtu maarufu ana maadui sana ndiyo maana tukawaambia watu wengine kwamba Zayina anasoma Ulaya ili tuwapoteze njia ya kumtafuta, sasa tujiulize huyu mtu ana ni nani na ana lengo gani mpaka amejua Zayina alipo na akafanya hilo alilolifanya" Hassani naye aliongea kwa mara ya kwanza katika kikao hicho.
"Shemeji tayari mimi nishawaambia uongozi wa chuo kikuu cha Dar es salaam watoe taarifa juu ya suala hilo hivyo tayari lipo kwenye vyombo vya dola, sasa tufanyeje?" Bi Farida aliongea
"Aaaah! Shemeji umekosea sana kufanya hivyo huoni huyo aliyemshikilia Zayina atazidi kuwa makini ili tusimjue" Hassani alimlaumu shemeji yake kwa kuwaambia uongozi wa chuo kutoa taarifa.
"Dada hapo umekosea sana kufanya hivyo kwani alichokuwa anaongea Shemeji hapa ni sahihi kabisa kukifanya katika suala hili kwani haitakiwi kuwashirikisha wanausalama inatakiwa tutumie pesa yetu mtoto apatikane" Hamis naye alimlaumu dada yake.
"Jamani nilikuwa nimechanganyikiwa haswa kutokana na kupokea taarifa hiyi, sasa tutafanyaje?" Bi Farida aliongea akionekana kutambua alichokifanya sicho katika kutoa taarifa ya kuwaambia uongozi wa chuo.
"Hukutakiwa kufanya hivyo dada" Hamis alimlaumu dada yake.
"Baba na mjomba hili suala limeshatokea na haliwezi kuwa halijatokea yaani tukubali Shangazi alikosea kuwaambia uongozi wa chuo kuto taarifa polisi lakini tusimlaumu kwa kufanya hivyo maana huo muda wa kulaumiana hamna, cha msingi ni kukaa na kujadili hilo tufanye nini ili Zayina apatikane jamani" Jamali kwa mara ya kwanza aliongea baada ya kuwasikiliza wakubaa zake, maneno yake yalionekana kuwaingia mjomba wake na baba yake hadi wakakaa kimya kwa muda wakijifikiria halafu wakatazamana na wakapeana ishara ambayo hakuna yoyote aliyeiona.
"Sawa mwanangu nimekusikia tuachienu hili suala tulishughulikie naamini Zayina atapatikana ndani ya muda mfupi tu" Hamis huku baada ya kushusha pumzi, Hassan naye alikubaliana na maneno naye.
"nafikiri hili suala lipo kwetu na tutalifanyia kazi sasa naomba Kaka asijue juu ya hili" Hassani naye aliongea kisha akasimama pamoja na Hamis.
"Shemeji yupo wapi tukamjulie hali kidogo kwani kuja huku bila kumjulia hali si jambo jema" Hamis aliuliza
"Yupo chumbani kapumzika baada ya mgongo kushtuka, nafikiri atakuwa kashaamka twendeni mkamuone" Bi Farida aliwaambia huku akinyanyuka kwenye akaelekea ndani, Hamis na Hassani walikuwa nyuma wakimfuata.
Wote kwa pamoja walielekea chumbani kwa Shafii ambapo walimkuta akiwa tayari ameamka.
"Karibuni jamani" Shafii aliwakaribisha
"Asante Chumbio" Hamis aliitikia ukaribisho huku akikumbushia jina la utani la Shafii, Hassani na Bi Farida wacheke.
"hilo jina husahau tu Bonoeza" Shafii naye aliongea huku akitia jina la utani la Hamisi nakupelekea wote wacheke humo ndani.C
"Bonoeza siku hizi umelizoea si ulikuwa ukiitwa unarusha mawe kaka" Bi Farida naye aliongea huku akicheka na kupelekea wote humo ndani wacheke sana.
"Ila hilo jina umenikumbusha mbali sana niliwahi kumpiga mwenzangu tukichunga mbuzi kisa hilo jina, ila toka naingia kwenye ujana hadi utuzima naona kawaida tu" Hamis aliongea huku akicheka.
"Haya jamani ngoja niwaache na soga lenu la kiutuzima" Bi Farida aliongea kisha akatoka humo chumbani akiwaacha Kaka yake, mume wake na shemeji yake.
Alipofunga mlango wa chumbani mwake mada ikabadilika papo hapo na ikaongelewa mada inayowahusu hao wanaume watatu waliokuwa na ukaribu tangu utotoni, mambo yao mengi ya siri walikuwa wakiambizana na hata mengine mazito walishirikiana.
" kajua Zayina anashikiliwa na mbaya wetu ambaye bado hatujamtambua" Hamis alimuambia Shafii
"Natambua sana kama anajua hilo kwani wakati anaongea na simu sikuwa nimelala kama anavyofikiri na hata alipolia kwa sauti na kulalamika nikawa namsikia" Shafii aliwaambia.
"Hiii ni balaaa haswa inabidi tumtafute mtaalamu mwenye uwezo wa kudhibiti majini maana anayefanya haya si mwanadamu wa kawaida" Hassani aliongea.
"Hilo ndiyo la kufanya inabidi atafutwe mtaalam ila asiwe mzee Mahmud maana yule mzee atatuvua nguo tuaibike kwanza halafu ndiyo atusaidie maana tiba zake hufanya kazi ukiongea ukweli tu, sasa sisi hatuko tayari kuvuliwa nguo" Shafii aliongea
"Kweli kabisa bwana Shemeji ni bora kufa na matatizo yetu shingoni kuliko kukubali kuvuliwa nguo" Hamis alidakia baada tu ya Shafii kumaliza kauli yake.
"Jamani hili suala tupiganeni hadi kufa maana wataalamu ni wengi hapa Tanga tena leo hii nimepata taarifa kuna mtaalam mwingine anaitwa Mafindo yupo Pangani nasikia huyo ni kiboko ninahisi ndiyo itakuwa mwisho wa matatizo" Hassani aliongea
"Enhee Hassani umenena haswa naona mkitoka hapa muanze huko au mnasemaje jamani na ningekuwa mzima ningeungana nanyi" Shafii aliafikiana na Hassani.
"Sawa naona tusipoteze muda bali twende huko ili mambo yasiwe mabaya" Hamis alisema kisha akanyanyuka akampa mkono Shafii na Hassani naye akafanya hivyo hivyo.
"Kila la heri jamani" Shafii aliwaambia kuwatakia heri katika mpango huo wanaoenda kuufanya, Hamis na Hassani waliondoka upesi ili wawahi kurudi kwani Pangani kulikuwa mbali na muda ulikuwa umeenda sana.
Hali ya hewa ilikuwa ni tulivu sana na mawingu ng'amba yalikuwa yamepamba anga zima na kulifanya jua lisionekane kabisa na kuweka hali ya kivuli na kuwafanya wakazi wa jiji la Tanga kuwa na ahueni ya joto haswa kwa wale wanaotembea kwa miguu pembeni mwa barabara. Hamis na Hassani walikuwa wapo ndani ya gari binafsi wakielekea Pangani na muda huo tayari walikuwa wanaimaliza barabata ya Taifa wakiingia katika mzunguko wa magari unaounganisha barabara nne zikiwemo barabara ya Taifa, barabara ya Pangani, barabara ya jamhuri na barabara iendayo kukutana na barabara ya Chuda.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni