MZOA TAKA (1)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA KWANZA
“Hallo halloo utajijuu tena mimi ndio Mwajei ukisikia mwengine basi ujuwe photo copy bibi ehee... utaisoma number mwaka huu unajisifu unambio msifu na
anae kukimbiza bibi wewe!" ni maneno yaliyo toka kinywani kwa binti mmoja hivi kashombe shombe bila shaka kanywa pombe. Mwembamba, kama ujuavyo
Wanawake wembamba kwa kuongea hawajambo tatizo nguvu ndio hawana. "Oyaa Mwajuma kuna nini hapa mbona unapayuka bila mpango?" Nikawa kama
nimechokoza nyuki vile
“ehee na wewe kifaurongo nilikuwa nakungojea kwa hamu tu nikupe vipande vyako!"
Nikamuuliza
"vipande gani tena dada yangu?"
“tabia ya kukaa kule kijiweni kwenu na kuanza kujisifia unatoka na mimi kimapenzi ukome tena wewe,"
“kwani Mwajei nani amekwambia mimi najitangazia hivyo?"
“Eti natoka na Mwajei pumbavu zako hivi ushaona hii shepu ya kutoka na wazoa taka kama wewe wakati kidudu chenyewe kibamia nikipiga chafya tu kinachomoka!"
dahaa ni bonge la dharau kinyama yani nikabaki kumtolea macho tu jinsi anavyo nichamba huku akitingisha vikalio vyake kama pasi ya mkaa yani akienda kama
anarudi mdomo umemkaukaa kama kanywa maji ya betri vile sura ngumuu kapaka wanja mpaka nyuma ya sikio yani wee acha tu arafu anajisifu bonge la demu
mmh! nikaona isiwe shida nikasukumiza mkokoteni wangu huyoo mpaka ninapo upaki kwakuwa kazi ya kusomba taka tayari nilikuwa nishamaliza. Na kupata
pesa kidogo, nikarudi zangu getto kufika tu vicheko vya kishambenga vikaanza "hahaha,,..",hahahaha mama Khadija umemuona?" “kumuona nani tena
mwenzangu?" “ahaaa wee hujui kwani?"
“ahaaa kumbe yule mnuka uvundo”
“kumbe umemuona eheee yani nnzi wote wanamfata yeye!"
"lakini sio vizuri kumcheka kaka wawatu wakati ile ndio kazi yake"
"ohooo wee nae hayakuhusu fata yako hapa naongea na shoga zangu umesikia nenda kapike huko ni maneno ya Mama mwenye nyumba sio siri ananiponda
vibaya sana mpaka nikatamani kuhama kwenye nyumba yake tatizo kwake chumba ndio bei rahisi yani kodi kwa mwezi ni tsh.20000 tu japo hakina umeme ndio
kwaanza nimetoka kijijini kwetu njombe mkoani iringa kuja kusaka maisha town nikafikia kwa jamaa yangu flani hivi kusema kwer nilipofika tu alinipokea
vizuri kwa mikono miwili baada kukaa nae miezi kazaa akaanza visa vya kiboya kwa kuja na mademu na kulala nao ndani mimi nalala nnje mpaka hasubuhi
Nikawa nalala nnje bila kujifunika chochote kile baridi langu mmbu wangu lakini ndio maisha nitafanyaje na nimekuja town kusaka life basi nakumbuka siku
moja nikiwa naosha vyombo akaja na kuinyanyua sufuria ambayo nimeweka miukoko akanimiminia kichwani kisha akanibamiza nayo kichwani huku
akinitukana "malaya wewe mtoto wa mmbwa kudadeki zako naomba pesa yangu uliyo ichukuwa mule ndani huku damu zikinivuja nikamuuliza "pesa ipi kaka
Sele?" unajifanya hujui sio ehee pesa yangu niliiweka chini ya kapeti pale K***mako nipe lasivyo ntakuuwa ohooo nikaona uboya huu pesa sijachukua
kunipasua na sufuria kanipasua afu tena ananitukania mama yangu nikainuka kwa kasi ya ajabu nikamtwanga kichwa nazani hakutegemea mimi kufanya vile
akaenda chini puhu akanyanyuka huku akiwa kafura kwa hasira tatizo uwezo wake mdogo tokea tukiwa wadogo kijijini nilikuwa namdunda tu watu wakajazana
kuja kutuamulia kuna mshkaji anaitwa madebe akasema "oyaa wee Sele yani kumuhifadhi jamaa yako ndio unamnyanyasa hivi ndugu huo uboya kwanza hiyo
pesa unayo sema kachukua si ulimpa demu wako kule unazani hatujakuona ukamwambia akaushe au?" kama umemchoka mwambie ukwer sio kumletea visa vya
kishamba oya boy kama vipi huyu mshamba asikutishe wala nini yeye mwenyewe wa kuja tu!! kaja hapa town michongo yote tumempa sisi leo kinajifanya
kidume embu chukua nguo zako boy tukakae maghetoni wanaume Siku zote twapeana compani leo kwake kesho kwako au sio masera,?" ndio kaka hapo umechonga nikazama ghetto na kuchukuwa nguo zangu kwa kuziweka kwenye kimfuko cha Rambo nikatoka na washkaji huku nikimuacha Sele analia takribani
miezi mitatu Salumu mie nikawa mzoa takataka ninae julikana tandika temeke mtongani yote walinifahamu kwa utendaji wa kazi yangu kidogo nikipatacho
nakigawa na kukituma kwa wazazi kijijini wakazidi kuniombea baraka niweze kufanikiwa katika maisha sasa leo nyumba niliyo panga nachekwa na wapangaji
hadi mama mwenye nyumba mtetezi wangu ni mmoja tu mtoto wa mama mwenye nyumba anaekwenda kwa jina la Mwanaidi binafsi alitokea kunikubar sana na
kuweza kuniletea chakula pasipo mama yake kutambua
basi baada kutoka kuoga nikiwa napita ndipo nikamsikia mpangaji mmoja wapo anaekwenda kwa jina Hidaya akisema humo chooni kuna nukaje itabidi
umwambie akapige deki, mmh mwambie wewe mi naogopa asije akaninasa mabao hapa," wee hivi unanisikia au unaniangaria kwa oga anipige aone ndipo
atakapo mtambua baba Mudy siku hiyo
nikiwa nazama gheto kwangu nikagongana na mwanaidi akiwa kajifunga kanga moko tu bira shaka nae anaenda kuoga kanga ikamdondoka na kubaki na chupi tu
jamani!!!
Kitendo cha mwanaidi kanga kumdondoka nikaweza kushuhudia dodo zake zilizo chongoka kifuani kwake ndipo akaiyokota kanga faster na kujifunga kwani
tuliweza kumsikia mama yake akinyanyuka huku akisema "ngojea nikakuletee hiyo pesa yako na leo ndio namaliza deni, nikazama chumbani kwangu huku
mwanaidi akitoka nnje na ndoo yake ya maji akaitwa na mmoja wawapangaji "wee mwanaidi,' abee dada, huko chooni kuna nuka uvundo ndugu yangu, "kwanini
kunanuka uvundo?" si kaingia yule mzoa takataka,' kitendo kile mwanaidi hakikupenda hata chembe akatoka chooni na kuanza kumtukana yule Dada "sikia wee
malaya usiekuwa na haya mshenzi wewe lione sura mbayaa kama tako la sokwe uso umekupauka kama mnywa gongo tabia ya kumsema sema kaka wawatu sijui
mnuka uvundo au mnuka kikwapa ukome tena kama ulivyo likoma ziwa la mama yako si akataka kumvaa ikabidi mama yake amzuie na kumwambia "mwanaidi
mwanangu acha basi yaishe ndipo akaenda kuoga "hivi mama mwanaidi mwanao kapewa nini na huyu mkaka mbona anamtetea hivi?" hata sijui mwenzangu, sasa
ipo siku nitamfumua mwanao hapa nimemkaushia kutokana na heshima yako tu vinginevyo ningemdunda vibaya sana,' mmh hivi wewe unamjuwa mwanaidi au
unamsikia ukitaka habari zake mtafute Mwajuma akwambie kitaa hiki chote wanamsoma usimuone mpore vile mashetani yake yakipanda hadi mama yake
anatoka nduki kama yule kaka ndio anatetewa na mwanaidi mimi simo kabsaa
baada kupita siku tatu nikiwa nimekaa kijiweni njaa nayo inaniuma dahaa yani siku hiyo sikuweza kuambulia chochote taka taka zote zilibebwa na gari ya manispaa ya temeke nikawa napiga miyaoo tu "aaam dahaa ndipo nikaweza kumshuhudia binti mrembo wa haja mfano wa Jacklin wolper akipita mbele yangu
viatu vya mchuchumio kapiga jeanse aina ya moder imemuwamba na kuweza kuonyesha hipsi zake za maana kapiga top iliyoweza kuacha kitovu chake kiasi
shingoni ana cheni na mikufu ya dhahabu na silver kichwani ananywele zilizo mfika hadi mgongoni sijui zake au wigi mi sijui kwa bahati mbaya akadondosha
kipochi ambacho kilitoka kwenye kimkoba alicho kibeba
nikaenda faster kukiokota na kukisunda ndipo nikakumbuka kauli ya mama akiniambia siku moja "mwanangu kipenzi Salumu usije ukathubutu kumuibia mtu
kitu chake, au kuzurumu cha mtu kama ukaokota kitu na ukamjuwa mwenyewe ni nani basi mpelekee ukifanya hivyo itakuwa vizuri zaidi huenda MWENYEZI
MUNGU akafungua milango ya riziki"
Baada kauli ile kuikumbuka nikajikuta namkimbilia yule Dada na kumkuta ndio anafunguliwa geti aingie ndani nikamwita "sister samahani, akanitizama juu
hadi chini kisha kwa dharau akatema mate chini
Yule aliyemfungulia Geti ni mtoto wa kiume akamwambia "Dada achana nae huyu mzoa takataka tu" akiwa anageuka kuingia ndani yani kanishit! ndipo
nikakitoa kile kipochi na kumwambia "Dada mzigo wako huu umedondosha pale" Akageuka kucheki dahaa hakuamini ikabidi apekuwe kwenye kibegi chake
hakukiona akaja mbio kukipokea kisha akakifungua kukagua hakuamini na kujikuta ananikumbatia.
Kitendo cha yule binti kuja kunikumbatia kilinifanya nipigwe na kitu kama short hivi dahaa kama haitoshi akanikiss kabisa huku akisema "shukrani sana baby
ahaa kaka kwa kuweza kuniletea mzigo wangu kwani kuna vitu vingi sana vya thamani kuna kama dollar 2000 ya kimarecan cheni zangu za dhahabu passport yangu ya kusafiria n.k sijui nikushukuru vipi embu twende ndani akanishika mkono na kunivutia kwenye mjumba wao wa kifahari dahaa Tanzania nchi masikini
ukiniambia nakataa kuna watu wana pesa wee acha tu basi nikaandaliwa msosi ambao sijawai kula tokea nizaliwe eti dagaa mboga ya masikini akila tajiri
anajenga hafya dahaa lakini nikaweza kugundua kitu kimoja ya kwamba yule kijana akawa amechukia mbaya mi kufanyiwa vile na Dada yake ila sikumjar baada
kula na kushiba ndipo akakaa tupige story mbili tatu akaniuliza "dahaa kumbe ulikuwa na njaa sana ehee?"
wee acha tu ukicheki leo mishe zimekaba mbaya kila kijiwe nikipita manispahaa wamesafisha jiji,' pole sana hivi unaitwa nani?" kwa jina naitwa Salumu salim
ndio jina nililopewa na wazazi wangu,' oky unajina zuri sana yani doubre S mimi kwa jina naitwa Joyce Joseph,' khaa kumbe nawe doubre J kweli noma baada
kuzungumza na kupiga story sana tu ndipo akanipa bahasha rangi ya kaki nikawa nasita kuipokea ila akaniambia "pokea usijari bana hizi pesa kiasi cha shilling
laki 5 zitakusaidia siku mbili tatu tu ndipo nikazipokea akanipa bossiness card yake nikaaga na kuondoka zangu njia nzima nikawa nafurahi kwa kupata zali
nikawa napiga mahesabu ya kwenda kunnua godoro na kitanda na kufungua biashara hata ya genge na kulipa kodi ya chumba mwaka mzima nikiwa sina hili wala
lile nakatiza kichochoro flani hivi nikastukia napigwa roba ya mbao nikajitahidi kujitoa nipambane kiume nikafanikiwa kuitoa na kumtwanga ngumi yule jamaa
kucheki mbele kuna vidume vya shoka vinakuja kucheki huku napo wanakuja nikawa nipo kati kati si unajuwa kichochoro dahaa nikajisemea "hapa kufa na
kupona tu wakanifikia nikajitahidi kupambana lakini wakanizidi nguvu vidume v5 kwa mmoja nikapigwa bapa za mgongo nikawa nisharegea damu tu zinanivuja
kati ya vidume vile mmoja tu kavaa mask usoni wakaichukua ile bahasha na bussnes card wakasepa dahaa
sikuwa na nguvu hata ya kusimama macho yakafumba Giza totoro
sikuweza juwa kilichoendelea nikaja kustuka baada kumwagiwa kitu cha baridii nikaweza kufumbua macho yangu na kuhisi maumivu kila maeneo nikicheki pembeni nikaweza kumuona Mwanaidi akiwa ameshika bakuri na kitambaa kumbe nilikuwa nipo chumbani kwangu nimelala chini ya mkeka
KUNA MATANGAZO YANATOKEA KWENYE APPLICATION YETU HIVYO UKIYAONA NAOMBA BONYEZA HAPO NDIO UNANIPA SAPOTI MIMI, UKIBONYEZA UNAWEZA KUCANCEL SIO LAZIMA UENDELE ULIKOPELEKWA, KIKUBWA UBONYEZE HATA MARA 2-3 KILA UKIFUNGUA APP YETU
TAZAMA KICHEKESHO HIKI KISHA BONYEZA SUBSCRIBE ILIYOPO CHINI YAKE WAKATI TUKIELEKEA KWENYE MUENDELEZO

USIKOSE SEHEMU YA MBILI
Maoni, Ushauri na Chochote Share Namimi Katika Mawasiliano Haya:
+255 718 274 413 Ipo WhatsApp
+255 764 339 438
ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Maoni, Ushauri na Chochote Share Namimi Katika Mawasiliano Haya:
+255 718 274 413 Ipo WhatsApp
+255 764 339 438
ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni