Notifications
  • MY DIARY (32)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA MBILITULIPOISHIA...Lakini kuchepuka kwangu na kuingia mgombani haikumaanisha kuwa sheria ingeniacha hivi hivi.Ilifika mahali ikabidi nizime gari na kutulia tulii kusikilizia nini kitafuata.Tayari nilikuwa nimezungukwa na mapolisi ambao walikuwa wakinifuatilia kwa kutumia pikipiki.Kwa bahati nzuri dereva wa lile gari na yeye alishafika hapo na alishawaambia polisi kuwa mimi naugua ukichaa na nilifufuka kutoka mochwari.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA…
  • MY DIARY (31)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA MOJATULIPOISHIA...“marehemu pia alinieleza kuwa ana miliki duka la vitu vya urembo wa kike ambalo pia Leah analisimamia ila hilo apewe mdogo wake Marry ambaye yupo hapa. Mama mdogo huyo mara baada ya kuyasema hayo alikaa zake chini. Baba mdogo ambaye hakurizika na maelezo hayo alisimama na kusema “kwa hiyo kama marehemu alijua kuwa atakufa hivi karibuni kwani nini hakufuata taratibu za kisheria za kuandika wosia na kurithisha mali.IKIWA UNASOMA…
  • MY DIARY (30)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINITULIPOISHIA...Baada ya hapo Nnilimwomba mama mdogo ajikaze na kuwatarifu ndugu wengine habari hizo za msiba.Tulisaidiana hivyo hivyo maana sio siri kila mmoja alikuwa na uchungu sana kutokana na mazingira ya kifo hicho. Habari zilizidi kusambaa kwa kasi na majirani walianza kukusanyika hapo kwa mama mdogo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Msiba ni msiba tu na ukitaka kujua binadamu…
  • MY DIARY (29)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TISATULIPOISHIA...Hapo sasa nikazidi kuchanganyikiwa ikabidi nimuulize mama huyo alikuwa akifanyia shughuli zake za kujipatia kipato sehemu gani.? Yule dada akanambia kuwa anafanyia soko la ndizi huko Korongoni. Sikuwa na jinsi nilimuomba anipeleke lakini na yeye alisita sita kwa madai kuwa alikuwa na kazi nyingi za kufanya na bado anatakiwa ampeleke mtoto shule.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (28)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NANETULIPOISHIA...Sisi tumesomea mambo haya bhana waliendela kuzungumza wale walinzi huku wakishuka ngazi kwa polepole. Hapo na mimi nikawa nimejifunza kitu kuwa kumbe unaweza kuingia na mtu guest akakuzuru kisha akaondoka zake.Sasa sijui kwenye zile guest zetu za uswahilini kama wanalijua hili.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi nilala japo usingizi ulikuwa hautaki kuja kwa…
  • MY DIARY (27)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SABATULIPOISHIA...Alinamba eti hayo ya mimi kuolewa tuyaeke pembeni na kwa nini siku hiyo nisilale Moshi tukumbushie enzi zetu. Mwalimu John aliendelea kusema kuwa amenimiss sana na anomba nisahu yaliyopita na turudie yale maisha yetu ya zamani.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijifanya simwelewi lakini ukweli ni kwamba nyota ya mwanaume huyu ilikuwa ni kali sana zaidi yangu na…
  • MY DIARY (26)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SITATULIPOISHIA...Joyce alinambia yeye haendi kujipanga foleni kama makahaba wengine hivyo yeye hufanya biashara hiyo kitaalamu zaidi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alisistiza pia kuwa eti huwa anatumia kinga kuwakinga wengine. Wakati mwingine alinambia acha awaambukize kwa sababu wanaume wangekuwa na akili basi wasingeenda kununua mwanamke. Anasema kuwa laiti biashara hiyo…
  • MY DIARY (25)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TANOTULIPOISHIA...Sikuisha hapo pia nilimpongeza kwa kunijali na kunipenda na kuhakisha kuwa siingii kwenye majanga kama yake mara baada ya kutoka jela. Siku hiyo nilimuelewa sana Joyce na nilikuwa tayari kumsapoti kwa lolote ili mradi tu atimize athma yake hiyo ya kuzaa. Tuliongea mengi sana na baadaye alinionesha picha ya mtu ambaye alitaka kuzaa naye.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (24)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NNETULIPOISHIA...Kwa kweli siku hiyo niliwaza sana na kutafakri vitu vingi. Wale wanachuo wenzangu wamenambia kuwa Msouth alikuwa kwa kimada mwingine na japo stori haikumalizikia ila ukweli ni kwamba alifumaniwa na kupigwa vibaya na huenda walimtupa mahali na ndio maana chanzo cha kifo chake hakieleweki.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijaribu kuijikontrol ili nisiwaze kitu…
  • MY DIARY (23)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TATUTULIPOISHIA...Alinisihi sana nisitoe niilee na yeye atatoa huduma zote lakini tuendelee kufanya siri ili tusije tukahatarisha ndoa yake na kusababisha familia yake kuyumba. Kwa kweli sikuweza maana ilikuwa ni kujipa tabu mimi na huyo mtoto atakayezaliwa. Bora ataa ingekuwa ni mimba ya ule mwalimu ambaye hajaoa.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilitamani nimchomekee hiyo mimba…

Nyumba ya Wachawi (5)

Mtunzi: Denis Benard

SEHEMU YA TANO
TULIPOISHIA...
‘’Peke yangu?mbona Faluu amekuja huku muda mrefu sana,maana muda Fulani ametoka sokoni akiwa analalamika hajisikii vizuri,mimi nikamwambia aje apumzike,kwani wewe hujamuona?’’ Elly aliongea huku akiwa na amepagawa.

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
Kutokana na majibu yale ya Elly hata mama yalimshtua sana..

‘’Hapana sijamuona huku nyumbani’’ mama alijibu na baada ya Elly kusikia hivyo alikimbia na kwenda kumuona ndani kwao kama hata mkuta.

Alipofika ndani,alijikuta nguvu zikimuisha maana alichokiona hakufikiria kama atakutana nacho..

‘’Mama….mama..mama’’aliita Elly

‘’Nini mwanangu??’’alijibu mama

‘’Njoo uone,Faluu ameondoka,maana hata nguo zake hazipo,sasa atakua ameenda wapi?’’ Elly aliongea

‘’Mmmh sidhani’’ mama alijibu.Elly alikua na wakati mgumu sana,alijitahidi sana kutoka huku na kule kuuliza kama watu watakua wamemuona,lakini hakufanikisha.Lakini baadaye baada ya kurudi huku akili yake ikiwa imetulia aliiona karatasi ikiwa imeanguka chini,Karatasi ile ilimshtua na hivyo akaamua kuikota ili ajue ina nini.Alipoishika alikutana na maneno haya…

‘’Rafiki yangu najua utakua na wakati mgumu baada ya kusoma haya kama mimi nilivyo na wakati huo,Lakini sasa sina jinsi maana inabidi yafanyike ili maisha yaendelee,Rafiki yako nimeondoka naomba usiwe na wasiwasi kwa maana niko salama,naamini siku moja tutaonana.MAISHA MEMA  Wako Faluu’’

Maneno yale yalimuumiza na kumfanya apige kelele mpaka mama alisikia na kuja haraka ili ajue kulikoni..,lakini mama alipofika Elly alimpa ile karatasi ilia some mwenyewe.Maneno yale yalimsikitisha sana na aliona namna mwanaye alivyokua akiumia..

‘’Mwanangu najua namna unavyoumia,lakini tambua kitu kimoja tu;Milima haikutani,ila binadamu tunakutana,usivunjike moyo sawa’’aliongea mama na baadaye aliondoka kwenda kuendelea na shughuli nyingine.

Wakati Faluu akiwa anatembea huku alikua na mawazo ambayo yaliambatana na huzuni ghafla aliisikia sauti ya mtu akicheka na alipogeuka alikutana uso kwa uso na mjomba wake.

‘’Mpwa wangu karibu sana’’aliongea mjomba huku akiwa amejaa tabasamu zito katika uso wake.

‘’Asante sana mjomba wangu,lakini umejuaje kama mimi nakuja? Au huu ulikua mpango wako?? Na kwanini haujakuja katika mazishi ya mama?’’ Faluu alijikuta akiuliza maswali mengi sana na mfululizo.

‘’Aaah, acha wasiwasi  mjomba nilijua tu nan i maagizo aliyoniachia mama yako,twende nyumbani ukapumzike’’aliongea mjomba.

‘’Sasa hadi siku ya leo umejua kama mimi nakuja! Unanipa wasiwasi mjomba wangu’’aliongea Faluu.

Wakati wakiwa wanajibizana Faluu na mjomba wake huku wakiwa wanatembea,Faluu alikua akijaribu kuchunguza pembezoni mwa njia,ghafla aliona kama kuna watu wamekaa pembezoni mwa njia hiyo wakiwa wamejificha na mbaya zaidi alimfananisha mtu mmoja aliyekua miongoni mwa watu waliomkamata siku ile,kitu ambacho kilimshtua sana na akajikuta akishindwa kujizuia na mwishowe ilibidi amuulize mjomba..

‘’Mjomba mbona kama naona kuna watu wamejificha pembezoni mwa njia hii?? Ni wakina nani?’’ Faluu aliuliza.

Swali lile lilimfanya mjomba ashtuke saana na akajikuta akishindwa kujibu na badala yake alio

‘’Aaah!...aah.. mimi sijui,….mimi sijaja nao,kwanza wako wapi?’’aliongea mjomba.

Majibu ya kubabaisha ya mjomba yalimfanya Faluu kuwa na wasiwasi na kua makini sana wakati mjomba anaongea,kutokana na wasiwasi wa mjomba alijikuta akipiga kipenga na bila kupoteza muda walitokea watu wengi na waajabu katika eneo

‘’Mjomba hii nayo nini?’’aliuliza Faluu,

Mjomba aliishia kumtazama tu na bila kupoteza muda walipotea ghafla katika eneo lile

Baada ya kupotea katika eneo lile,walijikuta wakitokea nyumbani kwa mjoma wake. Faluu alijikuta akijishangaa tu baada ya kutokea pale huku asijue nini afanye kwa wakati ule.Kwa upande wa mjomba alijikuta naye akishangaa,lakini lengo lake ilikua nikujitoa ili Faluu hasijue kitu chochote.

‘’Mjomba nini kinaendelea? Mbona mimi sielewi mjomba wangu?’’ Faluu aliuliza.

(Huku akisita,mjomba aliongea)

‘’Aaah..aah..! hata mimi sielewi mjomba wangu,lakini usijali sawa’’Mjomba aliongea.

Baada ya maneno yale Faluu aliishia kuguna tu na baadae alitoka nje..,Wakati akitoka nje Mjomba wake alishtuka na ghafla aliongea..

‘’Faluu unaenda wapi huko? Njoo nikuoneshe chumba chako huku’’ aliongea mjomba

‘’Hamna mjomba nilikua nataka niangalie tu huku’’ alijibu Faluu.

‘’Hapana usiende huko,njoo kwanza huku’’ aliongea mjomba na baadae Faluu ilibidi amsikilize mjomba na hivyo alirudi na kumfata mjomba wake.

Mjomba alienda kumuonesha chumba chake na sehemu mbali mbali katika ile nyumba,ilikua ni nyumba kubwa sana iliyokua nan a vyumba vingi,lakini mazingira ya nyumba ile yalimshtua sana na kumfanya kua na maswali mengi..

‘’Mjomba mbona kama kuko kimya,wengine wako wapi?’’ Faluu aliuliza

(Mjomba alishtuka)

‘’Mmmh!!.., hamna mjomba wangu,hapa nipo pekee yangu wengine wamesafiri kidogo” Mjomba aliongea..

Baada ya kupewa maelezo yale Faluu alikubali na baadae aliingia ndani kwake kupumzika,wakati akiingia ndani kupumzika ilikua ni saa tisa usiku.Alimuacha mjomba wake akiwa amekaa Sebuleni ,Wakati akiwa amelala ndani alianza kuota kama nyumba inaungua na katikati ya moto ule alimuona mama yake akiwa anaungua katika ule moto huku akitaja jina la Faluu..

‘’Faluu…!Faluu mwanangu …Mwanangu haya ndiyo maisha ya mama yako,kikubwa tulia mwanangu ili uyafikie mafanikio’’aliongea mama katika ndoto na baadae aliteteketea kabisa katika ule moto.

(Faluu alishtuka)

‘’MA…MA….MAMA!! MAMA..!!’’ Aliongea Faluu na ghafla mapigo ya moyo yalibadirika na Jasho lilianza akajikuta akimkumbuka sana mama yake

(Huku machozi yakimtoka aliongea)

‘’Mama inakuaje unaondoka na kuniacha mimi katika mazingira kama haya mama,embu angalia sasa mwanao ninavyoishi mama yangu..hiiihiii, Nakukumbuka sana mama,sijui hata niseme nini mama …’’Aliongea Faluu huku machozi yakimtoka na kutokana na ndoto ile alijikuta usingizi na uchovu ukimuisha nakumfanya aamke na kusongwa na mawazo sana katika akili yake.

Asubuhi ilipofika Mjomba waliamka wote na mjomba alimfata katika chumba chake kumjulia hali.

‘’Faluu mjomba salama’’ Mjomba wake Faluu aliongea

‘’Mimi mzima mjomba,shikamoo’’ alijibu Faluu.

‘’Marahaba,lakini mbona kama leo hujalala wewe’’aliongea mjomba

‘’Hamna mjomba…. Mmh….,niko salama lakini’’alijibu Faluu na mjomba alibaki kumtazama tu.

Baada ya muda mjomba alimuita tena ili ampe maagizo,

‘’Sasa mjomba Faluu,mimi nataka nitoke,lakini si unajua tupo wawili tu humu ndani,utaangalia pesa nimeacha pale juu ya kabati kama shilingi 2000,utaenda kununua mboga na utapika’’ aliongea mjomba.

(Faluu hakulipenda lile swala)

‘’ Mmh,sawa mjomba nitafanya hivyo,ila sijui mazingira ya huko unakonunua’’alijibu Faluu

‘’Mbona kama unaguna au haujaridhika? ” mjomba aliuliza.

‘’Aaah,hamna mjomba niko sawa’’ alijibu Faluu.

‘’Basi  sawa,ila kuhusu maelekezo ya eneo la soko,kuna mtu atakuja kukuelekeza sawa’’ alijibu mjomba Na kisha akaondoka..

‘’Kuna mtu atakuja kunielekeza?mtu gani huyo?’’ Faluu alijiuliza, Wakati akiwa anajiuliza alisikia sauti ya mtu akitembea mule ndani na wakati akigeuka alishtuka kwa maana alikua ni mtu mmoja mfupi sana,baada ya kumuona mwili wake ulisisimka sana…

‘’Na wewe nani?’’Faluu aliuliza

(Huku akicheka,yule mtu alijibu)

‘’Hahahahahhaha, unauliza mimi nani?, mimi ndiye natakiwa nikuulize wewe,ila kwa kua huu si muda wa maswali na majibu tuyaache maswali,nimeagizwa nikusindikize sokoni ukanunue mboga’’yule mtu aliongea.

Wakati yule mtu akiongea,sauti yake ilipelekea mtikisiko mkubwa sana wa ile nyumba na kumfanya Faluu kuishiwa maswali na badala yake ndiye alikua wa kwanza kutangulia mbele kutokana na uwoga aliokua nao..

“Twende sasa mbona unabaki nyuma?”aliongea Faluu

Baada ya yule mtu kusikia hivyo alitoka na baade waliambatana wote kwenda sokoni kununua hizo mboga,walipokua barabarani watu waliomuona Faluu walikua wakimshangaa na kuulizana maswali ya kwanini yule kijana kafatana na yule mtu..

‘’ Jamani yule kijana ni nani? Na mbona kafatana na yule mfanyakazi wa yule mzee Kachali? Au ndio mfanyakazi mpya nini? Na mbona anamtumikisha kijana mdogo hivyo” mama mmoja alijikuta akiwauliza wenziye maswali mengi  yaliyokosa majibu kwa masikitiko maakubwa.

‘’Mmmh! Na wewe unatuuliza maswali hayo wakati unajua kila kitu bhana,sisi tuko wote hapa halafu unatuuliza’’alijibu mama mmoja,Wenziye walimcheka sana yule mama ,kutokana na maswali yake,

(Kwa aibu yule mama alijibu)

‘’Jamani ndio mmeamua kuanzisha mjadala hapo,mimi nimeongea tu,kama maswali yangu yamewakela naomba mnisamehe’’ Yule mama alijibu na baadaye aliondoka katika eneo lile huku wale wakina mama wenzie wakiendelea kucheka.

‘’Watu wengine bhana,sasa sisi kucheka ndio tumemfukuza?,maswali gani haya anatuuliza sisi,kwanini asimuulize mumewake?’’mama mmoja aliongea pale..

(Wenzake kwa pamoja walimjibu)

‘’Acha naye huyo’’na baadaye waliendelea na maongezi yao.

Baada ya pale Faluu alienda na yule Mtu aliyepewa amsindikize mpaka katika bucha ya Nyama ili kwanza ajue mahali atakapotakiwa kupata huduma hiyo nan i huduma gani,

‘’Haya kijana mahali penyewe ndio hapa’’aliongea yule mtu.

‘’Mbona kama hii ni Bucha?’’Faluu aliuliza

‘’Ndiyo ni Bucha na ndio sehemu tunayonunua vitu vyetu’’alijibu.Baada ya kuangalia angalia,mazingira ya ile Bucha yalimfanya Faluu kupata wasi wasi kidogo na hivyo kumfanya kushindwa kuelewa..

‘’Mmmh,ndiyo Bucha yenu?kwa maana hiyo ndiyo sehemu mnayonunulia mboga zenu’’Faluu aliuliza .

“Ndiyo bhana aah!’’yule mtu alikasirika.

‘’Oyaa! Tunaomba mboga zetu,tupatie za shilingi 3000’’ yule mtu aliongea..

‘’Mboga zetu?? Mbona sikuelewi?’’Aliongea Faluu na alijikuta yale maneno yakizidi kumchanganya na kumuacha yule mtu afanye vile anavyotaka ,

‘’Haya bhana,basi fanya hivyo’’aliongea Faluu.Baaada ya kuongea vile,yule mtu alipima nyama. Wakati akipima ile nyama,Faluu alishtuka sana Baada ya kuiona ile nyama katika ule mzani kwa namna ilivyokua ikionekana..

‘’Mmmh!nyama gani hii,mbona kama haileweki?’’ alikua akiifikiria huku macho yote akiyaelekeza mahali ilipokuwepo.

‘’Wewe kijana mbona unaona sana? Kuna tatizo?’’ yule muuza nyama aliuliza.

‘’Aaah,hamna tatizo,ila naomba kujua,ni nyama gani hii?maana sijawahi kuiona’’ Faluu aliuliza pale.

‘’Mbona unakua na haraka hivyo utajua tu’’Yule muuza nyama alimjibu.

Baada ya pale Faluu hakua na maswali tena,mwisho wa siku yule muuzaji aliitoa ile nyama na Faluu alitoa hela huku na kupokea ile nyama na baadaye walirudi nyumbani. Ile nyama ilikua mchanganyiko wa steki na mifupa mifupa.Walipofika nyumbani yule mtu aliyepewa amuelekeze,alimpa maelezo pale juu ya nini anatakiwa aweke wakati anapika ile nyama.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
61 Nyumba ya Wachawi Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni