Notifications
  • MY DIARY (12)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA MBILITULIPOISHIA...Niliamua kufanya ziara ili nijue pakoje na mwisho wa siku niliamini kuwa kutokana na umaarufu wa marehemu baba yangu isingekuwa kazi sana kulipata shamba lake..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi nilitembea kijiji hadi kijiji huku nikijaribu kuuliza kwa wenye viti wa mtaa kama walikuwa wakimjua marehemu Bura. Kwa kweli kazi ilikuwa ngumu sikuweza kuvimaliza vijiji…
  • MY DIARY (11)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA MOJATULIPOISHIA...Wakati akiongea maneno hayo mara mtarimbo ukaanza kusimama nikajisemeha nimeshakosea nilitakiwa niondoke nilivyoona kimelele tu, nikajua hapo lazima atanitafuuna bila huruma. Basi akaingia bafuni akachukua sabuni akajipaka ili kujisisimua ngoma isimame vizuri.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Yaaani nilichanganyikiwa na huko bafuni nilisikia maneno ambayo yalinichekesha…
  • MY DIARY (10)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMITULIPOISHIA...Nikamwambia Joyce ndo maana mimi nakupendaga. Nikamwambia “nitakuapa feedback ngoja nimpigie asije akaja na makufuli yake leo hii. Nikampigia baba mwenye nyumba eti kwa kujiamini kabisa akapokea nakusema “ Halow mrembo” Nikamwambia Yes mpenzi kitu ambacho kilimfurahisha sana..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Kuokoa hela ya vocha nikamwambia nimekubali ombi lako alafu nikakata…
  • MY DIARY (9)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TISATULIPOISHIA...Basi Dj wangu aliendelea na mautundu yake akaniwekea mambo ya pwani na hapo ndipo uvumilivu ulipomshinda akaja kunibambia na mimi sikuona haja ya kumbania kwa kuwa ni mali zake mwenyewe. Nilizungusha nyonga na kiuno mpaka nikachoka nikajitupa kitandani ili nipumzike. Nafsi yake ilikuwa imeridhika kwani hakutka tena penzi bali alichukua lap top yake na kuanza kunionesha picha na vitu vingine ambavyo vilinipa raha.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA…
  • MY DIARY (8)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA NANETULIPOISHIA...Sijui hata haya maneno yalitoka wapi, fahamu zilinitoka na Ticha aliamua kuninyanyasa maana nilishajikojolea zaidi ya mara tano. Basi na yeye kwa kutafuta mbwembwe alianza yale mambo yao ya katerero, siunajua tena mwalimu John alitokea pande za Bukoba.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alinichezea sana na baadaye nilishangaa kukuta jamaa ameshaingiza kunako. Sikujielewa kwa…
  • MY DIARY (7)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA SABATULIPOISHIA...Kwaito zilivyonoga uzalendo ulinishinda nikajikuta na mimi nashuka ngazi kuelekea chini sehemu ya kuchezea.Nilizijua kwani shuleni tulikuwa tunazicheza sana hasa kwenye yale madisco yetu ya mwisho wa mwezi.John wangu alibaki juuu akiniangalia jinsi nilivyokuwa nikicheza vizuri.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Yeye alishindwa kushuka akiofika kile kitu kukaliwa na watu…
  • MY DIARY (6)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA SITATULIPOISHIA...Akanambia kuwa wamemwambia wapo East Africa Pub na tayari wamaeshaagiza mkuu wa mbuzi. Mmmmhhhh kusikia mguu wa mbuzi mate yalinijaa mdomoni. Basi kwa harakaharaka nikamwambia naomba niende niende nyumbani nikachukue viwalo vya club kisha nitawakuta hapo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alinambia mbona hizo nguo ulizofaa zipo poa tu wewe twende hivyo bhana si upo na…
  • MY DIARY (5)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TANOTULIPOISHIA...Akanisimamisha na kuanza kuiuliza maswali mengi yasiyo na maana huko akionekana kutojiamini. “samahani dada, sijui unaelekea wapi”? Nikamjibu dukani. Akavuta pumzi ndefu na kuniambia ok, nisaidie namba zako za simu. Nikamwangalia juu na chini nikwambaia nimezisahau na simu nimeiacha ndani nikirudi ndani nitakuletea..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Akaishiwa pozi akanambia,…
  • MY DIARY (4)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA NNETULIPOISHIA...Uchambuzi huu ulinigusa sana kwani hata mimi nilijihisi kuwa sikuwa na utando huo yaani bikira japo nilikuwa sijawahi kujamiana na mwanaume wa aina yeyote zaidi ya ile michezo ya utotoni ya kula mbakishie baba au ile ya kibabababa na kimamamama. Alianza kunishika mapajani na kunifanya nianze kusisimuka ajabu kwani japo alikuwa ni mwanaume mikono yake likuwa ni milani sana kama ya mtoto wa kike.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media…
  • MY DIARY (3)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TATUTULIPOISHIA...Nazani sasa unanielewa ninaposema nilikuwa sina ndugu kwani baba yangu hakuwa na ndugu yeyeote zaidi ya marafiki ambao na wao kwa sasa ndio hao wameshagawana mali zote. Nimebaki mimi na dunia yangu hivyo basi nilimwomba rafiki yangu wa kufa na kuzikana kwa jina Joyce anisaidie kunisitiri nyumbani kwao.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Likizo ilipoisha tulirusi shuleni na…

DHAMANA (21)

Jina: DHAMANA

SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA
TULIPOISHIA...
Alifika hadi sehemu iliyokuwa na matanki ya maji ambapo kama maji yakijaa na kumwagika basi hujulikana wa eneo hilo kulowana hasa bustani ya maua ambayo imezunguka eneo lenye matanki ya maji, cha ajabu eneo hili lilikuwa kavu kabisa hakuna dalili ya kumwagika maji.

KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA CnZ Media APP INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
Akiwa anashangaa hali hiyo alisikia sauti ya mjomba wake akipiga yowe la maumivu huko ndani na ikamlazimu kukimbia kuelekea chumbani kwa mjomba wake (muda huo Shafii anapiga yowe la maumivu ndiyo muda ambao Bi Farida alizirai kule kwemye himaya ya majini baada ya kutapika vitu visivyoeleweka).

Jamali alipofika chumbani kwa mjomba wake alimkuta akiwa ameanguka chini akiwa amekaukiwa na sauti, alimuinua na kumuweka kitandani ambapo Shafii alionesha ishara ya kutaka maji kwenye bilauri yaliyppo humo chumbani mwake mezani na ikamlazimu Jamali amletee maji upesi. Shafii alikunywa maji yote kwenye bilauri ndiyo akaweka kuongea na neno la kwanza kulitamka ni jina la mkewe, alipoona hamuoni mkewe alimuuliza Jamali mahali alipo shangazi yake. Jamali alimueleza kila kitu juu ya kutoonekana kwa shangazi na maajabu aliyoyaona, hali hiyo ilimshtua sana Shafii akabaki amechanganyikiwa.

"mpigie baba yako muambie aje hapa sasa hivi" Shafii alimuambia Jamali huku akimuonesha simu ilipo, Jamali alienda kupiga namba ya baba yake lakini haikuwa inapatikana na alijaribu zaidi ya mara nne lakini jibu ni lilelile.

"Haipatikani"Alimuambia mjomba wake

"He...hebu mpigie na Hassan usipompata piga nyumbani kwenu umuulizie baba yako" Shafii aliongea akionekana amepagawa kabisa, Jamali alupiga namba ya Hassani ila matokeo yalikuwa yaleyale na ikamlazimu apige nyumbani kwao amuulizie baba yake.

"Anko nyumbani wanasema hajarudi tangu alipoondoka na anko Hassani"Jamali alimuambia Shafii huku akionekana kuchanganywa na haliya mjomba wake.

"Etii?!" Shafii aliuliza kwa nguvu halafu akazirai papo hapo kutokana na taarifa anazoambiwa, hali hiyo ilimchanganya Jamali na ikambidi awaamshe wafanyakazi wote wa nyumba hiyo na jitihada za kumuwahisha hospitali zikafanywa mara moja.

****

Shafii alikuja kuzinduka siku iliyofuata akajikuta akiwa yupo hospitalini amelazwa akiwa ametundikiwa dripu ambayo ilikuwa inakaribia kuisha, alipoangaza pembeni aliwakuta Mzee Buruhan, Mzee Mahmud na Mama Jamali mke wa Hamis wakiwa wamezunguka kitanda chake.

"Faridaaa!" Shafii aliita jina la mke wake kwa nguvu huku akijaribu kuinuka kitandani

"Shafii hebu tulia kwanza utasababisha matatizo mengine tu" Mzee Buruhan alimuambia huku akimzuia asifanye fujo.

"Mama Zayina, Zayina mpo wapi?" Shafii alipiga kelele zaidi na ikabidi daktari aitwe mara moja ili kumtuliza, Mzee Buruhan na Mzee Mahmuf walimshikilia Shafii hadi daktari alipokuja akamchoma sindano ya usingizi ndiyo ikawa ahueni.

Baada ya Shafii kulala mzee Buruhan na mzee Mahmud walitoka pamoja na mke wa Hamis wakaenda kuka kwenye madawati ya kusubiria wagonjwa, baada ya muda mke wa Hamis aliondoka kwenda kufuata chakula kwa ajili ya mgonjwa akawaacha wazee hao peke yako.

"Kama nilivyokuambia mzee mwenzangu kuhusu huyu mwanao, awe mkweli ujue tatizo alilonalo ndiyo nitakubali kumsaidia" Mzee Mahmud aliongea.

"Mzee mwenzangu tatizo kila kukicha una misemo ambayo imejaa vitendawili vitupu hebu niweke wazi walau kidogo nipate fununu ya jambo linalomsumbua mwanangu" Mzee Buruhan alimlalamikia rafiki yake kutokana na kauli zake zilizo jaa mafumbo.

"mzee mwenzangu hiyo kinyume na utaratibu wa taaluma yangu siwezi kusema hata kama nalitambua tatizo hili, huwa sina tabia ya kukuficha kitu ila kwa hili wacha nikuambie ukweli tu nitakuwa nimekiuka masharti ya utalaamu wangu wa uganga ikiwa nitalisema suala hili pasipo muhusika mwenyewe kufungua kinywa chake na kuliongelea. Utanisamehe kwa hilo" Mzee Mahmud aliongea huku akimshika bega mzee Buruhan ambaye alionekana kuwa njia panda kutokana na matatizo yaliyomkumba mwanae

"mzee mwenzangu hakuna hata njia nyingine ya kunisaidia niweze pata fununu kidogo ya hili suala?" Mzee Buruhan aliuliza huku akiwa ameinamisha uso wake chini akionekana amekata tamaa kabisa ya suala hilo.

"Siku zote mwanamke atakaye mtoto lazima akubali kuvua nguo ya ndani ili alichokificha kionekane na hawezi kupata mtoto ikiwa atakataa kuivua hiyo nguo. Ndiyo hivyo hivyo mwanao akubali alilolificha moyoni mwake lifumbuke la si hivyo hataweza kupata msaada katika hilo, cha kukusaidia akiamka muambie umebaki peke yako ukitaka usipoteze vyote awe muwazi kwangu na kwako. Naenda msalani mara moja mzee mwenzangu" Mzee Mahmud aliongea kisha akajiinua kivivu  kwenye dawati la kusubiri wagonjwa akawa anaelekea chooni, mzee Buruhan alimtazama tu akiwa anatamani sana ajue jambo lililopo ndani ya kichwa chake lakini hakuwa na uwezo wa kufanya hivyo.

Mzee Mahmud  aliipopotea katika upeo wa macho yake aliinua kichwa juu akiweka ishara ya kuomba dua halafu akatikisa kichwa kuonesha anasikitishwa, hakuwa na jambo jingine alilomuomba Mungu zaidi ya kumshtakia tu  juu ya balaa lililomkuta mwanae na kumfanya awe na matatizo tu katika mwaka huo ambapo miaka mingine yote aliishi kwa amani na furaha pamoja na familia yake lakini sasa furaha hiyo imetoweka  katika maisha yake. Laiti angelijua kwamba alikuwa anashtaki mtuhumiwa kuwa ameonewa wala asingelifanya hivyo lakini kwakuwa hakujaliwa uwezo wa kulibaini kwani alikuwa ni mwanadamu wa kawaida tu, hakutambua kama jereha la mwanae ni  la kujitakia hivyo halihitaji pole hata kidogo.

Mzee Mahmud alipofika kwenye mlango wa msalani baada ya kuondoka pale kwenye dawati alihisi hali isiyokuwa ya kawaida katika mwili wake lakini aliipuzia na kuingia humo msalani, alipoingia ndani alipitiliza sehemu za kujisaidia haja ndogo akawa anaelekea sehemu maalum ya yenye vyoo ndani ambayo hutumiwa na wale wanaohitaji kumaliza haja zao kwa siri tu. Alipofika hilo eneo  alifuata mlango wa moja wa vyoo akashika kitasa ili aufungue lakini alisita baada ya  kusikia upepo mzito ukivuma kwa ghafla ambao ulitaka hata kuupeperusha msuli aliojifunga kiunoni lakini aliuzuia, upepo huo ulipotulia Mzee Mahmud alionekana kukerwa nao kwa kitendo cha kutaka kumuadhiri ambapo aligeuka nyuma akionekana kuwa na hasira za waziwazi juui ya tukio hilo.

"Adabu gani hizo ewe mwanajini wataka kuniadhiri kwa hizo nguvu zako ulizojaliwa?" Mzee Buruhan alilalamika baada ya kumuona yule aliyetaka kumuadhiri kwa kutaka kuupeperusha msuli aliojifunga kiunoni alikuwa yupo mbele yake baada ya kugeuka nyuma, alikutana uso kwa uso na Zalabain akiwa amefumbata mikono kifuani mwake.

"Samahani mzee wangu kwa hilo" Zalabain aliomba radhi.

"sema una shida gani" Mzee Buruhan aliongea huku akiuweka msuli aliojifunga kiunoni vizuri.

"nimekuja kukuambia tu mimi ndiye ninayemtesa Shafii na huwezi kuharibu kazi yangu kwa kujaribu kumsaidia" Zalabain aliongea kwa msisitizo.

"Ndiyo nimeshakutambua tangu unajitokeza pia sipo kwa ajili ya kumsaidia dhalim kama yule bali nipo kwa ajili ya kumsaidia Buruhan ili asiondokewe na nguzo zake zote, kiufupi ni hivi nazuia usimuue yule mziwanda wake asiye na hatia" Mzee Mahmud alimuambia huku akijiamini halafu akameza mate kidogo kisha akaendelea, "Shafii ni haki yake kwa alichokifanya ila Ally hana hatia yoyote na usimuingize katika orodha hiyo, pia ningependa mumponyeshe sikio lske na taya lake ambayo mumjeruhi kutokana na kujaribu kuleta kile kitakachoyafanya majini ya marehemu Hamis yafanye kazi. Ukumbuke pia  yeye anachukia ulilofanyiwa ila mali yako anayoimiliki Shafii ndiyo inamfanya ashindwe kufanya jambo lolote, usihukumu yule asiye na hatia kama ni ufalme utapewa pasipo yeye kupoteza uhai wake".

"unasema nini wewe?" Zalabain alimuuliza Mzee Mahmud

"kama ulivyosikia ewe mwana wa jini, ukumbuke mimi nilikataa kutengeneza uchawi kama uliomtapisha mama yako jana kwasababu najua siyo haki kufanya hivyo, pia niligoma kufanya dawa ya kumuua baba yako ili mama yako awe chini ya mwingine kwasababu najua haikuwa haki. Pia utambue nakuambia usimuue Ally kwasababu najua utakuwa hutendi haki ewe mwanajini kamuuulize ibin Zultash atakueleza, mwisho kabisa nakuambia hivi upotee sasa hivi kuna mtu anaingia humu msalani sasa hivi asije akaniona naongea peke yangu kama kichaa wakati nina akili  zangu timamu"

Mzee Buruhan aliongea kisha akageuka nyuma akaingia chooni bila kujali kama Zalabain ameondoka au yupo, baada ya kumaliza haja zake  alitoka hakumkuta Zalabain na akarudi kule alipokuwa yupo awali. Alimkuta mzee Buruhan yupo na Ally wakiongea na iilonekana Ally alikuwa kapona kabisa tatizo la kuvunjika taya na sikio kwani hakuwa mwenye kuweza kuzungumza wala kusikia, lakini hapo alikuwa akizungumza na kusikia vizuri kabisa.

Mzee Mahmud alimuonesha ishara ya kumsalimia Ally kama ilivyokuwa akifanyiwa kwa kutoweza kusikia vizuri lakini.

"Mzee mwenzangu anaongea huyu na kusikia sasa hivi usimsabahi kama vile unamsabahi bubu" Mzee Buruhan alimuambia rafiki yake.

"Yapaswa  tumshukuru Mungu basi mzee wangu maana huu muujiza tosha" Mzee Mahmud aliongea akionekana kufurahishwa na suala hilo.

"Alhamdililah" Ally na baba yake waliitikia kwa pamoja.

Mzee Mahmud alibaki kutabasamu tu kila alipomuangalia Ally kwa kufurahishwa na usikivu alionao Zalabain baada ya kufanya kile alichomuambia, tabasamu lake lilifanya Mzee Buruhan na Ally nao watabasamu  wakijua kafurahishwa na hali ya Ally kutengemaa.

"Ally hebu sogea karibu" Mzee Mahmud alimuambia Ally  huku akimtazama kwa umakini, Ally alimsogelea Mzee Mahmud pasipo kujua ni kipi alichokuwa anataka kufanyiwa kwani alimzoea sana mzee Mahmud na alimchukulia kama baba yake tu. Alipomsogelea Mzee Mahmud aliambiwa achuchumae mbele yake naye akatii amri kama alivyoambiwa, mzee Mahmud alimshika kichwani na akamtamka maneno yasiyoeleweka na kusababisha Ally ashtuke halafu aangalie mazingira ya hapo yalivyo halafu akaenda kukaa kwenye dawati pembeni ya baba yake alipokaa awali.

"Baba hivi hapa tupo kwa ajili gani?" Ally aliuliza tu baada ya kukaa pembeni ya baba yake akionekana kutotambua yupo hapo kwa ajili gani.

"Kha! We Ally maswali gani hayo hutambui kama tupo hapa kumuangalia kaka yako kalazwa tangu jana" Mzee Buruhan alimuambia Ally akionekana kutoelewa kitu alichofanyiwa na  mzee Mahmud hadi akasahau  yupo pale kwa lengo gani wakati alipoingia tu aliulizia hali ya kaka yake.

"Khaa! Kumbe tupo hapa kwa ajili ya kumuangalia firauni huyo, sina muda huo muache afe  maana huyo ni zaidi ya shetani" Ally aliongea maneno ambayo yalizidi kumshangaza sana Mzee Buruhan na akajikuta  akimtazama  mzee Mahmud akionekana kutoelewa kafanya nini, Ally alinyanyuka ili aondoke lakini mzee Mahmud alimuita akamuomba aketi akakaa chini.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
58 Dhamana Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni