Notifications
  • MY DIARY (32)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA MBILITULIPOISHIA...Lakini kuchepuka kwangu na kuingia mgombani haikumaanisha kuwa sheria ingeniacha hivi hivi.Ilifika mahali ikabidi nizime gari na kutulia tulii kusikilizia nini kitafuata.Tayari nilikuwa nimezungukwa na mapolisi ambao walikuwa wakinifuatilia kwa kutumia pikipiki.Kwa bahati nzuri dereva wa lile gari na yeye alishafika hapo na alishawaambia polisi kuwa mimi naugua ukichaa na nilifufuka kutoka mochwari.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA…
  • MY DIARY (31)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA MOJATULIPOISHIA...“marehemu pia alinieleza kuwa ana miliki duka la vitu vya urembo wa kike ambalo pia Leah analisimamia ila hilo apewe mdogo wake Marry ambaye yupo hapa. Mama mdogo huyo mara baada ya kuyasema hayo alikaa zake chini. Baba mdogo ambaye hakurizika na maelezo hayo alisimama na kusema “kwa hiyo kama marehemu alijua kuwa atakufa hivi karibuni kwani nini hakufuata taratibu za kisheria za kuandika wosia na kurithisha mali.IKIWA UNASOMA…
  • MY DIARY (30)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINITULIPOISHIA...Baada ya hapo Nnilimwomba mama mdogo ajikaze na kuwatarifu ndugu wengine habari hizo za msiba.Tulisaidiana hivyo hivyo maana sio siri kila mmoja alikuwa na uchungu sana kutokana na mazingira ya kifo hicho. Habari zilizidi kusambaa kwa kasi na majirani walianza kukusanyika hapo kwa mama mdogo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Msiba ni msiba tu na ukitaka kujua binadamu…
  • MY DIARY (29)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TISATULIPOISHIA...Hapo sasa nikazidi kuchanganyikiwa ikabidi nimuulize mama huyo alikuwa akifanyia shughuli zake za kujipatia kipato sehemu gani.? Yule dada akanambia kuwa anafanyia soko la ndizi huko Korongoni. Sikuwa na jinsi nilimuomba anipeleke lakini na yeye alisita sita kwa madai kuwa alikuwa na kazi nyingi za kufanya na bado anatakiwa ampeleke mtoto shule.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (28)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NANETULIPOISHIA...Sisi tumesomea mambo haya bhana waliendela kuzungumza wale walinzi huku wakishuka ngazi kwa polepole. Hapo na mimi nikawa nimejifunza kitu kuwa kumbe unaweza kuingia na mtu guest akakuzuru kisha akaondoka zake.Sasa sijui kwenye zile guest zetu za uswahilini kama wanalijua hili.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi nilala japo usingizi ulikuwa hautaki kuja kwa…
  • MY DIARY (27)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SABATULIPOISHIA...Alinamba eti hayo ya mimi kuolewa tuyaeke pembeni na kwa nini siku hiyo nisilale Moshi tukumbushie enzi zetu. Mwalimu John aliendelea kusema kuwa amenimiss sana na anomba nisahu yaliyopita na turudie yale maisha yetu ya zamani.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijifanya simwelewi lakini ukweli ni kwamba nyota ya mwanaume huyu ilikuwa ni kali sana zaidi yangu na…
  • MY DIARY (26)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SITATULIPOISHIA...Joyce alinambia yeye haendi kujipanga foleni kama makahaba wengine hivyo yeye hufanya biashara hiyo kitaalamu zaidi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alisistiza pia kuwa eti huwa anatumia kinga kuwakinga wengine. Wakati mwingine alinambia acha awaambukize kwa sababu wanaume wangekuwa na akili basi wasingeenda kununua mwanamke. Anasema kuwa laiti biashara hiyo…
  • MY DIARY (25)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TANOTULIPOISHIA...Sikuisha hapo pia nilimpongeza kwa kunijali na kunipenda na kuhakisha kuwa siingii kwenye majanga kama yake mara baada ya kutoka jela. Siku hiyo nilimuelewa sana Joyce na nilikuwa tayari kumsapoti kwa lolote ili mradi tu atimize athma yake hiyo ya kuzaa. Tuliongea mengi sana na baadaye alinionesha picha ya mtu ambaye alitaka kuzaa naye.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (24)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NNETULIPOISHIA...Kwa kweli siku hiyo niliwaza sana na kutafakri vitu vingi. Wale wanachuo wenzangu wamenambia kuwa Msouth alikuwa kwa kimada mwingine na japo stori haikumalizikia ila ukweli ni kwamba alifumaniwa na kupigwa vibaya na huenda walimtupa mahali na ndio maana chanzo cha kifo chake hakieleweki.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijaribu kuijikontrol ili nisiwaze kitu…
  • MY DIARY (23)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TATUTULIPOISHIA...Alinisihi sana nisitoe niilee na yeye atatoa huduma zote lakini tuendelee kufanya siri ili tusije tukahatarisha ndoa yake na kusababisha familia yake kuyumba. Kwa kweli sikuweza maana ilikuwa ni kujipa tabu mimi na huyo mtoto atakayezaliwa. Bora ataa ingekuwa ni mimba ya ule mwalimu ambaye hajaoa.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilitamani nimchomekee hiyo mimba…

Nyumba ya Wachawi (6)

Mtunzi: Denis Benard

SEHEMU YA SITA
TULIPOISHIA...
Baada ya pale Faluu hakua na maswali tena,mwisho wa siku yule muuzaji aliitoa ile nyama na Faluu alitoa hela huku na kupokea ile nyama na baadaye walirudi nyumbani. Ile nyama ilikua mchanganyiko wa steki na mifupa mifupa.Walipofika nyumbani yule mtu aliyepewa amuelekeze,alimpa maelezo pale juu ya nini anatakiwa aweke wakati anapika ile nyama.

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
‘’Wewe!! Sikia hiyo nyama hatuweki viungo vyovyote,nisikie wewe,usiweke nyanya wala kitunguu chochote,huwa tunakula hivyo hivyo’’aliongea yule mtu huku akitokwa na udenda kutokana na uchu aliokua nao.

‘’Mbona kama mimi siwaelewi?? Embu nipe maelezo yakutosha ili mimi nikuelewe,sikuelewi kabisa’’Faluu aliongea huku kichwa chake kikionekana kujaa maji.

‘’Sikia hakuna maelezo mengine zaidi ya hayo,chemsha hiyo nyama na usiweke kiungo chochote,hiyo huwa tunakula hivyo hivyo na hayo ndiyo maelekezo yangu ninayoweza kukupa zaidi ya hapo mimi sijui’’ alijibu yule mtu.

‘’Bado mimi sijakuelewa hapa kabisa’’aliongea Faluu

‘’Utajua mwenyewe,ila kikubwa fanya hivyo ,mengine utakuja kumuuliza mjomba wako sawa’’ aliongea yule na kuondoka.Wakati anaondoka ulitokea upepo kidogo na pasipo kutarajia yule mtu aliingia katika korido moja  na ghafla kulikua kimya katika eneo lile.

‘’Mmmh,mbona kama mimi sielewi?,hivi usalama upo humu ndani kweli? Haya mambo vipi?’’

aljiuliza Faluu na baadaye aliona apike kama jinsi alivyopata maelekezo kutoka kwa mwenyeji wake.

Baada ya hapo,Faluu alianza kupika ile nyama huku akiitafakari sana na wakati huo alikua na njaa sana kutokana na safari na pia likua hajaweka kitu chochote katika tumbo lake,hivyo masaa yalizidi kusonga.Ilipofika saa 6 mchana,baada ya njaa kuzidi aliamua kupakua ile nyama bila kujali ni nyama gani ilikupoza njaa yake,alipotaka tu kuiweka mdomoni,aliisikia sauti ya mtu ikimueleza..

‘’Wewe hiyo nyama huwa hatuli kizembe hivyo,embu acha!’’Alishtuka na kuanguka chini na mara alipogeuka nyuma alimuona yule mtu aliyekua akimuelekeza …Jambo lile lilimstahajabisha sana.

Baada ya hapo,Faluu alianza kupika ile nyama huku akiitafakari sana na wakati huo alikua na njaa sana kutokana na safari na pia likua hajaweka kitu chochote katika tumbo lake,hivyo masaa yalizidi kusonga.Ilipofika saa 6 mchana,baada ya njaa kuzidi aliamua kupakua ile nyama bila kujali ni nyama gani ilikupoza njaa yake,alipotaka tu kuiweka mdomoni,aliisikia sauti ya mtu ikimueleza..

‘’Wewe hiyo nyama huwa hatuli kizembe hivyo,embu acha!’’Alishtuka na kuanguka chini na mara alipogeuka nyuma alimuona yule mtu aliyekua akimuelekeza …Jambo lile lilimstahajabisha sana.

‘’Kwani wewe ulikua wapi?’’Faluu alimuuliza

‘’Acha maswali yako ya kejeli,kwani wewe haukuniona?mbona nilikua hapa hapa’’Yule mtu aliongea huku akicheka.Swala lile lilimpa shida sana

‘’Ulikua hapa hapa ?kwani mimi ningekuona ningekuuliza?’’aliongea Faluu.

‘’Basi ndio hivyo’’alijibu yule mtu..

Wakati wakijibishana alitokea mjomba wake Faluu (Kachali)..

‘’Vipi mbona mnabishana?kulikoni?’’ aliuliza Mjomba.

‘’Aaah,hamna mjomba tunaongea tu hapa’’ Faluu alijibu.

‘’Halafu mjomba mimi nahisi njaa sana,naoma nifanye utaratibu’’aliongea Faluu

(Mjomba alicheka sana)

‘’Hahahahah,mjomba hapa sisi huwatunakula maramoja tu tena usiku,kwa hiyo subiri sawa’’mjomba alijibu.Majiu yale yalimshtua sana Faluu..

‘’Nisubiri hadi usiku?sawa’’alijiongelea Faluu na baadae alitulia tuli.Masaa yalizidi kusonga ilipofika saa mbili usiku walianza kuandaa chakula na kupeleka katika chumba kimoja kilichokua ndani ya hiyo nyumba,jambo lile lilimfanya Faluu azidi kujiuliza maswali juu ya mazingira halisi ya ile nyumba,

‘’Mjomba na hiki chumba vipi?’’aliuliza Faluu

‘’Humu ndani ndio tunakolia chakula’’alijibu Mjomba.

‘’Mbona giza sana?tunafanyaje’’aliongea Faluu..

‘’Hamna kukosawa tu  na mbona ndani kukosafi’’aliongea mjomba..Wakati Faluu akiwa nje alianza kusikia sauti za watu wakiongea ongea mule ndani,sauti zile zilimuogopesha sana na kumfanya kua na hofu,aliogopa sana na kujikuta akisita kuingia mule ndani…

(Mjomba aligeuka nyuma na kumuangalia)

‘’Mbona unasita?embu ingia ndani’’ Aliongea Mjomba na baadae alirudi na kumshika mkono na kuingia ndani.Faluu aliishia kuguna tu na walipoingia ndani kulikua kimya tu na hakukua na mtu yoyote zaidi ya mjomba na yule mtu aliyekua akimuelekeza namna ya kupika ile nyama.

Faluu alibaki kushangaa mazingira ya mule,kwa maana yalikua yametapakaa na michoro ya ajabu ajabu yenye kutisha ambayo ilimfaya Faluu ashindwe kuvumilia..

‘’Mjomba mbona kama mimi sielewi humu ndani kwa jinsi mlivyo? Embu naomba uniambie basi mjomba wangu’’ aliongea Faluu

Kabla mjomba hajajibu kitu chochote juu ya swali alilouliza Faluu,yule mtu aliyekua karibu alisimama na kuongea..

‘’Sikia Faluu huu sio muda wakumuuliza mkuu maswali,embu leta chakula tule hapa hayo maswali baadae’’ aliongea huyo mtu huku akiwa ametoaa macho yake. Mambo yale yalizidi sana kumchanganya Faluu na baada ya mambo yale mjomba wake Faluu alicheka sana na kwa sauti ya kuunguruma aliongea..

‘’Embu nenda ukalete mara moja kama ulivyoelekezwa kule ‘’ aliongea mjomba, maneno yale yaliyokua yakiongelewa yalimfanya Faluu ashindwe cha kufanya maana hakujua wanachomaanisha…Ama kweli kila jambo na mtu wake

‘’Mbona mnanichanganya sasa eti mjomba na wewe baba,sikilizeni sasa!! Mimi siwaelewi kabisa ‘’ Aliongea Faluu kwa ujasiri mkubwa sana.

Walibaki wakimtolea macho tu wasijue nini cha kumueleza Faluu kwa muda ule na wakati huo masaa yalizidi kusonga na ilipofika saa 7 usiku,ghafla Mjomba alianza kucheka kwa sauti tofauti tofauti za kutisha sana,ambazo zilimfanya Faluu kuanza kua muoga na muda muda huohuo kulitokea upepo mkali sana mle na alipogeuka nyuma  hakumuona yule mtu mwingine,alijikuta mwili mzima ukitetemeka na kujikuta akishindwa kuongea,ndipo alipojivuta mpaka pale alipokuwepo mjomba wake akiwa anatembelea magoti maana hakuwa na nguvu za kutembea kutokana na miguu yake kuishiwa nguvu.Alimshika bega mjomba wake na mara mjomba alipogeuka doooh!! Sura yake yote ilikua imejaa vidonda hali ile ilimshtua na kujikuta akipata nguvu na kusimama  na kukimbilia mlangoni na alipofika mlangoni kufungua mlango ili atoke nje,mlango haukufunguka ndipo akajikuta akiongea maneno haya kwa ghadhabu..

‘’Sasa mambo gani haya,mbona unafanya vitu kama mtoto mdogo mjomba wangu?’’aliongea Faluu na hakuna mtu yeyote aliyemjibu na muda mfupi baadae alianza kuona watu waajabu wakitokea katika pembe za kile chumba…

Baada ya Faluu kuona vitu vile alianza kurudi nyuma na ghafla alijikuta akimgonga mjomba wake,alipogeuka na kumuona alikutana na kundi kubwa sana la watu wenye maumbile na sura tofauti tofauti,nguvu zilimuisha na pale pale alipoteza fahamu.

‘’Hii nyama tena bado laini kabisa’’aliongea kiumbe mmoja.

(Mjomba wake alishtuka kusikia vile)

‘’Hapana huyu mwanangu sikumleta huku kwaajili ya kazi hiyo’’ aliongea mjomba wake Faluu

‘’Unamsaidia sio” waliongea wale viumbe huku wakionekana kukasirika

‘’Hapana mimi simsaidii,lakini mnasahau kama nyie ndiyo mlio muua mama yake ?huyu pwa wangu nimemleta kwaajili ya kazi nyingine kabisa tulieni’’aliongea Mjomba wake Faluu na kwa vile ndiye aliyekua kiongozi wote walimsikiliza na baada ya pale walikula zile nyama na ilipofika saa 11 alfajiri walipotea katika mazingira yale.

Faluu alikaa muda mrefu sana akiwa amepoteza fahamu,hasa ni kutokana na njaa iliyosababishwa na kukaa muda mrefu bila kula.Ilipofika saa 4 asubuhi  Faluu alishtuka na alijikuta akiwa katika kile chumba ,Moyo wake ulizidi kuingiwa na hofu bila kujua hatima ya matatizo yake.

‘’Mungu wangu haya yanayotokea kwenye maisha yangu ni kitu gani?mbona mimi sielewi jamani? Et Mungu nijibu basi” Faluu alikua akijiongelea.

  Alikua akijiongelea huku machozi yakimtoka na wakati mgumu sana Katika kipindi hicho,baada ya muda wa dakika kadhaa alikuja mjomba wake huku akiwa anatabasamu..

‘’Aaaah, mjomba umeamka,daah pole sana’’ aliongea mjomba wake.Wakati mjomba akiongea Faluu alikua akimtazama huku sura yake ikionekana kua na hasira sana..

‘’Samahani mjomba,hivi unaweza kuniruhusu nikuulize swali?’’ Faluu aliongea

‘’Hahahah,usiogope mpwa wangu wewe uliza tu’’ Mjomba alijibu huku akiwa anacheka.Kicheko cha mjomba kilimpa hasira sana Faluu,maana alijiona kama mjomba anamdharau,ila kwake aliona muda ule siyo sahihi kuonesha anachofikiria.

‘’Hivi mjomba maana halisi ya wewe kuniambia niingie mule ndani nini hasa na mbona unanifanyia mambo ya ajabu? Na wale watu waajabu walikua akina nani?’’Faluu aliuliza maswali huku akionekana kua na mambo mengi sana.

Wakati mjomba akitaka kumjibu ghafla alitokea yule mtu ambaye jana alikua anamuelekeza kupika na kutengeneza ile nyama,Faluu alishtuka sana na kujikuta akijiuliza maswali mengi sana katika ufahamu wake..

‘’Hivi huyu mtu ni nani? Na ,mbona ninapokua naongea na mjomba wangu na kumuuliza maswali anapotaka tu kunijibu anatokea na kunuiletea ubabe,ngoja nimuone atakachoniambia leo’’ Faluu alikua akifikiria.

Alipoinua macho yake na kumtazama yule mtu akiwa amesimama pembeni ya mjomba wake,yule alikua akimuona kwa macho ya hasira sana na Faluu aliogopa sana..

‘’Wewe Faluu vipi,embu simama hapa na uondoke na usipende sana kumuuliza mjomba wako maswali sawa,yasije yakakutokea puani’’Yule mtu aliongea

Faluu aliogopa ,ila kila alipokua akitaka kusimama alijikuta akianguka,alijaribu mara kadhaa lakini alishindwa kutokana na njaa.

‘’Mjomba mimi nashindwa kusimama,tumbo na njaa inauma sana,naomba unisaidie mjomba wangu’’Faluu aliongea.

Kutokana na Faluu kupata shida ile,Mjomba wake alimuonea huruma sana mpwa wake,kwasababu ata yeye aliamini motto wa dada yake ana muda mrefu hajakula..

‘’Wewe Mfupa embu kamnunulie Faluu chakula kwa huyo mama hapo nje’’ Mjomba wake Faluu alimuagiza yule mtu (Mfupa)..

‘’Hamna mzee,kuna ile nyama ilibaki jana humu,kwanini tusimpe tu hii’’ Mfupa aliongea

‘’Hapana hawezi kula ile nyama,kamnunulie chakula mimi nasema’’Aliongea mjomba wake Faluu.

‘’Aaah,wewe unasema kwa sababu ni motto wa dada yako siyo,haya naenda kumnulilia ila tutaona’’Mfupa aliongea.

‘’Nitaona nini sasa,wewe nenda kalete hicho chakula tu,mengine achana nayo’’ Aliongea mjomba huku akicheka kwa dhalau.

Wakati mvutano ukiendelea Faluu alikua akiwashangaa tu huku akishindwa aongee nini,

‘’Mjomba usijali kwa kila kitu kinachoendelea humu,kikuwa naomba uzoee sawa na usiwe na wasiwasi kabisa,amini kua huko nyumbani kwa mjomba wako’’ Mjomba wake Faluu aliongea.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
61 Nyumba ya Wachawi Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni